Maelezo ya Wizara ya Elimu kuhusu mchakato wa kurekebisha matokeo ya Kidato cha 4


tunduruboy,

Wewe ndiyo useless person!Your broken English reveals and tell the true inside of you. Sijui kiwango chako cha elimu, na wewe ulipata daraja gani F4 yako,ninachotaka kukuambia ni kwamba ulichoongea ni pumba na hakina mantiki.
Tangazo la Wizara ya Elimu liko wazi kabisa kwamba wanatekeleza agizo la Serikali kukingana na maelekezo ya Tume ya PM kuwa LAZIMA MCHAKATO WA MATOKEO YA F4 MWAKA 2012 UFANANE NA MICHAKATO YA MIAKA YA NYUMA(GRADING PROCESS) AMBAO UMEKUWA UKITUMIKA TANGU MWAKA 1973. SINA HAKIKA KAMA ULIKUWA UMESHAZALIWA!

Sasa kama utaratibu wa Grading umekuwa ukitumika kwa miaka yote tangu 1973,utaratibu ambao hata mimi umeweza kunifikisha hapa nilipo na elimu yangu nzuri kabisa ambayo nina hakika hata tukiingia darasani leo ninatoka na flying colours. Iweje vijana,watoto na wadogo zetu leo wafelishwe kwa kutumia utaratibu mpya baada ya miaka 40?????!!!!

Umesema 'politics and education can never walk together'!!Seems you don't know what you're talking. SERA ZA ELIMU MAHALI POPOTE DUNIANI ZINAHUSISHA SIASA KWA MAANA WANAOTUNGA SERA NI HAOHAO WANASIASA(WABUNGE) WALIOCHAGULIWA NA WANANCHI WENYEWE. So, you can never separate politics and education. Never!

Acheni NECTA wafanye kazi yao kulingana na maelekezo ya Tume na Serikali halafu tuone sasa matokeo yatabakia vilevile au kutakuwa na mabadiliko. Kama mwanafunzi wa kidato cha 4 mwaka 2011 alipata D kwa kupata alama 30% kwa utaratibu wa (D:alama 21-40) kwa utaratibu ulokuwa unatumika tangu 1973 lakini mwanafunzi wa kidato cha 4 mwaka 2012 aliyepata 30% apate F(F:alama 0-34)???
 
Mkuu hoja yako ni ya msingi sana. Lakini kabla ya kujua hilo uliwahi kujiuliza ni kwanini matokeo ya CSEE 2012 kwa mara ya kwanza katika historia ya uanzishwaji wa Baraza la Mitihani na tokea Dr. J. Ndalichako aingie madarakani, hakutangaza yeye bali alitangaza Waziri wa Elimu Dr Kawambwa mwenyewe.

Wa-TZ tukiendelea kuchanganya siasa mpaka kwenye mambo nyeti ya kitaalamu kama Elimu tumekwisha.
 
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea

Shida kubwa inayoangamiza taifa letu ni kufanya kila kitu siasa, kila kitu serkali inachofanya ni kuhakikisha wananchi hawachukii, hata kama sio swala la siasa. Baraza la mitihani liko chini wizara ya elimu sasa kwakuwa sura kufeli kwa watoto sehemu ilichangiwa na serikali kwa kutoa elimu duni! alafu sasa mzigo wanawatwisha baraza la mitihani heti walibadirosha viwango!!

Haya mambo yanapatiana Tanzania tu! Kwani matokeo hayawezi kutangazwa mpaka yapitie wizarani, kwanza serikali illizika ndo waliyatangaza. Lakini yakuona wananchi wamechukia ndo waamua kuyachakachua ili wapiga kura wafurahi.

Mambo ya kuwa ni mapendekezo ya tume kuna walakini.
 

wakati wanaangaika kuchakata matokeo ya form four ya form six yapo njiani sijui nayo yataingia kwenye uchakataji huu ili kuwafurahisha wananchi kwa ufaulu wa juu wakati ni changa
 
Hivi kwa nini usitumie kiswahili?....kiingereza hiki ndicho ulichotumia kujibu mitihani 2012....? hata Le Mutuz hawez ongea hiv...kibovu sana...pu...mb....a.fu

Kiingereza ni lugha ya pili, tatu au hata ya nne kwa baadhi ya watu. Ni sawa na ww Mmakonde ukajifunza Kigogo, huwezi kukosa makosa ktk matumizi. Mwenziyo amejitahidi kukitumia we unamtukana badala ya kumkosoa pale ww unapoona amekosea..., hatuwezi kufika popote maana mvunja nchi ni mwananchi!
 
Mwaka huu tutayabadilisha sawa lakini tatizo halijatatuliwa je, tutayabadilisha kila mwaka kwa kua mumeshindwa kutatua matatizo ya walimu ambacho ndio chanzo cha watoto kufeli kila mwaka?
 
Its a Hypocrite country,, hata kama wakirekebisha,, ila wajue kuna maisha ya wanafunzi yameharibika,,wachache wamejiua,, na wengi there state of mind its disrupted,,

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

Kama nilivyoeleza kwenye makala yangu kwenye Raia Mwema, hakuna kigeni katika hili. Serikali inafanya propaganda katika jambo kubwa kama hili. Kila kitu kinajulikana na kilijulikana serikali, kwa sababu hakuna wanachoweza kufanya NECTA bila serikali kujua. Kumbuka NECTA ni moja ya vyombo vinavyoangaliwa sana na usalama wa taifa kwa sababu nzuri kabisa. Sasa watanzania tumezoea kudanganywa na kudanganyika. Kinachofanyika ni kujaribu kufukia takataka ndani ya carpet na kujidanganya kwamba takataka hizo hazipo!!
 
mbona Lukuvi mwenyewe hamtaji yeye digree zake za wapi? Mrema je mwenye digree ya kuangua maembe ha-ha-ha!
 
Kitila Mkumbo,

..naomba kama una nafasi utusaidie kujibu maswali ambayo NasDaz ame-raise ktk posting niliyo-quote hapo juu.
 
Last edited by a moderator:
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea

Mkuu naomba unisaidie kuelewa hapa kwa kiswahili, kuna utaalamu gani wa kupitia upya mtihani unaoweza kumfanya mtoto aliyefeli kwa vigezo vilivowekwa na afaulu kwa vigezo hivyo hivyo na mtihani huo huo aliofanya?. Lugha pia hata kama ni kiswahili inatusumbua baadhi yetu ambao vidato vimetupita, "kupitia upya" kama watalaamu walivyokutana wanataka tuelewe nini, ni mtaalamu gani mwenye uwezo huo wa kupitia, bila kuchakachua na yaendane na matakwa ya kitaalama? Bila kujali kama ni Lukuvi amesema kwa niaba ya serikali, au kama ni kwa niaba ya "watalaamu", kitendo hiki cha kuboresha matokeo ili kuridhisha wazazi wa watoto waamini kuwa watoto wao wanafanya vizuri.

Kwa watu wa kawaida wa mtaani kama mimi, tunaona kuwa ni kama mchezo wa kuhamisha goli ili mshambuiliaji mzembe afunge. Kuchakachua matokeo ya uchaguzi labda kunaweza.......lakini kuchakachua hata matokeo ya mtihani wa kitaaluma? kidogo hapo mkuu inaleta mashaka kuhusu utaalamu wa wataalamu.
 
Siasa kama kansa mkuu...imeshatuingia sana... Why Waziri ?...
 
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea

uko sawa ndugu serikali imefanya kitu kizuri sema kuna mijitu mingne wao kila kitu kibaya kwao
 

ahsante
 
Mkuu NasDaz hongera kwa uchambuzi mzuri, sema kuna mijitu humu ambayo kazi yao ni ubishi tu. Acha madogo wapate haki yao.
 
Last edited by a moderator:
Hoja ya msingi ni kuwa serikali ilijua lini haya mambo? Taarifa ya habari ITV jana makamanda wamesema kuwa wanao ushahidi kuwa mabadiliko hayo ni maelekezo ya Wizara. Kama hilo ni kweli, kwa nini Serikali ikubali kubadili? Kwa hiyo ni muhimu madogo wapate haki yao lakini waliosababisha sintofahamu hiyo nao wapate haki zaidi
 
Hili ndilo jambo la msingi sana ambalo watu wenye hekima wanapaswa kuliunga mkono kwa 100%. Period.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…