Madaktari bingwa Muhimbili waanza ku-resign!

Aliwashangaza wareno walipofika ili kumuhadaa wao wakiwa n aviti vyao vya kukunja,naye akaita kijana hlf akamkalia duh!Very bad.Hawa maqueen walikuwa wabaya sana hata wakifa wanaua mtu wa kuzikwa naye ili akawahudumie kaburini.

Alikua anazikwa mzima, kijana wa miaka 10-15 hivi. All in all this is the fall of JUA KALI, and the rise of.......
 

Dah! Ni Dokta mchapakazi sana huyu mama, nampenda sana sana sana, alikuwa akifanya upasuaji mpaka saa nane za usiku! nadhani ni bora akabadili uamuzi wake pale ward ya watoto watasuffer sana, sijui kama watapata daktari mchapakazi kama huyu SubhanaLLAh ... Dk Mung'ongo rudisha roho nyuma labad kuwe na lingine !
 
Reactions: Aza
ao walio resign wanasehemu za kwenda sio bure!

hata kama wanasehemu za kwenda ni bora kulko kukaa katika sehemu mbovu na huthaminiwi, kuwekewa vikwazo kibao!!hakuna anayependa kufanya kazi akiteseka!!hata kama mafao huwezi mlipa, basi boresha mazingira na kumtia moyo na si maneno ya kukatisha tamaa na ubabe wakyi kiukweli unamtegemea!
 
ni kweli tupu mkuu ,huyu mama ndiyo alikuwa anafanya operation zote za maskini ......madokta wengine wanafanya zile za pesa tu (IPPM).
dah!wanyonge sijui tutakimbilia wapi sisi.
 
Reactions: Aza
Bora wa-Resign watakuja wengine hao wanaotaka 7.7m wa nini jamani?
Walijiuzulu Mawaziri wakaja wengine sembuse hao MaDr wasio wazalendo!
Kwa nini humu ndani mnawatetea wakati mambo yalishaisha, na waliambiwa kuwa atakayeona anaonewa na kupewa ujira mdogo NI BORA AJIONDOE mwenyewe na sio kuanza kuleta chokochoko na Serikali yenu. Serikali yenu haina uwezo wa kuwalipa wanavyotaka wao
 
I respect maamuzi and absolutely was perfect, there were two choices! Kuacha kazi mwenyewe kwa sababu malipo hayatoshi au kufanya kazi kwa terms na malipo yaliyowekwa. Kama umekiuka, lazima sheria ichukue mkondo wake. Tutabembelezana hadi lini sasa.
 
i hope hizi ni tetesi tu kama heading ilivo madaktari tunawaitaji sana kuliko wanasiasa jtj nchi yeyote duniani kwanza li-nchi lenyewe madaktari hawatoshelezi kabisa afu......
 
Kweli hapa JF great thinker ni wachache sana.hivi we unafikiri udaktari ni cheo cha kuteuliwa kama political position? Kama kitu hukijui ni bora kuuficha upumbavu wako kwa kutochangia pumba kama zako.
 

Hawa madokta maslahi waache tu kazi hatuwahitaji, aende akatafute mishahara mikubwa au cdm wamuajiri awe katibu mwenezi wampe mshahara mnono
 
hakuna serikali yoyote duniani ambayo ilifikia hatua ya kuwadharau wanasanyasi, kama nchi ikifikia hatua hiyo basi hiyo ni nchi mfu, ambayo inaongozwa na wanasiasa ambao kazi yao ni kutetea serikali iliyoko madarakani ili wapate kushiba matumbo yao.

Nakumbuka baba wa taifa alikuwa na wazo la kuanzisha kijiji cha sayansi na technologia, kipindi hicho nikiwa form two, tena nasoma sayansi na ufundi niliona ni kama ndoto kwa ujio huo, lakini mpaka leo sijui kiliishia wapi - kilichobaki ni ndoto tu. sasa leo ndiyo nasikia wanasayansi hawatakiwi nchi hii kisa eti wamedai haki zao. Aibu kubwa.

Hii nchi imebaki ni makapi tu, tunaenda bila dira wala mwelekeo: - Namnukuu RIP Katibu Mkuu wa CCM - Kolimba.

1.`Bunge limekosa dira
2. Mahakama zetu mashakani kutenda haki - wanatenda haki kwa vibaka na wizi wa kuku tu, ila kama una hela aisee hufungwi.
3. Serikali haiaminiki kwa wananchi
4. Usalama wa taifa hawatumii mbinu mpya za ulimwengu wa sasa kunasa detective informations, badala yake wanatumia mbinu za miaka ya 47, kutesa na mpaka kuua. Naomba wajifunze kwa mashirika ya kijasusi ya nchi za ulaya, marekani waone wanavyofanya kazi.

Usalama wa Taifa unapogeuka kuwa usalama wa CCM ni hatari wa taifa, badala ya kukamata wanaoiba rasmimali za taifa, kuchukua ardhi ya nchi yetu, wizi wa maliasili hata kusafiisha wanyama nje ya nchi, wao wanajua kumkata Oimboka na kumtesa --- we're at very low level, very low.....

Sasa ikifikia hatua kama hiyo ndiyo sasa tunatafuta mchawi ni nani, Olimboka anatetea haki za wanasayansi wenzake anaambiwa yeye ni mwana Chadema, JASUSI anataka kuangusha nchi. HATUFIKI 2015.
 
Nitaendelea kusema hivi Madakatari wote wanaogoma please wekeni barua zenu za kujiuzuru..Ukicha kazi kwa kujiuzuru unajiondolea wajibu wa kuponyesha watu hivyo watu wanaokufa Hospitalini halitakuwa jukumu lako wala kuhusika. Mwogopeni Mungu hawa watu wanaokufa kila siku kwa mgomo wenu vifo vyao vipo mikononi mwenu Haijalishi sababu gani imemkuta iwe jambazi au serikali imekataa kuwapa mishahara tosha bado ni jukumu lako kumponya mgonjwa unapoweza..

Jiondoe ktk wajibu huu nasi tutawaunga mkono vizuri halafu kama serikali itawahitaji tena basi italazimika kuingia mkataba mpya, wakiwanyang'anya liseni mlisema mtaende nchi nyinginezo kwa hiyo uwezo mnao na mko ktk nafasi nzuri zaidi kuliko serikali yenyewe..
 
Safi sana watanzania tunaumia lakini hatun budi kuwaunga mkono madaktari. Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, muachie ngazi wote mpaka waliofukuzwa warudishwe maana hiyo ndio njia pekee kwa serikali iliiweka mfukoni Bunge na Mahakama.
 

Ni kweli mkuu, hataki kuja kuwa na nyumba kama hii ya "THE ONLY PROFESSOR IN ENDOCRINOLOGY IN EAST AND CENTRAL AFRICA" ipo kule Magu, hivi hii ni nyumba ya daktari professor tena aliyefundisha vijana wengi na madaktari wakubwa pale MUHAS miaka hiyo?

 
Hivi watanzania mlilitoa wapi hili dubwana JKilaza jamani?!!

Ndugu yangu weee utawaweza wajinga waliojaa vijiji! Wanakufa kila uchao lakini pilau ya siku moja, shida zooooooooooooote wanasahau!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…