Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Mkuu nimepitia maelezo yake ila still naona too general, hakuna facts za kutosha yeye akiwa kama mwenyekiti wa hiyo kamati ina maana hana clue zozote, mbona amekimbia hoja, yawezekana ni mtazamo wangu ila sioni kipya alichosema zaidi ya siasa tu
Umetoa maelezo magumu mno hawezi kukuelwa huyu. Usibishane nayemohamedi shosi acha ushabiki wa kinafiki.Ni wazi kuwa hakuna mbunge wa upinzani aliye makini anayetamani au kutafuta uenyekiti wa kamati ya POAC.Uenyekiti wa kamati haupewi na Spika bali wajumbe wa kamati ndiyo wanapiga kura.Kumbukeni ZZK kupata uenyekiti huo ni baada ya JK na Pinda kushauriana na kuamua kumwacha kuendelea kwa sababu yeye kama kiongozi wa CDM hakuwa na madhara kwa CCM.Leo hii endapo ZZK atatolewa kwenye nafasi ni CCM hawako tayari kumpatia nafsi hiyo mbunge wa CDM kwa haina yye ile ni bora apewe NCCR au CUF ,mbona CCM walimpa CHEYO nafsi ya uenyekiti PAC wakati UDP ina mbunge mmoja kwenye Bunge.
mimi sijasema Zito hafai .. wala sijui wala siamini kama kuna mkakati wa kumshambulia zito hafai hapa jf ...nasikia kutoka kwako leo mkuu
Mbunge wa Singida mashariki Tundu Lisu amefanya conference mjini Dodoma leo mchana amewataja wabunge wafuatao kuwa ndio vinara wa rushwa kamati ya nishati na madini.
I.Munde Tambwe
2.Sara msafiri
3.Mwijage
4.Nasir mbunge wa korogwe
Cha kushangaza lisu ameshindwa kumtaja zito kabwe kwa sababu zisizofahamika,nimeamini jamaa sio objective,ikumbukwe katibu mkuu Maswi amtaje Zitto ,Lisu anaficha ukweli for which reason mwizi ni mwizi tu
Tundu Lisu angefanya la maana kama angemtaja na zito kuliko kuwataja wabunge wa CCM tu.
Dah kumbe na wewe mkali wa Siasa eeeeh? Hongera sana nimezoea kukuona kuleeeee kwa kina nanihiiii Smile.ni kweli maana anapelekea watu kufikiria mbali zaidi...kumbe upinzani nako kuna makundi bwana...
Narudia kusoma maelezo ya Zitto kuna kitu kinachanganya: Maelezo yake ya awali alisema tuhuma hizi ni vita ya URAIS na POSHO, leo naona sababu ni nyingine kabisaaa!
Smile mtu mwenye akili timamu ni kweli kabisa kuwa wapo wabunge wa upinzani wanakitolea macho kiti cha mwenyekiti wa POAC.
Nimeandika moja ya reply leo kuwa Zitto hana back up ndani ya chama dhidi ya tuhuma zinazomkabili youpo peke yake na sio kwenye hili tu Zitto ni kama mtoto wa kambo ndani ya CDM ona watu wanavyomnanga humu jf siamini na wewe ni mmoja wa watu walioweza kutekwa na mkakati wa kumshambulia Zitto ili aonekane hafai!
Siku zote kwenye ukweli uongo utajitenga, Zitto tunamwamini na Mungu anajua yaliyo mioyoni mwetu Mungu atamwepusha na kila jicho la ubaya kama tuhuma alizo nazo ni za uwongo zenye chuki na uzandiki Amina.
Jambo moja tu ambalo ningependa kufahamu kutokana na hii press release hii na ambalo sijapata kulifahamu ni hili;
Ni Taratibu zipi zilizokiukwa na bodi ya wakurugenzi ya Tanesco katika kumsimamisha kazi Mhando ili apishe uchunguzi??
MAELEZO BINAFSI YA MHE. ZITTO ZUBERI KABWE DHIDI YA TUHUMA ZA RUSHWA HUSUSAN KUELEKEA KATIKA KUPITISHA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
- Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
- Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.
- Ni lazima tufike mahali kama viongozi kwamba utaratibu unapokiukwa na yeyote yule,au uongo unapotolewa hadharani tuseme bila kuogopa. Hili ndio jukumu letu kama wabunge na viongozi. Kusimamia ufuatiliaji wa utaratibu ni jukumu letu kama Kamati ya POAC na ndio sababu ya msingi ya kuanzishwa kwa mamlaka kama CAG na PPRA. Haiwezekani, tuwe na set ya kanuni kwa kundi fulani na nyingine kwa makundi mengine, au kuhukumu ufuataji wa taratibu kwa kuangalia sura ya mtu usoni
Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, 'Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga".
Ahsanteni sana.
I think Zitto hana haja ya kusema yote haya! Apige kimya tu! Always ukweli huwa unajitenga at the end of the day!
Nashindwa kuelewa ni kwanini ameshindwa kabisa, kabisa kuwa 'calm'.
hapo red sijaelewa zzk....mmmh
- Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
- Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa
Kuna vitu vingine hata hakutakiwa kuongea bwana ..zaidi anazidi kuharibu cheki hiki kipengele
Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.....
4. Baada ya tukio hilo, nikiwa hapa Dodoma, mwandishi wa habari wa gazeti moja alinifuata akiniambia kuwa wamekutana na Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake, Nd. Eliachim Maswi hapa hapa Bungeni na wamewaambia kuwa mimi nimepewa rushwa. Hakutaja nimepewa rushwa na nani, kiasi gani na wala kwa lengo gani!
5. Nimejaribu kumtafuta kwa simu Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake ili wanipe ufafanuzi juu ya mimi na Kamati ya POAC kuhusishwa na tuhuma hizi bila mafanikio, hali ambayo inaniondolea mashaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. Najaribu sana kujizuia kutokuwa na mashaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti
wenyewe amesema
Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga.
Zitto ana upweke wa kitambo! ana upweke usiopingika na usio na ubishi. Viongozi wa chama waliowanachama wa jf wamekaa kimya pale Zitto anaposhambuliwa na kuwa treated kama mtoto wa kambo!
wakati umefika kila lilifichika linatoka hadharani..ikumbukwe kwamba ni zitto huyuhuyu aliye ungamkono hoja ya kupandishwa kwa bei ya mafuta ya taakwa kisingizio cha kukomesha uchakachuaji, kama hiyo haitoshi ni zitto huyohuyo ndiye aliye piga kelele serekali inunue mitambo iliyo tumika ya ilyokuwa kampuni pacha ya richmond yaani dowans huku akijua fika ni kinyume cha sheria ya manunuzi ya umma..nadhani mmesahau kuwa zitto alishauriwa na watu wengi ikiwemao chama chake asiingie kwenye iliyokuwatume ya uchunguzi wa sakata la dowans kwa walio kwepo pale kona ya mlimani walisikia majibu aliyotoa..alisema hivi 'nimesikia mliyoyasema ila maamuzi juu ya hili suala ni yangu' huku akitahadharishwa kwamba waliokua kwenye kamati wengi ndio wahusika wa tuhuma zenyewe kesho yake tukasika zitto kakubali kuingia kwenye kamati na akahusika kuisafisha dowans,sasa mimi kwa maoni yangu zitto tunae muona leo ndiye zitto halisio mwenye tamaa na mwenye kuweka maslahi yake mbele..haya ni maoni yangu tu.ila zitto kwa sasa ni mtuhumiwa mpaka sheria itakapomtia hatiani nadio tunaweza kausema kuwa ni mwizi au fisadi,au mla rushwa ila mimi simuamini tena.