Dada Leti
JF-Expert Member
- Oct 3, 2019
- 285
- 396
Nimeona wapinzani wetu wanamshangilia Rais Samia kuwaalika waingie Serikalini.
Bila shaka, Mama atawateua wale wapinzani wenye majina makubwa kwa malengo fulani ya kisiasa, pamoja na kuunda umoja wa kitaifa kama anavyodai.
Wasiwasi wangu ni kuwa, hawa wapinzani sijui kama wanajielewa.
Sijui kama wanaelewa madhara ya mfupa wanaotupiwa wautafune.
Wale wawindaji wanafahamu jinsi ya kumpoteza fisi anayekukimbiza. Unamtupia fupa ahangaike nalo wakati wewe unatokomea.
Wapinzani watakapojiloga kupokea hizo nafasi, kwanza watakuwa wameua vyama vyao kwa sababu hawawezi kufanya tena siasa za kipinzani wakiwa serikalini.
Pili, Mama Samia atakuwa amefanikiwa vizuri kutumia kanuni ya "divide and rule".
Wapinzani na wafuasi wao wataparaganyika huku na kule na hawatakua wanaelewa waunge mkono juhudi za serikali ya mseto ama waendeleza siasa zao za kipinzani.
Mama atakuwa amefanikiwa kuiua demokrasia kwa njia tulivu na ya kisayansi, tofauti na mtangulizi wake aliyewashugulikia wapinzani waziwazi.
Bila shaka, Mama atawateua wale wapinzani wenye majina makubwa kwa malengo fulani ya kisiasa, pamoja na kuunda umoja wa kitaifa kama anavyodai.
Wasiwasi wangu ni kuwa, hawa wapinzani sijui kama wanajielewa.
Sijui kama wanaelewa madhara ya mfupa wanaotupiwa wautafune.
Wale wawindaji wanafahamu jinsi ya kumpoteza fisi anayekukimbiza. Unamtupia fupa ahangaike nalo wakati wewe unatokomea.
Wapinzani watakapojiloga kupokea hizo nafasi, kwanza watakuwa wameua vyama vyao kwa sababu hawawezi kufanya tena siasa za kipinzani wakiwa serikalini.
Pili, Mama Samia atakuwa amefanikiwa vizuri kutumia kanuni ya "divide and rule".
Wapinzani na wafuasi wao wataparaganyika huku na kule na hawatakua wanaelewa waunge mkono juhudi za serikali ya mseto ama waendeleza siasa zao za kipinzani.
Mama atakuwa amefanikiwa kuiua demokrasia kwa njia tulivu na ya kisayansi, tofauti na mtangulizi wake aliyewashugulikia wapinzani waziwazi.