Madaktari (PhD) wasipangiwe muda wa kustaafu

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,586
4,273
Nimekuwa nafuatilia wasomi wazuri hasa wa Saiyansi kufikia hatua ya PhD na kuona kuwa kuwastaafisha eti kwa kuwa umri umefika kwamtazamo wangu sio sawa.

Kusoma na kufikia kiwango hicho cha Elimu wengi hufikia kwenye miaka 40 na 50. Naona ni hasara kumuachia mtaalam wa aina hiyo astaaf baada ya kutumikia kisomo chake cha PhD pengine kwa miaka 10 hivi na kustaafu

Kumbuka kuna reseach nyingi zinazotumia muda mrefu sana kuzipatia majibu mfano: Utafiti wa mbegu za Korosho hutumia takribani miaka 25 kupata mbegu/majibu halisi ya utafiti nk

Kitendo cha kuwaachia wataalam wetu wastaffu na kuanza kuwalipa part time (baadhi yao) nafikiri sio sawa; kwa nini wasiendelee hadi watakapo poteza uwezo wa kufanya kazi husika au pengine tuweke miaka 75 hivi?

Nakumbuka mtafiti wetu mmoja mbobezi (nafikiri ndiye alifanikisha utafiti wa Mbegu bora za Mihogo na Korosho ambazo zote ni hot cake hapa Africa na Asia) alistaafu miaka 4au tano hivi iliyopita kwa mujibu wa sheria; Miezi michache baadae Kachukuliwa Nchini Zambia kama mshauri mkuu wa Wizara ya Kilimo; binafsi niliona ni hasara kubwa kwa Taifa letu

Nijuavyo huko Ulaya mtu akishasoma kufikia Level hiyo hakuna kustaaf hadi apoteze uwezo wa kufanya kazi husika
Angazo: Mimi sio msomi wa daraja hilo.
 
Kwa mtazamo wangu naona huo muda wakustafu ubaki vilevile ili ipatikane fursa ya ajira kwa wengine kuhusu swala utaalamu basi mhusika akibakisha miaka mi5 au mi3 kustafu basi anze kuwapa maarifa wanaobaki Over.
 
Retirement is a must by law. He who wants him, will follow him after his retirement. No problem.
 
Kwa mtazamo wangu naona huo muda wakustafu ubaki vilevile ili ipatikane fursa ya ajira kwa wengine kuhusu swala utaalamu basi mhusika akibakisha miaka mi5 au mi3 kustafu basi anze kuwapa maarifa wanaobaki Over
Sio chai hiyo yakusema utampa formula ya kuunga sukari kwenye chai mtu kafanya research miaka 4 -5 halafu watu waelekezwe bila kusoma wakaelewa uwii.
 
Wastaafu tu penshen zao wakaanzishe za kwao tutawafata.

Ukumbuke vijana wamejaa mtaani.
 
Kwa mtazamo wangu naona huo muda wakustafu ubaki vilevile ili ipatikane fursa ya ajira kwa wengine kuhusu swala utaalamu basi mhusika akibakisha miaka mi5 au mi3 kustafu basi anze kuwapa maarifa wanaobaki Over.
Kiongozi; Suala la utafiti, ni zaidi ya kusoma darasani
Inahitaji kipaji BINAFSI na dedication ya hali ya juu; hivyo Doctor anaweza kumuelekeza mtu kile tu alichokuwa anafanya kwa wakati ule ila tutakosa Fursa ya kupata mengi mapya yajayo.
Kimsingi hao watu wa PhD na Prof kwa masomo ya Sayansi wala sio wengi, kwanza tuna upungufu mwingi tu ndio sababu wengi wao huendelea kufanya kazi kwa mkataba ( hivyo hawazuii ajira)
Kimsingi iliniuma kuona mtafiti mbobezi kiasi hicho anaachiwa tu, eti kwa kuwa amefikisha miaka 60? tumetumia muda na gharama kiasi gani kumuandaa/kumsomesha?
 
Wastaafu tu mkuu, kwa sababu hawaandai vijana kwenye maeneo yao ili waendeleze hizo tafiti na hii imetokana na mfumo uliopo nchini kujenga unafiki, woga na ubinafsi. Sasa hii inapelekea hawa maprofessa kwa makusudi kukataa kuwachukua vijana ili waendelee kusikika wao tu miaka yote.
 
Kiongozi; Suala la utafiti, ni zaidi ya kusoma darasani
Inahitaji kipaji BINAFSI na dedication ya hali ya juu; hivyo Doctor anaweza kumuelekeza mtu kile tu alichokuwa anafanya kwa wakati ule ila tutakosa Fursa ya kupata mengi mapya yajayo.
Kimsingi hao watu wa PhD na Prof kwa masomo ya Sayansi wala sio wengi, kwanza tuna upungufu mwingi tu ndio sababu wengi wao huendelea kufanya kazi kwa mkataba ( hivyo hawazuii ajira)
Kimsingi iliniuma kuona mtafiti mbobezi kiasi hicho anaachiwa tu, eti kwa kuwa amefikisha miaka 60? tumetumia muda na gharama kiasi gani kumuandaa/kumsomesha?
Kwa kukazia hapo, wasomi wa viwango hivyo pia wasiruhusiwe kabisa kujihusisha na SIASA maana wakishaenda huko ndio basi tena hata akili zao sijui hua zinayeyukia wapi?
 
Nimekuwa nafuatilia wasomi wazuri hasa wa Saiyansi kufikia hatua ya PhD na kuona kuwa kuwastaafisha eti kwa kuwa umri umefika kwamtazamo wangu sio sawa.

Kusoma na kufikia kiwango hicho cha Elimu wengi hufikia kwenye miaka 40 na 50. Naona ni hasara kumuachia mtaalam wa aina hiyo astaaf baada ya kutumikia kisomo chake cha PhD pengine kwa miaka 10 hivi na kustaafu

Kumbuka kuna reseach nyingi zinazotumia muda mrefu sana kuzipatia majibu mfano: Utafiti wa mbegu za Korosho hutumia takribani miaka 25 kupata mbegu/majibu halisi ya utafiti nk

Kitendo cha kuwaachia wataalam wetu wastaffu na kuanza kuwalipa part time (baadhi yao) nafikiri sio sawa; kwa nini wasiendelee hadi watakapo poteza uwezo wa kufanya kazi husika au pengine tuweke miaka 75 hivi?

Nakumbuka mtafiti wetu mmoja mbobezi (nafikiri ndiye alifanikisha utafiti wa Mbegu bora za Mihogo na Korosho ambazo zote ni hot cake hapa Africa na Asia) alistaafu miaka 4au tano hivi iliyopita kwa mujibu wa sheria; Miezi michache baadae Kachukuliwa Nchini Zambia kama mshauri mkuu wa Wizara ya Kilimo; binafsi niliona ni hasara kubwa kwa Taifa letu

Nijuavyo huko Ulaya mtu akishasoma kufikia Level hiyo hakuna kustaaf hadi apoteze uwezo wa kufanya kazi husika
Angazo: Mimi sio msomi wa daraja hilo.
PhD zipi za korosho? Akina Kabudi? akina Mukandala? Akina Kitila? takataka!
 
katika chuo kikuu sitakitaja nilikutana na professa mmoja mzee wanasema alikuwa vizuri sana na hata alipostaafu walimrudisha alikuwa amezeeka sana ukiongea naye unasubiria ajibu ashalala usingizi niliona wanamtesa yule mzee baadaye nikaja ona taarifa alikufa nadhani mwaka jana..
 
Madaktari wapi? Hawa akina Mwigulu Nchemba? Akina Kigwa wanaoshinda twitter wanasuta na kuchamba? Muda wa kustaafu upunguzwe kabisa ili wapishe vijana mapema
 
Back
Top Bottom