Huyu ni Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari aliyeshikilia kiti hicho tangu katikati ya mwaka 2016.
Tangu ashike nafasi hiyo amefanya mabadiliko mengi sana katika taasisi hiyo mengi yakiwemo yenye maslahi kwa taifa lakini pia amefanya mengi zaidi kwa maslahi yake binafsi ikiwa ni pamoja na kuligeuza shirika hilo kuwa kama kampuni yake binafsi.
Amefanikiwa kuwa dikteta wa shirika kwani amewafanya wasaidizi wake (wakurugenzi wa Idara na mameneja wa vitengo) kuwa kama picha tu maamuzi yote anafanya yeye bila kushauriana nao na kisha huwageuka pale mambo yanapoharibika. Mfano mzuri ni hili suala la bi. Nuru Mhando na meneja matumizi lililoibuliwa na Mh. Waziri Mkuu siku za hivi karibuni (amewatoa kafara tu , mhusika mkuu ni yeye)
Kwa mtazamo wa nje Serikali kuu inamuona kama ni mtu sahihi kushika nafasi ile kwamba amefanikiwa kuinyosha bandari lakini ukweli ni kwamba huyu jamaa ameiharibu bandari kwa kiasi kikubwa na athari zake zimeanza kuonekana dhahiri kama ifuatavyo:-
a) Ameondoa morali ya wafanyakazi kwa kufuta malipo yao ya masaa ya ziada ilihali anawafanyisha kazi mpaka usiku wa manane.
b) Amefitinisha kwa kiasi kikubwa mahusiano kati ya wafanyakazi wa ngazi za chini na viongozi wao kwa kuwa anawasiliana nao na kuwapa maagizo bila hata kuwajulisha mabosi zao.
c) Anashirikiana na kampuni za wachina kutafuna hela za Serikali katika miradi ya ujenzi kwa kuwapa kazi bila ushindani yaani Single Source procurement bila ya kuwepo sababu za msingi.
d) Pamoja na uwezo mzuri alionao wa kufanya kazi bila kuchoka mapema amekumbatia kazi zote za shirika yaani anataka kujua mpaka idadi ya vijiko vya sukari vinavyotumiwa na wafanyakazi wanapokunywa chai ofisini na hivyo kusababisha ucheleweshwaji wa maamuzi mbalimbali ya kikazi yaani amekumbatia kila kitu.
e) Katika kipindi alichokaa madarakani ameajiri na kufukuza kazi wahandisi na wakurugenzi wengi kwa kuwa tu walithubutu kumchallenge katika wizi wake anaoufanya hii ni pamoja na kuifukuza idara nzima ya ukaguzi wa ndani ambayo ilithubutu kuainisha ubadhilifu wake.
Haya ni baadhi tu ya madudu yake lakini ni jambo la kushangaza kwamba anaendelea kushika nafasi hiyo ya kuiongoza taasisi hiyo muhimu kwa uchumi wa taifa.
Natumia fursa hii kuziomba mamlaka za juu zifanye uchunguzi wa kina juu ya utendaji kazi wa huyu mtu na kuchukua hatua stahiki kwa maslahi mapana ya taifa