Maelezo ya Wizara ya Elimu kuhusu mchakato wa kurekebisha matokeo ya Kidato cha 4

oduko

Senior Member
Dec 16, 2012
169
56
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

UFAFANUZI KUHUSU KUPITIWA UPYA KWA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE MWAKA 2012


Mnamo tarehe 03 Mei, 2013 Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Wiliam Lukuvi (Mb) ilitoa Kauli ya
Serikali Bungeni Kuhusu Taarifa ya Awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Sababu za kushuka kwa ufaulu wa Mtihani wa Kidato cha
Nne Mwaka 2012.

Kauli ya Serikali ilielekeza kuwa matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne mwaka 2012 yafutwe na yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011 ili Wanafunzi hao wawe katika mazingira yanayofanana na ya wenzao wa miaka iliyopita kwa kuwa mfumo uliotumika mwaka 2012 katika kupanga matokeo na madaraja ni tofauti na ule uliotumika mwaka 2011 na miaka
iliyotangulia.

Kwa kuzingatia mapendekezo ya Tume na Maelekezo ya Baraza la Mawaziri, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwar mamlaka
aliyonayo chini ya Sheria ya Baraza la Mitihani Tanzania, kifungu cha 20, sura 107 ameliagiza Baraza la Mitihani la Taifa kupitia upya
Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012.

Aidha, imeagizwa kwamba matokeo hayo yaandaliwe kwa kutumia utaratibu uliotumika mwaka 2011. Serikali haikuagiza kufanyika upya kwa mitihani hiyo na wala haikuagiza kusahihishwa upya. Hivyo, Serikali inapenda kuwahakikishia wananchi kwamba
hapatakuwa na zoezi la kurudia usahihishaji wa mtihani huo kwa sababu hakuna dosari zilizobainishwa kwenye usahihishaji
wa mitihani hiyo.

Alama za watahiniwa ambazo zimehakikiwa zipo tayari, kitakachofanyika ni kwa Baraza la Mitihani kutumia alama hizo kuchakata matokeo upya kwa kutumia viwango vya ufaulu vilivyotumika mwaka 2011. Utaratibu ambao umekuwa ukitumika tangu mwaka 1973
wakati Baraza lilipoanzishwa, ni wa kuweka viwango vya ufaulu kila mwaka kwa kuzingatia ufaulu wa somo husika na ufaulu katika
mwaka uliotangulia.

Kutokana na maelezo hayo, ni dhahiri kuwa zoezi la kupitia upya matokeo ya Kidato cha Nne 2012 litachukua muda mfupi na matokeo yatatangazwa hivi karibuni.

Selestine Gesimba

KAIMU KATIBU MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO
YA UFUNDI
10/05/2013
 
useless people where are we taking this country we need people who are upright to lead this country we are tired of these crooks, Let the go to hell, Politics and education can never walk together, Let the experts do there work Lukuvi is a stdr 7 so he cant know the negative impact this will have of the future generation
 
useless people where are we taking this country we need people who are upright to lead this country we are tired of these crooks, Let the go to hell, Politics and education can never walk together, Let the experts do there work Lukuvi is a stdr 7 so he cant know the negative impact this will have of the future generation
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea
 
Hivi hii wizara ya elimu naibu waziri si ndiye kafoji vyeti, yeye anaona poa tu........, sijui ila inauma....sumu,zemarcopolo..hawa viongozi wenu wa CCM wanatumia makalio kufikiri..........manake majibu mepesi kwa maswali magumu.....tutafika kweli?
 
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea

You can not know the value of something unless you have being through that, Lukuvi and fellow ministers do not know the extent of damage they are creating to this country or Is it that you are doing that deliberately so that they can create the educated people who will not protect the integrity of this country, The previous results which have been suspended were approved by the same cabinet with president Kikwete chairing the meeting, Are you telling me that they did not see that problem, What am saying is improve the education sector not stardandising them get me correct you hypocrite
 
Watanzania tunahaki ya kujua kilicho sababisha Baraza la Mitihani kuachana na mfumo uliokuwa unatumika toka 1973... Sababu za kurejea mfumo huo zinajulikana kuwa ni kuongezeka kwa kasi watahiniwa waliofeli! Je nini kilisababisha Baraza kubadili mfumo?...
Tusifanye mchezo katika elimu hata kidogo, hapa ndipo ambapo Taifa linazalisha madaktari, mainjinia, marubani, manahodha, wapiganaji, wanasiasa, waalimu aitha vipanga ama vilaza!...Kama Taifa, maendeleo yetu yatategemea na uwezo wa Rasilimaliwatu tuliowaandaa...
Kwa upande wa pili wa shilingi; Tunaweza kuendelea kutawaliwa kiakili na kimwili kwa kukosa maarifa! Kwa kukosa maarifa tunajikuta RASILIMALI zetu hazitusaidii bali zinawanufaisha mabeberu plus makuwadi wachache... nina mashaka na huu mkakati unaoendelea kama kweli unaangalia maslahi mapana ya Taifa letu, na si mbinu za kutufanya duni na kuendelea kutawaliwa kwa miongo mingine mingi ijayo...
 
kuliko kushiriki kwenye hii dhambi ya kuchakachua matokeo itakayopelekea kuzalisha fake engeneers,fake doctors,fake teachers ni bora uache kazi.
 
You can not know the
value of something unless you have being through that, Lukuvi and fellow
ministers do not know the extent of damage they are creating to this
country or Is it that you are doing that deliberately so that they can
create the educated people who will not protect the integrity of this
country, The previous results which have been suspended were approved by
the same cabinet with president Kikwete chairing the meeting, Are you
telling me that they did not see that problem, What am saying is improve
the education sector not stardandising them get me correct you
hypocrite

Hivi kwa nini usitumie kiswahili?....kiingereza hiki ndicho ulichotumia kujibu mitihani 2012....? hata Le Mutuz hawez ongea hiv...kibovu sana...pu...mb....a.fu
 
@ilboru1995, thatha,

..kama mna muda someni article ya Kitila Mkumbo aliyochapishwa na gazeti la raia mwema.

..if u dont have time soma key point nilizo-highlight.

..kwa mtizamo wangu serikali inachakachua elimu, na huo ni mchezo wa hatari sana kwa future ya taifa letu.

Dr.Kitila Mkumbo said:
LINI SERIKALI ILIJUA KWAMBA MATOKEO YA 2012 YALIKOSEWA??

UENDDESHAJI wa sekta ya elimu nchini hauishi vituko. Kituko cha hivi karibuni kabisa ni uamuzi wa Serikali kufuta matokeo ya kidato cha nne na kuliamuru Baraza la Mitihani liyaendae upya.
Dr.Kitila Mkumbo said:
Niwakumbushe wasomaji kwamba hiki si kituko cha kwanza na cha mwisho katika uendeshaji wa sekta ya elimu nchini chini ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM). Miaka ya 1980 tuliwahi kutumia watu waliohitimu darasa la saba kuwa walimu, maarufu kama walimu wa UPE. Baadaye tukaamua kujenga shule za sekondari katika kila kata bila maandalizi yeyote ya maana. Matokeo yake kila kitu kikawa hakitoshi, isipokuwa majengo yaliyojengwa chapuchapu na bila usimamizi wa kihandisi.

Tulipoona walimu hawatatoshi kukidhi mahitaji ya shule zilizoongezeka sana, tukaibuka na walimu wa voda fasta, tukichukua vijana waliomaliza kidato cha sita na'kuwafundisha’ ualimu chapuchapu.
Sasa hili la kufuta matokeo linahitaji mjadala kama tulivyojadili mambo mengine huko nyuma. Tunajua mijadala haisaidii kwa Serikali hii lakini ni vizuri wengine tukasema ili isijeonekana wote tumeridhika na hatua hii ya Serikali au kwamba maamuzi ya Serikali yapo sawa. Ukweli ni kwamba uamuzi wa kufuta matokeo ya kidato cha 2012 haujakaa sawa kama nitakavyoonesha katika makala haya.

Katika kuhalalisha uamuzi wake wa kufuta matokeo ya kidato cha nne 2012, Serikali inasema kwamba Baraza la Mitihani la Tanzania lilitumia viwango vipya vya ufaulu bila kuwashirikisha na kuwaandaa walimu na wanafunzi, na kwamba kiwango kipya hakikutenda haki kwa walimu na wanafunzi waliofanya juhudi kubwa katika mazingira ya elimu ya sasa.

Swali la kwanza la kujiuliza ni je, tangu lini Baraza la Mitihani linawahusisha wanafunzi na walimu katika kupanga viwango vya ufaulu? Ukweli ni kwamba maamuzi ya Baraza la Mitihani siku zote hufanywa na vikao mbalimbali vya Baraza lenyewe, ambapo wadau mbalimbali ni wajumbe, ikiwamo Serikali yenyewe na kwa pande zote za Muungano! Shule, walimu na wanafunzi hupokea taarifa tu kuhusu maamuzi ya Baraza.

Swali la pili la kujiuliza ni je, Serikali ilijua lini kwamba matokeo haya yalipangwa kwa viwango vipya vya ufaulu? Kama nilivyosema hapo juu, Serikali ni mjumbe kamili wa Baraza la Mitihani Tanzania, ikiwakilishwa na Makamishna wa Elimu wa Tanzania Bara na Visiwani, pamoja na taasisi nyingine za elimu nchini. Kwa hiyo ni wazi kwamba Serikali ilijua na kuridhia matumizi mapya ya viwango vya ufaulu kabla ya kuanza kutumika, na wala hapakuwa na haja ya kuunda tume kujua jambo hili.

Kwa kawaida, kabla matokeo hayajatangazwa siku zote hufanyika uhakiki na kufanya marekebisho muhimu, ikiwamo kufanya uwiano (standardisation). Sasa swali la kujiuliza ni lini Serikali ilijua kwamba matokeo ya kidato cha 2012 yalikuwa mabaya kwa kiwango tulichokiona? Je, ni kweli kwamba Serikali ilikuwa haijaona matokeo haya hadi Waziri Dk. Shukuru Kawambwa anayatangaza?

Mantiki hapa inatuambia kwamba Serikali ilikuwa inayajua matokeo kabla ya kutangazwa na kuridhia kwamba yatangazwe. Kuamini vinginevyo ni kujidanganya. Kwa mantiki hii ni wazi kwamba Serikali ilishituka baada ya watu mbalimbali kupaza sauti kubwa wakiyazomea matokeo yale kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea.
Ndiyo kusema kwamba Serikali iliwajibika kuunda tume kwa sababu ya shinikizo la umma na ilikuwa haijajiandaa katika hili kwa kuamini kwamba tutalalamika na kisha litapita kama ilivyo ada ya sisi Watanzania.

Tukiangalia maudhui yenyewe ya sababu za Serikali za kufuta matokeo utakuta kwamba hapakuwa na sababu za kuunda tume. Kiwango kipya cha ufaulu kinacholalamikiwa na Serikali kupitia katika taarifa iliyowasilishwa na William Lukuvi ni jambo ambalo limekuwa likijadiliwa na wadau wa elimu kwa muda mrefu.
Tulikuwa tunalalamikiwa sana katika ukanda wa Bara la Afrika kwamba viwango vyetu vya ufaulu vipo chini sana, na hili limekuwa likisababisha vijana wetu wanaoenda kusoma nchi mbalimbali kupata taabu katika kukubalika moja kwa moja.

Kwa mfano, kiwango cha chini cha ufaulu katika mitihani ya kidato cha nne katika nchi nyingi za Kiafrika ni 40. Ndiyo kusema yeyote anayepata chini ya alama hii katika somo lolote inamaanisha amefeli somo husika. Nchi hizi ni pamoja na Ethiopia, Sudan, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika Kusini, Ghana, Nigeria, Gambia, Liberia, Sierra Leone na Uganda.

Kwa hiyo utaona kwamba ni sisi peke yetu katika ukanda huu wa Afrika ambao tulikuwa tunatumia kiwango cha ufaulu cha alama 21, ambacho kwa kweli ni kidogo mno na ni udanganyifu ukilinganisha na nchi nyingine za Kiafrika tunazofanana nazo.

Nieleze pia hapa kwamba hiki kiwango kipya kinacholalamikiwa kimeshajaribiwa kwa kuangalia matokeo ya 2010 na 2011 yangekuwaje kama Baraza lingetumia viwango hivi vipya. Katika mithani hii ilionekana tofauti ndogo sana katika ufaulu katika kutumia kiwango kipya na cha zamani.

Kwa mfano, tofauti katika mitihani ya mwaka 2010 ilikuwa 1.24 na asilimia 0.5 kwa mitihani ya 2011. Ndiyo kusema wazazi na wanafunzi waliofanya mitihani ya kidato cha nne 2012 wasichekelee sana kwa sababu uwezekano ni mdogo kwamba kutakuwa na tofauti kubwa kati ya matokeo yaliyofutwa na yale yatakayokokotolewa upya.

Serikali inaposema kwamba Baraza litumie viwango vya ufaulu vya mwaka 2011 ni kana kwamba matokeo ya mwaka huu yalikuwa bora. Nikumbushe kwamba matokeo ya mwaka 2011 yalikuwa mabaya vilevile na hayana tofauti kubwa na matokeo yaliyofutwa.

Hii ni kwa sababu asilimia 90 ya wanafunzi waliofanya mitihani ya kidato cha nne ya mwaka 2011 walipata madaraja ya IV na sifuri ukilinganisha na asilimia 93.6 waliopata madaraja haya katika matokeo yaliyofutwa ya mwaka 2012.

Niikuikumbushe Serikali kwamba Baraza la Mitihani lilibadilisha pia viwango vya ufaulu kwa Kidato cha Sita ambapo sasa kiwango cha chini cha ufaulu ni 40-44. Ni vizuri sasa serikali isisubiri matokeo yatoke ndipo ishtuke. Nashauri Serikali iwaamuru Baraza la Mitihani watumie kiwango cha zamani cha ufaulu ili kuepuka usumbufu kama ulivyojitokeza kwa matokeo ya kidato cha nne ya 2012.

Nimalizie kwa kuwaasa Watanzania wenzangu na Serikali yetu kwamba matatizo yetu ya elimu hayawezi kutatatuliwa kwa kutumia viwango vya chini vya ufaulu ambavyo haviendani na viwango katika nchi nyingine za Kiafrika na dunia kwa ujumla. Tuache kufanya mambo rahisi kwa kujifurahisha muda mfupi na kutengeneza maumivu kwa muda mrefu ujao. Sababu za wanafunzi kufeli zimeanishwa katika tafiti mbalimbali na Serikali inajua, lakini haijachukua hatua za maana kwa sababu tumezoea kufanya mambo kukidhi haja ya leo.

Kufuta matokeo na kuyapanga upya hakutatua matatizo ya msingi yanayoikabili elimu yetu. Suluhisho ni kuwa na mipango endelevu katika kuwekeza kwa walimu na miundo mbinu ya ufundishaji na kujifunza.



cc:mad:tunduruboy, Kichuguu, NasDaz, ZeMarcopolo, Zitto
 
Hivi kwa nini usitumie kiswahili?....kiingereza hiki ndicho ulichotumia kujibu mitihani 2012....? hata Le Mutuz hawez ongea hiv...kibovu sana...pu...mb....a.fu

It does not matter what language I use tanzania has two official languages if you dont know English go to hell with your Lukuvi
 
Ni wazi serikali imeona bora iwape marks za bure na ipunguze sifuri aalf watangaze kiwango cha ufaulu kimepanda na watu wazidi kujidanganya alaf walio pata zero ndio watakwenda kwenye vyuo vya ualimu maana wataongezewa marks watapata divion 4 na3
 
Acheni kupiga kalele za kasiasa hapa nyie,nani kawaambia kusoma ni deal hapa Bongo?

Viigizo vyangu katika maisha ni hawa wafuatao.

1.Mbowe huyo anapeta na hana elimu hiyo munayoipigia kalele hapa
2.Sugu huyo anapeta form four failure
3.Mnyika huyo anapepa na maeshindwa kumalizia degree yake ya jioni
4.Lema huyo anapeta jambazi ala arusha mstaafu
5.Maji marefu huyo anapeat mganga wa kienyeji
6.Selemani Bungala huyo anpeta darasa la saba

Orodha ni Ndefu jamani naomba tu munisaidie wan jamvi.

Kama unabisha wewe komaa kupiga shule na ujifanye wewe ni kichwa hao vilaza wa hapo juu watakuja kukupeleka mbio mpaka ukome,chezea Tanzania wewe.

Bora hayo matokeo yarudiwe tu uenda yatawasaidia hao vijana kupata hata uwezo wa kununua unga na dagaa kwa kufanya certificate za ualimu.

Ukitaka ufanikiwe Bongo basi kuwa mjanjamjanja wa mjini mambo yako yatakuwa super lakini ukijifanya kichwa sana na mishule yako maisha yatakupiga mpaka mwisho,wananifurahisha sana akina Joti na yule Professa wao,duh ule ndio ualisia wa Bongo.
 
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea

Ila hao hao wataalamu walikuwepo pamoja na waziri wao wakati matokeo yakitangazwa kama wangekuwa watu makini wangeshituka kulikoni matokeo 65% ni zero na waliofaulu ni wachache kivile kabla ya hata kuyaweka kwenye public maana haya mambo wanayofanya leo yalishafanyika miaka ya nyuma na matokeo yakitoka yameshatoka, nadhani tuchukue kama changamoto ili siku nyingine waumize vichwa kabla ya kutangaza vitu
 
Acheni kupiga kalele za kasiasa hapa nyie,nani kawaambia kusoma ni deal hapa Bongo?

Viigizo vyangu katika maisha ni hawa wafuatao.

1.Mbowe huyo anapeta na hana elimu hiyo munayoipigia kalele hapa
2.Sugu huyo anapeta form four failure
3.Mnyika huyo anapepa na maeshindwa kumalizia degree yake ya jioni
4.Lema huyo anapeta jambazi ala arusha mstaafu
5.Maji marefu huyo anapeat mganga wa kienyeji
6.Selemani Bungala huyo anpeta darasa la saba

Orodha ni Ndefu jamani naomba tu munisaidie wan jamvi.

Kama unabisha wewe komaa kupiga shule na ujifanye wewe ni kichwa hao vilaza wa hapo juu watakuja kukupeleka mbio mpaka ukome,chezea Tanzania wewe.

Bora hayo matokeo yarudiwe tu uenda yatawasaidia hao vijana kupata hata uwezo wa kununua unga na dagaa kwa kufanya certificate za ualimu.

Ukitaka ufanikiwe Bongo basi kuwa mjanjamjanja wa mjini mambo yako yatakuwa super lakini ukijifanya kichwa sana na mishule yako maisha yatakupiga mpaka mwisho,wananifurahisha sana akina Joti na yule Professa wao,duh ule ndio ualisia wa Bongo.

Point hiyo mkuu ila hao wote uliowataja pamoja na elimu zao hizo lakini wengi wao kuna vitu walikuwa wanavifanya ambavyo kwa namna moja ama nyingine vimewaunganisha na watu wengi na ndio maana ukatumia aka ya maji marefu na sugu ambao baada ya kujitambua waliamua kufanya shughuli ambazo mpaka leo wanatambulika kwa majina hayo. Nilichojifunza kwa hao uliowataja ni kwamba elimu ikigoma usikate tamaa wewe komaa na issue zako lakini bado issue ya kupiga shule bado ni muhimu mkuu maana shule ni kuongeza maarifa na si kwa ajiri ya kuajiriwa
 
mkuu LUKUVI katoa tamko kama serikali, suala la kupitia upya mtokeo ni limekuja baada ya wataalam kukaa ni kufikia muafaka huo, unaweza kujifanya na kiingereza chako, lakini kumbe hujui hata kinachoendelea

sina hakika kama serikali ya ccm ina wataalam labda kama ukisema wabaishaji ntakuelewa
 
Serikali kupitia Wizara ya Elimu kwa kauli hiyo inasema uthamani wa matokeo ushushwe ili ufaulu uwe na taswira nzuri na si uhalisia wa ubora wa kipimo cha mtihani.


Si kosa la serikali ni kosa la walioiweka serikali madarakani. Waziri Kawambwa ni mtoto wa nasaba ya Kikwete; tafuta ufaulu wao kwenye mitihani utajiridhisha walioiweka serikali hii madarakani wametuua bila kututazama.


TAFAKARI CHUKUA HATUA.
 
Back
Top Bottom