hakuna serikali yoyote duniani ambayo ilifikia hatua ya kuwadharau wanasanyasi, kama nchi ikifikia hatua hiyo basi hiyo ni nchi mfu, ambayo inaongozwa na wanasiasa ambao kazi yao ni kutetea serikali iliyoko madarakani ili wapate kushiba matumbo yao.
Nakumbuka baba wa taifa alikuwa na wazo la kuanzisha kijiji cha sayansi na technologia, kipindi hicho nikiwa form two, tena nasoma sayansi na ufundi niliona ni kama ndoto kwa ujio huo, lakini mpaka leo sijui kiliishia wapi - kilichobaki ni ndoto tu. sasa leo ndiyo nasikia wanasayansi hawatakiwi nchi hii kisa eti wamedai haki zao. Aibu kubwa.
Hii nchi imebaki ni makapi tu, tunaenda bila dira wala mwelekeo: - Namnukuu RIP Katibu Mkuu wa CCM - Kolimba.
1.`Bunge limekosa dira
2. Mahakama zetu mashakani kutenda haki - wanatenda haki kwa vibaka na wizi wa kuku tu, ila kama una hela aisee hufungwi.
3. Serikali haiaminiki kwa wananchi
4. Usalama wa taifa hawatumii mbinu mpya za ulimwengu wa sasa kunasa detective informations, badala yake wanatumia mbinu za miaka ya 47, kutesa na mpaka kuua. Naomba wajifunze kwa mashirika ya kijasusi ya nchi za ulaya, marekani waone wanavyofanya kazi.
Usalama wa Taifa unapogeuka kuwa usalama wa CCM ni hatari wa taifa, badala ya kukamata wanaoiba rasmimali za taifa, kuchukua ardhi ya nchi yetu, wizi wa maliasili hata kusafiisha wanyama nje ya nchi, wao wanajua kumkata Oimboka na kumtesa --- we're at very low level, very low.....
Sasa ikifikia hatua kama hiyo ndiyo sasa tunatafuta mchawi ni nani, Olimboka anatetea haki za wanasayansi wenzake anaambiwa yeye ni mwana Chadema, JASUSI anataka kuangusha nchi. HATUFIKI 2015.