EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
MTOTO wa Baba wa Taifa, Madaraka Nyerere amesema taifa linayumba kutokana na viongozi wengi kutumia nafasi zao kujilimbikiza mali kutokana na kukiuka miiko ya uongozi iliyoasisi na Mwalimu Julius Nyerere. Hali hiyo imesababisha uchumi kuhodhiwa na watu wachache huku umaskini ukiongezeka kwa Watanzania.
Kauli ya Madaraka inakuja wakati Watanzania wakiungana kukumbuka kifo cha Mwalimu Nyerere aliyefariki miaka 13 iliyopita mjini London Uingereza. Katika andiko lake alilotuma kwa Mwananchi Jumapili, Madaraka alisema kuachwa kwa sera ya Ujamaa na Kujitegemea na uchumi kuwa mikononi mwa wachache kumeifanya Tanzania ishindwe kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo.
Zamani kulikuwa na miiko ya viongozi ambayo iliwataka wasijihusishe na biashara, lakini sasa ni tofauti. Nawaomba Watanzania katika mchakato wa Katiba Mpya wachangie mawazo ambayo yataleta faida kwa umma kama Mwalimu Nyerere alivyopigania wakati wa uongozi wake, anasema.
Madaraka alisema anasikitishwa na baadhi ya viongozi wanaotamba hadharani kwa utajiri walionao huku wakibeza familia ya mwasisi wa Taifa, Mwalimu Nyerere kutokana na umaskini wao.
Madaraka: Taifa limeshindwa kumuenzi Nyerere
Kauli ya Madaraka inakuja wakati Watanzania wakiungana kukumbuka kifo cha Mwalimu Nyerere aliyefariki miaka 13 iliyopita mjini London Uingereza. Katika andiko lake alilotuma kwa Mwananchi Jumapili, Madaraka alisema kuachwa kwa sera ya Ujamaa na Kujitegemea na uchumi kuwa mikononi mwa wachache kumeifanya Tanzania ishindwe kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo.
Zamani kulikuwa na miiko ya viongozi ambayo iliwataka wasijihusishe na biashara, lakini sasa ni tofauti. Nawaomba Watanzania katika mchakato wa Katiba Mpya wachangie mawazo ambayo yataleta faida kwa umma kama Mwalimu Nyerere alivyopigania wakati wa uongozi wake, anasema.
Madaraka alisema anasikitishwa na baadhi ya viongozi wanaotamba hadharani kwa utajiri walionao huku wakibeza familia ya mwasisi wa Taifa, Mwalimu Nyerere kutokana na umaskini wao.
Madaraka: Taifa limeshindwa kumuenzi Nyerere