Maelezo ya mkutano wa Al-Adawi na Ridhwan Kikwete

TANleaks

Member
Dec 22, 2010
24
0
Utangulizi:
Jana nimeweka thread ya mkutano wa wabunge kadhaa wa Kamati ya Nishati na Madini kisha ikang'olewa kwa kile kilichoelezwa kutojitosheleza. Lakini kile nilichokiandika kikaandikwa na gazeti la Nipashe Feb 24, 2011 katika muundo mwingine: Angalizo langu kwa MoD: Uwe na moyo wa subira hata kwa yale usiyoyapenda:

HABARI MPYA
Jumapili ya Februari 20, 2011, saa kadhaa baada ya taikuni wa Dowans kukutana na wahariri na kisha kugoma kupigwa picha, taikuni huyo alikuwa na kikao na Rizwan Kikwete. Taarifa zilizotiririka kwa mtindo wa Diplomatic kebo zinaeleza bila shaka kuwa Rz1 alimfata taikuni huyo katika hoteli ya Kempinski majira ya saa tatu usiku na kisha kuongozana naye hadi katika nyumba anayoishi ile inayoaminika kujengwa na mafisadi wa EPA iliyopo Mikocheni jirani na Rose Garden. Kikao hicho kilifanyika hadi saa tano usiku ambapo vijana wetu ambao walikuwa wakivizia nyendo za Al-Adawi walimuona akitoka na RZ1 saa 5:15 na kurejea hotelini kwake.

Katika kikao hicho Rz1 alimhakikishia Al-Adawi kuwa Dowans italipwa na pia itapewa kazi zaidi, huku pia akimuomba ushirikiano katika biashara za sekta ya nishati katika siku zijazo.

Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Rz1 kujiingiza katika mkakati wa kuwekeza katika sekta hiyo ikiwa ni baada ya hatua yake ya kwanza kushindwa mwaka 2006 wakati alipoenda kusaka kampuni la kufua umeme toka Ujerumani lakini wataalam wa TANESCO wakalitilia mashaka kwa kuwa lilikuwa halina uwezo wa kuleta mashine zake na walizokuwa nazo zilikuwa za kizamani zaidi.
 
:decision::decision:Huuu ni upuuz !!! it seems that this is ongoing african culture ukienda Libya mtoto wa gadaf an say kwenye govt,same apply to Zanziba(aman karume jr),Now riziwan anaongea na huyu fisad au yeye ndo msemaji wa tanesco sku hz? hiz ni tabia za kifalme inabd zikomeshwe
How can the son of president ruin our country lyk this??? Ole wao wanotumia vyeo vya wazaz wao kujinufaisha wenyewe 2tawafyeka wote na kuwaangamiza siku unakuja
This country is fo tanzanians and not for Kikwete's CLAN!!! dammit.:decision::decision::decision:
 
Let's assume hayo aliyoandika Tanleaks ni kweli, ingawa yana walakin, kwani ni dhambi au sheria hazimruhusu Rz1 kukutana na Adawi na wakazungumza ya ama biashara ya ama kusoshalaiz?

Hivi huyu Adawi na hii Kampuni ya Dowans imekosa nini? Kuna mtu anaweza kusema kosa lao ni nini?

Au hizo ni chuki na roho mbaya tu? Rizwan akikutana na tajiri yeyote duniani, hakuna kosa analolifanya. Yeye ana life yake, ana biashara zake na Mungu kamjaalia ana jina na nasaba nzuri tu, ya kuwa mtoto wa Rais.

Hivi. Nyinyi hamna watoto zenu wanaojidai kwa kuwa na baba au mama kama nyinyi? Kama ni wahandisi, madaktari, waandishi, vinyozi, madereva, hamuoni sifa watoto zenu wakisema "mimi babangu kinyozi". Sasa kwa nini Rz1 asitumie hayo na kusema "mimi babangu Rais wa JMT"? Kuna kosa hapo?

Wacheni roho za korosho.
 
:decision::decision:Huuu ni upuuz !!! it seems that this is ongoing african culture ukienda Libya mtoto wa gadaf an say kwenye govt,same apply to Zanziba(aman karume jr),Now riziwan anaongea na huyu fisad au yeye ndo msemaji wa tanesco sku hz? hiz ni tabia za kifalme inabd zikomeshwe
How can the son of president ruin our country lyk this??? Ole wao wanotumia vyeo vya wazaz wao kujinufaisha wenyewe 2tawafyeka wote na kuwaangamiza siku unakuja
This country is fo tanzanians and not for Kikwete's CLAN!!! dammit.:decision::decision::decision:

Hivi wewe una ufikiri wa uhalisia? Hiyo ndio dream ya kila mtoto duniani, kuwa na kazi ya baba'ke. Hata Merekani tunawaona kina Bush kina Kennedy Kina clinton, India kina Ghandi. Na hizo ni demokrasi za kusifika kama ilivyo Tanzania. Jee, kuna ubaya gani mtoto wa kinyozi akiwa kinyozi?
 
RIz 1 TZ next presidaaaaaaa?!

Anatafuta hela za kutosha may be ili aununue....! just dreaming:A S 13:
 
Mdau online nitakuja kukupa hiyo ya Lake OIL bdaye! TANleaks ina watu wanaokusanya data maeneo mengi. Kuhusu uhakika wa taarifa hizi wala sina shaka nawaachia nyie mjiulize maswali maana taarifa yangu naamini inajitosheleza na ni ya uhakika
 
Mdau online nitakuja kukupa hiyo ya Lake OIL bdaye! TANleaks ina watu wanaokusanya data maeneo mengi. Kuhusu uhakika wa taarifa hizi wala sina shaka nawaachia nyie mjiulize maswali maana taarifa yangu naamini inajitosheleza na ni ya uhakika

Jee kwa hiyo taarifa yako ya uhakika, kuna dhambi hapo? Ya Rz1 kukutana na Adawi? Au unaeleza nini?
 
Duh! umesema vizuri ila umechoka kidogo kuendelea kufikiria. Wanajamvi wanachopinga hapa ni masuala ya nchi yenye kuhitaji maamuzi ya kimamlaka kufanywa na familia badala ya mamlaka husika. Ebu tupe mfano mmoja wa mtoto wa Rais wa Marekani aliyefanya kazi za Urais ? Umeanza na fikra nzuri sana ebu ziendeleze basi!!!
Hivi wewe una ufikiri wa uhalisia? Hiyo ndio dream ya kila mtoto duniani, kuwa na kazi ya baba'ke. Hata Merekani tunawaona kina Bush kina Kennedy Kina clinton, India kina Ghandi. Na hizo ni demokrasi za kusifika kama ilivyo Tanzania. Jee, kuna ubaya gani mtoto wa kinyozi akiwa kinyozi?
 
Sasa mlitaka mtoto wa NYOKA awe MJUSI? Wa mbili havai moja.

Kwa hiyo mtoto wa fisadi awe fisadi, mtoto wa mkulima awe mkulima tu. Kama ni hivyo JK mwenyewe asingekukuwa rais kwa kuwa baba yake hakuwa rais! Hata baba yako wewe asingesoma kwa kuwa baba yake (babu yako) hakuwa amesoma!
Hayo ni mawazo yanayofunga watu kufikiri na kubadilika kwa kisingizio kuwa baba yangu alikuwa hivi nami niwe hivyohivyo. Kulinganisha nyoka kuwa mjusi ili kujustify fisadi kuwa fisadi ni kushindwa kufikiri zaidi ya pua yako. Nyoka na mjusi wako tofauti kwani genetic makeup yao iko tofauti; lakini ufisadi, wizi, uongozi, ushoga nk ni tabia ambayo mtu anaweza kuiacha au kuiendekeza; siyo ya kurithika (heriditary)
 
Back
Top Bottom