Inasikitisha kuona Makao makuu ya Wizara inakuwa na Madaktari zaidi ya 80 ambao wanafanya kazi za kisiasa wakati sisi katika wilaya yetu hatuna Daktari( MD) hata mmoja kwani hata DMO aliepo ni AMO inasikitisha sana. Nchi hii haina chembe kabisa ya equity na fairness. Tukijaribu kufikiria kwa kina kama wachambuzi wa mambo inakuwaje Wilayani hakupelekwi Madktari na badala yake wanalundikwa Makao makuu ya wizara ya Afya hii ni aibu. Au kazi yao hao nikusubiri Madaktari Madaktari wenzao wagome na wao wakazibe pengo.
Naimba serikali baada ya kutatua mgogoro wa Madaktari na kuboresha Maslahi ya Watumishi wote wa sekta ya Afya iwapange kazi Madaktari waliopo makao makuu ya Wizara kwenda katika Wilayani kuokao maisha ya ndugu zetu.
Naimba serikali baada ya kutatua mgogoro wa Madaktari na kuboresha Maslahi ya Watumishi wote wa sekta ya Afya iwapange kazi Madaktari waliopo makao makuu ya Wizara kwenda katika Wilayani kuokao maisha ya ndugu zetu.