Madiwani Kigamboni wamshukia Ndugulile

Madiwani Kigamboni wamshukia Ndugulile

Jangakuu

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2012
Posts
513
Reaction score
221
MADIWANI wa mji wa Kigamboni wamemtaka mbunge wa jimbo hilo, Faustine Ndugulile, kuomba radhi kutokana na kauli yake kuwa hawajui kitu kinachoendelea katika uanzishaji wa mji mpya wa Kigamboni (KDA).

Faustine aliwatuhumu madiwani hao kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Mji Mwema Februari 23 mwaka huu kuwa ni mbumbumbu juu ya suala hilo na kwamba walisafiri kwenda mkoani Dodoma kufanya kikao cha kujadili uundwaji wa KDA bila mbunge huyo kufahamu.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya habari (MAELEZO) jijini Dar es salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Madiwani wa Kigamboni, Selemain Methew, alisema kuwa mbunge wao amekiuka taratibu za uongozi kutokana na kuwachonganisha na wananchi katika mradi huo.

Alisema mbunge amekuwa kigeugeu kwa kuwazunguka madiwani katika mipango mbalimbali ambayo mwisho wa siku anajitoa na kwenda kuzungumza na wananchi.

Methew alibainisha kuwa safari ya madiwani wa Kigamboni kwenda Dodoma, mbunge wao ndiye aliyependekeza, lakini sasa anarudi nyuma na kusema hatambui uwepo wa kikao hicho.

Kwa upande wake, mlezi wa kamati, Diwani wa Tungi, Kanali mstaafu, Abel Luambano, alisema Ndugulile anakiuka taratibu za utawala bora na maazimio ya kikao walichofanya Dodoma na kwamba mgongano uliopo ni kiongozi kutokujua mipaka ya madaraka yake.

Jitihada za Tanzania Daima kumtafuta Ndugulile kupitia simu yake ya kiganjani kuzungumzia madai hayo hazikufanikiwa.


Source: Tanzania Daima | na Chalila Kibuda
 
Huku Mbagala tuna Matatizo kibao lakini huyu mbunge Ndungulile nilimuona Mara ya mwisho wakati wa kampeni 2010. Sasa hivi hata bungeni hasemi lolote kutwa anashinda chako ni chako akitafuna vipande vya kuku na bia
 
Huku Mbagala tuna Matatizo kibao lakini huyu mbunge Ndungulile nilimuona Mara ya mwisho wakati wa kampeni 2010. Sasa hivi hata bungeni hasemi lolote kutwa anashinda chako ni chako akitafuna vipande vya kuku na bia

unataka umuone akiwa Mbagala au afanye kazi awasaidie mbagala??

vipi mkuu huendi hata mjini wala chooni ukisubiri kumuona??

what a stupid comment

kumuona pekee haisaidii we need actions
 
Madiwani wengi wa Kigamboni hawajui wanataka nini...... wengine wana magari ya wizi, wengine wanahongwa vigori, wengine walipanda gari kwenda dodoma hotel nk

Daktari is too advanced kwao, sijui kwanini alijiigiza kwenye hao wapuuzi, his vision doesnt match madiwani na chama alichopo
 
unataka umuone akiwa Mbagala au afanye kazi awasaidie mbagala??

vipi mkuu huendi hata mjini wala chooni ukisubiri kumuona??

what a stupid comment

kumuona pekee haisaidii we need actions
Wenzake wakina Mnyika wanafanya Mikutano kukusanya Kero za wananchi ndio maana yangu kumuona. Sasa nije mjini kufanya nini? Kumuona Ndungulile? Wakati wakati wa kura nilipigia mjini? Hebu peleka ujinga huko! Kwahiyo anawakilisha watu wa mjini wakati sisi wapiga kura wake tuna Kero ambazo anatakiwa aziwakilishe serikalini au atakuja tena 2015?
 
Madiwani wengi wa Kigamboni hawajui wanataka nini...... wengine wana magari ya wizi, wengine wanahongwa vigori, wengine walipanda gari kwenda dodoma hotel nk

Daktari is too advanced kwao, sijui kwanini alijiigiza kwenye hao wapuuzi, his vision doesnt match madiwani na chama alichopo
Mkuu naona umejikita kumtetea huyu gamba!! Sisi Huku mbagala tunataabika mbunge hafanyi Mikutano na sisi wananchi wake kukusanya Kero zetu natamani ningehamia ubungo au kawe ambako kuna wabunge active lakini uwezo sina!!! Lakini 2015 sio mbali
 
Huku Mbagala tuna Matatizo kibao lakini huyu mbunge Ndungulile nilimuona Mara ya mwisho wakati wa kampeni 2010. Sasa hivi hata bungeni hasemi lolote kutwa anashinda chako ni chako akitafuna vipande vya kuku na bia
ndio mjifunze sasa watu wa Kigamboni,kuchagua mtu anaestahili kwa maendeleo ya Kigamboni yenu.Watu wapuuz.i puuz.i kama hawa kina Ndugulile next time wasipewe nafasi kabisa.
 
Mimi binafsi ni mhanga wa zoezi la Kigamboni. Kwa mkazi na mmiliki wa nyumba hapa Kigamboni anajua kabisa kwamba Zoezi hili ni mradi wa wakubwa na madiwani.

Huyu diwani wa Tungi ndugu Lwambano ni miongoni mwa watu wanaoshirikiana na waziri kutudhulumu haki yetu. Kama mtu angefanya just a simple research by asking a Kigamboni home owner angejua ukweli kwamba mbunge wetu anatetea maslahi yetu. Hawa madiwani ni wachumia tumbo.

Lakini kwakuwa humu jamvini kila mtu ana haki ya kusema hata kama hajui lolote kuhusu mradi wa Kigamboni, basi ninaheshimu mawazo yote japo siyapokei.
 
ndio mjifunze sasa watu wa Kigamboni kuchagua mtu sasa kwa maendeleo ya Kigamboni yenu.Watu wapuuz.i puuz.i kama hawa kina Ndugulile next time wasipewe nafasi kabisa.
Mkuu Nakubaliana na wewe kabisa sitarudia tena 2015
 
Ndugulile anaweza kuwa sahihi.hawa madiwani wanapelekeshwa tu! kwanini mh Mbunge amekuwa akilalamika kutohusishwa ktk mpango huu wa KDA?
 
Wenzake wakina Mnyika wanafanya Mikutano kukusanya Kero za wananchi ndio maana yangu kumuona. Sasa nije mjini kufanya nini? Kumuona Ndungulile? Wakati wakati wa kura nilipigia mjini? Hebu peleka ujinga huko! Kwahiyo anawakilisha watu wa mjini wakati sisi wapiga kura wake tuna Kero ambazo anatakiwa aziwakilishe serikalini au atakuja tena 2015?

ujinga nilishapeleka Mbagala... wewe wako bado unao?
 
Mkuu naona umejikita kumtetea huyu gamba!! Sisi Huku mbagala tunataabika mbunge hafanyi Mikutano na sisi wananchi wake kukusanya Kero zetu natamani ningehamia ubungo au kawe ambako kuna wabunge active lakini uwezo sina!!! Lakini 2015 sio mbali

hahahaaa, mie na Gamba mbalimbali

ila hoja yako ni dhaifu, hata kawambwa anakutana sana na wananchi wake kula kahawa

all we want ni kazi


utanielewa siku moja

Ila madiwani wa kigamboni ni utumbo mtupu, afadhali hata ya mbunge
 
sijui wananchu wa kigamboni walichagua mtu wakiwa wamelala...... Hao madiwani ni bureeeeeeeeeee.... Na mbunge ndo chaliiiii acha wapelekeshwa na kina tibaijuka......

Wamekutana wote wachumia matumbo...
 
Mkuu naona umejikita kumtetea huyu gamba!! Sisi Huku mbagala tunataabika mbunge hafanyi Mikutano na sisi wananchi wake kukusanya Kero zetu natamani ningehamia ubungo au kawe ambako kuna wabunge active lakini uwezo sina!!! Lakini 2015 sio mbali

Hiyo ya Kawe hapo unampa 'promo' tu Halima Mdee...mimi ni pro-Chadema supporter lakini sijawahi kuona mBunge dhahifu kushughulikia kero za wananchi wa jimboni kwake kama Halima Mdee. Nakubali ni mBunge mahiri kwa kushughulikia mambo ya kiTaifa, lakini Mdee hujachaguliwa na Taifa, umechaguliwa nasi wanaKawe...na hutujali, tuna kero kibao, tunatengeneza vikamati vya kujitolea na task-forces kufuatilia kero zetu pasi wewe kushiriki hata kidogo!
 
Hawa madiwani wameingizwa mjini na mama tibaijuka.
Safi dr.ndungulile, endelea kuwachapa madiwani njaa kali wamewauza wakazi wa kigamboni kwa vipande thelathini vya pesa.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
ndugulile anajitahidi sana kutetea wakazi wa kigamboni lakini nina wasiwasi naye tokea tibaijuka aliposema keshapewa chake(fidia),madiwani hawa ni mapoyoyo kabisa especially huyu mathew selemani(mchezaji wa zamani wa yanga?)ndio ovyo kabisa.,anawadanganya sana wakazi wa kigamboni wakati mlango wa nyuma anaenda ardhi kupokea milungula
 
Hiyo ya Kawe hapo unampa 'promo' tu Halima Mdee...mimi ni pro-Chadema supporter lakini sijawahi kuona mBunge dhahifu kushughulikia kero za wananchi wa jimboni kwake kama Halima Mdee. Nakubali ni mBunge mahiri kwa kushughulikia mambo ya kiTaifa, lakini Mdee hujachaguliwa na Taifa, umechaguliwa nasi wanaKawe...na hutujali, tuna kero kibao, tunatengeneza vikamati vya kujitolea na task-forces kufuatilia kero zetu pasi wewe kushiriki hata kidogo!

Halima Mdee is the biggest disappointment kwa Vijana wanaopenda mageuzi

hakuna kitu pale na anajua hawezi kurudi
 
Sina imani na hawa madiwani maana wakipewa mlungula tuu wanakuwa bendera fuata upepo!
Yaani full magumashi
Kuna siku walimtuhumu mama Tibaijuka kuwa anaongea kwa vyombo vya habari mambo ya kuanza iyo authority bila wao kujua leo hii wanajifanya wanajua iyo KDA
 
sijui wananchu wa kigamboni walichagua mtu wakiwa wamelala...... Hao mas
diwani ni bureeeeeeeeeee.... Na mbunge ndo chaliiiii acha wapelekeshe na kina tibaijuka......

Wamekutana wote wachumia matumbo...

Madiwan na Mbunge ni km pipa na mfuniko
 
Mnaweza kukesha kumlaumua mbunge au madiwani lakini ukweli unabaki palepale kuwa iwapo sheria ya nchi ya ardhi inaipa nguvu kubwa wizara kuliko local governments wawakilishi hawa hawataweza kumsimamisha mama Tibaijuka kuendekea na mikakati ya wizara ya jiji jipya la Kigamboni.
 
Back
Top Bottom