Madaktari wa Tanzania kuendelea kudhaminiwa kwenda kusoma Cuba

diana chumbikino

JF-Expert Member
May 29, 2018
428
368
1568011619795.png



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Mhe. Marcelino Medina Gonzalez.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamegusia namna ya kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya Nchi hizo na kumshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufungua ubalozi wa Tanzania Nchini humo.

Pia wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika nyanja za Afya kwa kutoa udhamini kwa Madaktari wa Tanzania kwenda Cuba kwa masomo ya ubobezi,kilimo hususani Kilimo cha miwa ili kuwa na viwanda vya sukari na ujenzi wa viwanda vya dawa hapa Nchini.
 
Back
Top Bottom