Maendeleo ya CHADEMA Njombe

Hongereni sana, tutafurahi ikiwa mtatupa matokeo ya huko tuyajidili hapa na pigana msasa ili baada ya 2yrs hivi tufanye tathimi.
 
mkuu.. kazi nzuri nawatakia mafanikio mema... tukipata contacts tutakuhabarisha haraka
 
Hongereni.

Concern yangu hapa ni kama hatujaona mchango wa CDM makao makuu katika hizi jitihada. Naamini kama hizo contacts si ajabu ingekuwa rahisi kuzipata kwa ushirikiano na na uratibu kutoka makao makuu mpaka ngazi ya mkoa in this case nadhani mngehitaji kushirikiana na viongozi wa mkoa wa iringa kwani ndio mkoa wenu wa njombe ulipotokea.

Nawatakia kila la kheri
 
Kwa niaba ya M/kiti wa CDM Wilaya ya Njombe (mkoa mpya wa Njombe) napenda kuwafahamisha wapenda mabadiliko wote hasa wapenzi, wanachama, mashabiki wa CDM na wananchi kwa ujumla kwamba tunaendelea vizuri na kazi ya kusambaza moto wa mabadliko kama yalivyoasisiwa na Mh Thomas Nyimbo.
Wale wenye kumbukumbu mtakumbuka kuna siku nilileta hapa mada inayoeleza jinsi Mh. Nyimbo alivyojitolea kwa hali na mali kuwasha moto wa mabadiliko. Kwa hakika tumefanikiwa sana kwa ngazi ya jimbo la Njombe Magharibi na sasa tumeunganisha juhudi na Majimbo mengine ya Njombe kusin na Kaskazini. Kuanzia mwezi wa pili (Februari) tunatarajia kuwasha moto kuelekea LUDEWA na MAKETE kwa msaada mkubwa wa Mh. Nyimbo ili hatimaye mkoa wa Njombe uwe na nguvu kama ile ya Mwanza, Mbeya, Iringa, Arusha na Kilimanjaro.
OMBI MAALUM
Kama yupo mwanaJF anaweza kutusaidia contacts za mtu yeyote wa Makete na Ludewa tunaomba tafadhali sana atusaidie kabla ya Jumapili ya wiki hii ili tuwasiliane naye mapema iwezekanavyo. Tumefikia hatua hii baada ya jitihada zetu kuelekea kukwama. Tafadhali kama unayo namba ya mtu au watu au wewe mwenyewe tujulishe kupitia 0789149165 (M/Kiti CDM Njombe (W) au mgosa81@yahoo.com.
Tunawashukuru sana kwa support yenu

Hakuna kulala.........
Posted by Kiongozi

....kwanza nimefurahi sana kwa harakati hizo ambazo mpenda maendeleo yeyote yule lazima akubali jitihada mnazofanya kuwa zina maana kwa taifa hili! Nilisikitika sana sana eti kuona Mh.Mkinda na Deo Filikunjombe wanapita bila kupingwa? wapi Demokrasia mkoa wa Njombe? Yes, wananchi wetu Njombe wanahitaji elimu ya kutosha juu ya Demokrasia ya kweli!

Juu ya ombi lako, hapo niliopohighlight, je, unahitaji contact za mtu YEYOTE yule? hata akiwa ni adui yenu? au unataka contact za mwanaharakati wa maeneo hayo? Kuna vijana hapa kama Fidel & Teamo wanaweza saidia sana hapa....!
 
ukombozi wa kweli ni mapambano kwa vitendo km wafanyanvyo watu wa njombe wakiwa na jemedari wao Mzee Nyimbo-Hongereni sana. Keep it up!! Natamani moto huo tuwashe wilaya zote-kufungua MATAWI VIJIJI VYOTE ILI KUWEKA WENYEVITI WAKE CDM NEXT ELECTION (SERIKALI ZA MITAA)
 
....kwanza nimefurahi sana kwa harakati hizo ambazo mpenda maendeleo yeyote yule lazima akubali jitihada mnazofanya kuwa zina maana kwa taifa hili! Nilisikitika sana sana eti kuona Mh.Mkinda na Deo Filikunjombe wanapita bila kupingwa? wapi Demokrasia mkoa wa Njombe? Yes, wananchi wetu Njombe wanahitaji elimu ya kutosha juu ya Demokrasia ya kweli!

Juu ya ombi lako, hapo niliopohighlight, je, unahitaji contact za mtu YEYOTE yule? hata akiwa ni adui yenu? au unataka contact za mwanaharakati wa maeneo hayo? Kuna vijana hapa kama Fidel & Teamo wanaweza saidia sana hapa....!

Nafikiri anahitaji wanaharakati hao, sasa Fidel na Teamo contact zao angepewa kama wazijua ili awasiliane nao,au vije GERARD????
 
ni harakati za kuelimisha wananchi wazifahamu haki zao na kuzisimamia na kutekeleza wajibu wao kama watanzania katika taifa lao kwa ajili ya maendeleo

Heshima mbele mheshimiwa! Nimeona mambo ya iringa, naskia nguvu sasa umezihamishia Singida? Keep up.
 
Pia nawashauri mtoe elimu ya katiba kwa wanavijiji wote huko kupita vijana kadhaa ambao mtawapa elimu nao wawafikie watu wengi zaidi, kukumu la kuikomboa Tanganyika ni letu sote, tunafurahi wenzetu Njombe mmehamasika. Naamini kwa jitihadi hizi mikoa yote itaunga mkono. Vp wadau wa mikoa tuliyofanya vibaya kama Mtwara, Lindi, Singida n.k jamani shime tuing'oe CCM kwqa vitendo kama Njombe walivyoanza
 
....kwanza nimefurahi sana kwa harakati hizo ambazo mpenda maendeleo yeyote yule lazima akubali jitihada mnazofanya kuwa zina maana kwa taifa hili! Nilisikitika sana sana eti kuona Mh.Mkinda na Deo Filikunjombe wanapita bila kupingwa? wapi Demokrasia mkoa wa Njombe? Yes, wananchi wetu Njombe wanahitaji elimu ya kutosha juu ya Demokrasia ya kweli!

Juu ya ombi lako, hapo niliopohighlight, je, unahitaji contact za mtu YEYOTE yule? hata akiwa ni adui yenu? au unataka contact za mwanaharakati wa maeneo hayo? Kuna vijana hapa kama Fidel & Teamo wanaweza saidia sana hapa....!

....Teamo,

Angalia hapo juu na do the needful please!
 
Nafikiri anahitaji wanaharakati hao, sasa Fidel na Teamo contact zao angepewa kama wazijua ili awasiliane nao,au vije GERARD????

Nimesha msoma moto wa mabadiliko unaanzia Ruhuji, Ramadhani, Ulembwe, Usalule, Makoga-Ikonda- Makete
 
Nipo mkuu ila Makete nina maza angu mdogo kanywa maji ya bendera ya kijani mpaka shuka anazo lalia rangi hiyo hiyo duh

...wewe kama vipi huyo usimwambie issue za CDM unaweza mzuga akutafutie contacts huko...then akurushie wewe utampa mshikaji hapa au?
 
Thanks mdau kwa juhudi mnazofanya kwa mkoa wetu mpya wa njombe. Ninachofahamu mie ni kuwa wilaya hizi zina uongozi kamili ambao kwa hakika contacts zao zipo cdm hq. Mkipata contacts mtaanzia hapo kuendeleza mapambano.
Nashukuru sana. Kwa mujibu wa katiba ya CDM M/kiti wa Wilaya ni mjumbe wa baraza la uongozi la mkoa. Kwa hiyo wakati wa uchaguzi wa ndani ya chama wa mwaka 2009 wilaya za Ludewa na Makete zilihesabiwa kuwa hazikuwa na uongozi rasmi. Ndivyo inavyojulikana hadi makao makuu. Hata hivyo tunatambua uwepo wa wakereketwa ambao walijitolea na wanaendelea kujitolea ikiwa ni pamoja na waliogombea Ubunge. Ushahidi wa hili ni kilichotokea Ludewa wakati wa uchaguzi mkuu.Hata hivyo mpango wetu ni kutengeneza uongozi rasmi utakaochaguliwa kikatiba toka ngazi ya chini mpaka mkoani ukihusisha wilaya zetu zote nne yaani wanging'ombe, Makete, Ludewa na NjNjombe. Tunaomba mawazo zaidi Mkuu
 
Hongereni.

Concern yangu hapa ni kama hatujaona mchango wa CDM makao makuu katika hizi jitihada. Naamini kama hizo contacts si ajabu ingekuwa rahisi kuzipata kwa ushirikiano na na uratibu kutoka makao makuu mpaka ngazi ya mkoa in this case nadhani mngehitaji kushirikiana na viongozi wa mkoa wa iringa kwani ndio mkoa wenu wa njombe ulipotokea.

Nawatakia kila la kheri
Mkuu makao makuu wanatoa support ingawa sisi tumeamua kuanza wenyewe ili mako makuu watakapokuja watukutuke tukiwa tunatembea sio tunatambaa. Kumbuka wametoa kadi zaidi ya 4000 na bendra zaidi ya 100 kitu ambacho ni kinatusaidia sana hasa kwa kuanzia. Kuhusu Mkoa wa Iringa mimi na M/kiti wangu wote kikatiba tulikuwa viongozi wa mkoa wa Iringa (Wajumbe wa baraza la uongozi wamkoa) tatizo ni kwamba Wilaya hizo mbili pamoja na Jimbo la Njombe magh yalikuwa ni maeneo ambayo yalikuwa inactive kwa miaka mingi. HATA HIVYO HABARI NJEMA NI KWAMBA JANA MARA YA KUPOST MADA HII TULIPATA CONTACTS ZA WATU WA MAKETE BADO LUDEWA HATUJAPATA KABISA
 
Nimesha msoma moto wa mabadiliko unaanzia Ruhuji, Ramadhani, Ulembwe, Usalule, Makoga-Ikonda- Makete
Aisee mkuu upo juu. Ulembwe na Makoga ni baadhi ya vijiji ambavyo watu wake wanasupport sana mabadiliko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom