KML
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 861
- 133
Viongoziwa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Jumuiya ya Madaktari na Madaktari waliofukuzwa kazi na wengine kusitishiwa usajili wa leseni zao za muda walikutana jijini Dar es Salaam jana na kupitisha azimio la kuishtaki Serikali na Baraza la Madaktari mahakamani.
Umuzi huo ni matokeo ya ushauri uliotolewa na wanasheria kwa madaktari hao waliopendekeza hatua mojawapo ya kuchukua kuwa ni kulifikisha suala hilo mahakamani.
Mwakilishi wa Madaktari hao, Dk Frank Kagoro, alilimbia gazeti hili kuwa wamefikia hatua ya kwenda mahakamani kudai haki baada ya kugundua kuwa hatua waliyochukuliwa haikuwatendea haki.
"Tumekubaliana kutekeleza usahuri wa wanasheria wetu, tunafikiria kufungua kesi mahakamani kupinga kitendo kilichofanywa na Serikali cha kufukuza baadhi ya madaktari kutokana na mgomo na (MCT) kusitisha leseni za muda kwa baadhi yetu", alisema Dk Kagoro.
Umuzi huo ni matokeo ya ushauri uliotolewa na wanasheria kwa madaktari hao waliopendekeza hatua mojawapo ya kuchukua kuwa ni kulifikisha suala hilo mahakamani.
Mwakilishi wa Madaktari hao, Dk Frank Kagoro, alilimbia gazeti hili kuwa wamefikia hatua ya kwenda mahakamani kudai haki baada ya kugundua kuwa hatua waliyochukuliwa haikuwatendea haki.
"Tumekubaliana kutekeleza usahuri wa wanasheria wetu, tunafikiria kufungua kesi mahakamani kupinga kitendo kilichofanywa na Serikali cha kufukuza baadhi ya madaktari kutokana na mgomo na (MCT) kusitisha leseni za muda kwa baadhi yetu", alisema Dk Kagoro.