Madakatari wakosa kauli juu ya Mponda/Nkya

Madakatari wakosa kauli juu ya Mponda/Nkya

Wakati mwingine ukimya ni kauli tosha: hivyo ukimya wa madaktari uchukuliwe kama kauli inayojitosheleza ambayo yahitaji kusikilizwa kwa umakini mkubwa kupata ujumbe wake.
 
Basi kama ni kuboresha maslahi na kama madaktari wanatujali sana wananchi basi wasubiri kwanzA na polisi na walimu mshahara ufike 900,000 halafu na wao ndio tuwapeleke kwenye hayo mabilioni wanayotaka.
 
mgomo bora?....kwa hiyo wanastahili sifa kwa kusababisha vifo.!!!

niambie ni vifo vingapi vimesababishwa na madaktari waliokuwa kwenye mgomo.naamini kwenye takwimu zaidi.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
aaah..madaktari wetu wa internet.,walosahau kuwa wamesomeshwa na kodi za hao hao waliowanyima haki ya kuishi..time will tell..guilty conscience will take its part..:crazy:
 
wewe acha uzuzu, mafundi bomba na mafundi umeme wametapakaa kila kona wakigoma fasta tunawapiga chini tunaajiri wapya. making a doctor ni isue nyingine mjomba. Acheni porojo.


Ukweli ma-dr wameitia doa taaluma/weledi wao. Ma-dr wa tz wamegeuka kichekesho cha dunia.

Wamekosa busara na hekima za kawaida kabisa ambazo hata konda na wasukuma mikokoteni wanazo.

Wamekalia tamaa na ulafi wa pesa, hata kama watz wenzao watakufa.

Wanatukuza taaluma yao kana kwamba wao ni miungu watu. Hawajui kuwa mkulima asipolima na kuwauzia chakula hawataishi.

Mtumishi wa DAWASCO akigoma kuwapa maji wanajua hali itakavyokuwa. Fundi wa TANESCO akigoma kumpa umeme anajua matokeo yake. Hata mzoa taka pale hosp akigoma dr hawezi kufanya kazi.

Wamekosa uelewa mdogo ....kwamba tunategemeana sana kila mtu kwa fani yake. Kwa kifupi uwezo wao wa kufikiri ni kichekesho na wamegeuka vilaza wanaokimbizana na pesa.
 
MS JUDITH, unazijua symptoms of profound mental retardation?

unajua mtu anakaa kuropoka tu aafu anataka aonekane naye amechangia. We unalinganisha daktari na mtu wa sociology kuna usawa gani? Daktari anasoma five years ukiongeza na internship inajuwa sita just for first degree we si unakuwa umemaliza mpaka phd? muwe mnafuatilia na nchi zingine wanalipwa kiasi gani,siyo just kukurupuka na inferiority complex na kusema tuko sawa kama kauli mbiu za vikao vya wanawake. Daktari hana weekend wala sikukuu na anafanya kazi 24 hours, wao wanafanya kazi masaa mangapi? Watu wawe wanajiuliza,ulishawahi kwenda hospitali ukaambiwa huu siyo muda wa kazi? Ulishawahi fika hospitali baada ya muda kuisha ukaambiwa njoo kesho. Kuna appointment ambazo doctor anakubaliana na mgonjwa wake kulingana na hali ya mgonjwa na uwezo wa hospitali. Tunatambua uwepo wa wengine na waliotuwezesha kufika hapa lakini we are not equal in importance, hata kichwa maji wa nchi hii aliwaambia!
 
Basi kama ni kuboresha maslahi na kama madaktari wanatujali sana wananchi basi wasubiri kwanzA na polisi na walimu mshahara ufike 900,000 halafu na wao ndio tuwapeleke kwenye hayo mabilioni wanayotaka.

unataka nani adai haki yako? Ndo maana mnanyanyaswa na mnakaa kimya. Mnatukanwa na ps wa mabosi wenu mnasubiri Mungu ndo aje awaokoe. Lazima ujifunze kupigania heshima yako na haki yako ndo utaipata..
 
kuna wengine humu wanaandika tu kwa sababu hatuwaoni au wamekane wanachangia hoja. Siku wakikutana na daktari wanakuwa wa kwanza kusema ooh,unajua serikali hii haijali watu wa afya, ooh mnafanya kazi kwenye mazingira magumu na maneno kibao. Hawa ni sawa na wadada ukiwakuta kwenye vikao vyao wanaanza kusema, mi nikiugua/nikiwa mjamzito daktari wa kiume hawezi kunihudumia! Siku akifika hospitali anakuwa wa kwanza kukufunulia nguo hata kabla hujamwambia afanye hivyo. Mi huwa nawaenjoy tu na maneno yao! The best thing,badala ya kupiga kelele zisizo na msaada ni bora ukawekeze kwa mdogo wako au mwanao asome sayansi awe daktari!!
 
Wakati mwingine ukimya ni kauli tosha: hivyo ukimya wa madaktari uchukuliwe kama kauli inayojitosheleza ambayo yahitaji kusikilizwa kwa umakini mkubwa kupata ujumbe wake.


Mkuu umegonga msumari kichwani! Docs walikutana na JK wakakubaliana mambo na akaahidi kuyatekeleza makubaliano. Asipotekeleza walichokubaliana bado lolote laweza kutokea Docs watakapokutana kupeana feed back ya swala zima lilivyoenda! Ndo maana jamaa kajibu vema - "Raisi alikuwa anaongea na wazee wa Dsm"!!!
 
wapendwa,

hawa madaktari ni watu wa ajabu sana na tena ni wenye dharau kupita kiasi, wauaji wakubwa! hivi wasingebahatika kusoma kabisa wangekuwa na uelewa wa kiwango gani?

sasa mbwembwe zole zooote hadi kuuua ndugu na wapendwa wetu bila hatia yoyote, dawa yao ilikuwa ni juice ya ikulu? kwani hawakujua kabisa kuwa hawana uwezo wala uhalali wa kupanga baraza la mawaziri? pinda laishawaambia ukweli, wakamdharau! hivi kama kitu kile kile pinda alichosema kikashindwa kuwaridhisha, kiliporudiwa na jk kimewaridhisha, sasa tuwaeleweje? mbona akili kidogo tu hata inayotosha kwenye kijiko cha chai ingetosha kujua kuwa kwa unyeti wa sekta ya afya, hawapaswi kugoma? hawa wenzetu wana akili yenye ukubwa gani?

mtu akisikia mgomo anadhani ni jambo la kihunihuni, kumbe mgomo ni suala la kisheria na limeainishwa kisheria sababu pamoja na taratibu zake. sasa watwambie mponda na nkya hawang'oki na hawapewa hata senti moja hadi hivi sasa, hicho walichoahidiwa na jk ndicho alichwaahidi pinda, kwa nini walimpuuza pinda na kuua watu wasio na hatia?

hebu angalieni, daktari anaanza na mshahara wa laki 9+, sekta nyingine mtu mwenye shahada anaanza na laki 4+! hivi hata hapo hawaoni kuwa serikali inawachukulia kwa uzito mkubwa zaidi ya kada nyingine? hayo majivuno yao na kujiona kada yao iko juu ya kada nyingine ndiyo ya kukemewa kwa nguvu zote. kila mtu anajua nchi ilipo kiuchumi, hiyo neema wanayolilia kila siku, wanategemea itatoka nchi gani? au kila mtanzania ageuzwe ng'ombe akamuliwe maziwa (kodi) na maziwa yote wanyweshwe madaktari pekee?

napenda serikali ichukue hatua kuimarisha sekta ya afya pamoja na sekta nyingine, lakini nimehuzunishwa sana na uelewa wa mambo wa madaktari wetu pamoja na viwango vya upendo na maadili ya kazi zao walionao.

kumradhi wote niliowaudhu kwa maoni haya,

mbarikiwe sana

Glory to God!

Lazima weye ni mmoja wa waliopata kikombe cha uzima cha babu! Na kama ulikipata na ukakiamini kwa nini una wasi wasi na madaktari wakigoma au la? Kama wanakiburi na ni wauaji kwa nini rerikali iwaruhusu wananchi wake waende kwa wauaji? Je tushtaki serikali kwa kuwapeleka kwa wauaji?

Hivi huo mshahara wa laki tisa, ni take home au ni baada ya kukatwa kodi? Hivi wakina Ngeleja tulisikia walilipwa posho ya miliono nne kwa siku, hivi hawa hawawaonei huruma watanzania walala hoi? Hivi hawa hawajasomewhwa na kodi za watanzania??


Hivi BoT, TRA, bandarini, TANAPA sio za watanzania hizi? Mishahara yao mbona ipo tofauti? Kwani wao wana haki gani kulipwa zaidi ya mwalimu au polisi? Je mhudumu tu anaanza na mshahara wa tsh ngapi?

Acheni propaganda kwenye masuala ya muhimu... Kwa hiyo mnavyoona madaktari wamekaa kimya nyie mnashangilia kuwa mmeshinda?? ( sidhani kama ni wajinga kiasi hicho, kama hatujifunzi kwa walimu na ubora wa elimu, ngojea tuone kwa ukimya wa madaktari kwa wagonjwa, labda itatushtua maana inahusisha uhai!

Najisikitikia kuwa Mtanzania mnyonge maana sina mtetezi.
 
mgomo wa madaktari utabakia kuwa mgomo bora kuwahi kutokea tanzania.busara waliyoonyesha madaktari ni kubwa kama ilivyotegemewa kutoka kwao.

Bint yangu ms judith naona wewe ni mchochezi usiyeamini kwenye maridhiano.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

hapana baba yangu!

mimi si mchochezi. mimi sioni maridhiano yoyote, naona kiburi tu na majivuno ya madaktari wakijioona bora zaidi ya wengine. zaidi sana naona dharau yao kwa pinda. huwezi kwenda ikulu ukitarajia kufikia maridhiano na rais kuhusu nani awe waziri wa wizara ipi na nani awe naibu waziri wake. huo ni utoto na kupoteza muda bure, na umesababisha upotevu wa maisha ya watu wasio na hatuia. sioni tofauti yake na ujambazi!


Ms Judith, salaam sana,karibu tena jamvini ulipotea muda hivi.

Huo mshahara wa laki 9(900,000) kwa mwezi (siku 30) ni sawa na posho iliopendekezwa ya mbunge akikaa katika kiti chake kwa siku 4.5.( jumatatu-alhamisi na ijumaa hadi saa 6 mchana) Ni posho nasisitiza. Sijui hawa ni muhimu sana kuliko kada zingine!!

Spika Makinda alisema wabunge wa Kenya wanawacheka wa Tanzania, na nina hakika madaktari wa Kenya wanawacheka wa Tanzania. Sasa hapo kuna ubaya gani wakiomba waongezewe kama wabunge walivyoomba?

Kada nyingine kama walimu nao wanadai, umesahau Tucta ya mgaya ilikuwa inalalimikia nini. Kama Polisi na mabwana shamba kwa mfano, wameridhika na wanachopata kwanini wawazuie wengine wasidai haki zao?

Kuhusu Nkya na Mponda wao wamesema waendelee kuwepo kama ni busara lakini hawatawapa ushirikiano. Mdau wa sekta ya afya ni nani zaidi ya wataalamu waliomo. Mponda ni mpita njia tu kesho anaweza kuwa ujenzi n.k. Kama uwepo wake utakwaza watu kwanini wasifikirie wao kwanza halafu rais naye apime. Neno kutotoa ushirikiano ni pana na linagusa sehemu kubwa sana.

Ahsante

asante sana mpendwa Nguruvi3,

mi sijambo na nashukuru kunikaribisha tena hapa jamvini.

sikatai kuwa baadhi ya maamuzi ya serikali yakiwemo ya kuweka viwango vya mishahara , marupourupu na posho mbalimbali kwa kada mbalimbali hapa nchini kwetu hayana dosari. zipo na tena nyingine ni za waziwazi sana hata mtoto mdogo anaweza kuzikosoa. ila naomba tukubaliane kuwa hatutakuja kulingana mishahara, marupourupu na posho watumishi wote wa umma nchini kwetu. na sidhani kama kuna nchi ambayo imeishafikia usawa kama huo.

ninachokosoa ni khako katabia ka madaktari kuringa na kufanya mambop ya kitoto hadfi kusababisha vifo. baadhi ya madai yao ni ya msingi (kama nyongeza za maslahi yao, mazingira bora ya kazi na upatikanaji wa vitendea kazi) na mengine ni ya kitoto (kama hayo ya kuondolewa kwa mponda na nkya wizara ya afya na malipo ya mshahara wa 7.5 hadi 17milioni)

pia nawakemea kwa kiburi na majivuno yao ya kumdharau pinda na kuzidharau sheria za nchi. wanaitisha mgomo wao kihuni kupitia professional association badala ya chama cha kisekta chenye uwezo wa kubargain kwa niaba yao kisheria. wanagoma bila kutoa notisi ya mgomo ya siku 30 kama sheria inavyotaka wala hawahangaiki kusajili madai yao ya maslahi kwa ajili ya arbitration kama inavyotamka sheria. vipi kama kada nyingione nazo zikijifanyia mambo kihunihuni namna hii, nchi itatawalika?

tafakari mpendwa

ubarikiwe sana

kama madaktari ni wauwaji ukiugua baki hapo nyumbani kwako. tuone kama wakati unakata roho hutaita daktari kwa sauti kuu.

na kwa kauli yako hii wewe ukiugua ni kifo tu, kisaikologia huwezi kupona kamahuna imani na daktari anaye kutibu. pole you are a deadly walking body.

mpendwa,

soma post yangu #13 hapo juu

mbarikiwe sana wapendwa wote

Glory to God!
 
aaah..madaktari wetu wa internet.,walosahau kuwa wamesomeshwa na kodi za hao hao waliowanyima haki ya kuishi..time will tell..guilty conscience will take its part..:crazy:

hukumu ni zake Mwenyezi Mungu aketiye juu ya kiti cha enzi na Mwana Kondoo

Glory to God!

unajua mtu anakaa kuropoka tu aafu anataka aonekane naye amechangia. We unalinganisha daktari na mtu wa sociology kuna usawa gani? Daktari anasoma five years ukiongeza na internship inajuwa sita just for first degree we si unakuwa umemaliza mpaka phd? muwe mnafuatilia na nchi zingine wanalipwa kiasi gani,siyo just kukurupuka na inferiority complex na kusema tuko sawa kama kauli mbiu za vikao vya wanawake. Daktari hana weekend wala sikukuu na anafanya kazi 24 hours, wao wanafanya kazi masaa mangapi? Watu wawe wanajiuliza,ulishawahi kwenda hospitali ukaambiwa huu siyo muda wa kazi? Ulishawahi fika hospitali baada ya muda kuisha ukaambiwa njoo kesho. Kuna appointment ambazo doctor anakubaliana na mgonjwa wake kulingana na hali ya mgonjwa na uwezo wa hospitali. Tunatambua uwepo wa wengine na waliotuwezesha kufika hapa lakini we are not equal in importance, hata kichwa maji wa nchi hii aliwaambia!

mpendwa,

hivi PhD unaijua vizuri kweli? tuambie ni sociolojia ya wapi uliyokuta miaka mitano tu, mtu anasoma kuanzia bachelor hadi PhD. halafu urudi hapa utuambie wanasheria wanasoma miaka mingapi kupata LLB, na ukip[ata muda utuletee na miaka wanayosoma wahandisi.

hayo ya kufanya kazi 24/7, jaribu pia kupita na tanesco, polisi, magereza, dawasco, fire nk uulize wanapumzika lini kabla ya kuja hapa. kama ukikosa nauli, muulize hata huyu konda wa daladala hapo kituoni akuambie huwa anapumzika lini na saa ngapi.

jaribu kujibu hoja na sio kuleta visingizio. huko mahospitalini sio kila mtu ni daktari. hata wao ulisikia wanawakana wauguzi kuwa si madaktari (majivuno? kiburi? ubaguzi?). pia sio mahospitalini tu watu hufanya kazi sehemu nyingi sana 24/7 ila ni kugawana majukumu tu ndio humpa mtu muda wa kupumzika na sio kwamba ofisi imefungwa. pia ujue si hospitali zote hutoa huduma 24/7. na hata muhimbili kwenyewe si division zote hutoa huduma 24/7. inaonekana unahitaji kurudi darasani ujue vizuri maana ya "organization"


ubarikiwe sana

unataka nani adai haki yako? Ndo maana mnanyanyaswa na mnakaa kimya. Mnatukanwa na ps wa mabosi wenu mnasubiri Mungu ndo aje awaokoe. Lazima ujifunze kupigania heshima yako na haki yako ndo utaipata..

kupigania heshima na maslahi, sawa lakini sio kihuni kama walivyofanya madaktari bali kwa kufuata sheria za nchi

Lazima weye ni mmoja wa waliopata kikombe cha uzima cha babu! Na kama ulikipata na ukakiamini kwa nini una wasi wasi na madaktari wakigoma au la? Kama wanakiburi na ni wauaji kwa nini rerikali iwaruhusu wananchi wake waende kwa wauaji? Je tushtaki serikali kwa kuwapeleka kwa wauaji?

Hivi huo mshahara wa laki tisa, ni take home au ni baada ya kukatwa kodi? Hivi wakina Ngeleja tulisikia walilipwa posho ya miliono nne kwa siku, hivi hawa hawawaonei huruma watanzania walala hoi? Hivi hawa hawajasomewhwa na kodi za watanzania??


Hivi BoT, TRA, bandarini, TANAPA sio za watanzania hizi? Mishahara yao mbona ipo tofauti? Kwani wao wana haki gani kulipwa zaidi ya mwalimu au polisi? Je mhudumu tu anaanza na mshahara wa tsh ngapi?

Acheni propaganda kwenye masuala ya muhimu... Kwa hiyo mnavyoona madaktari wamekaa kimya nyie mnashangilia kuwa mmeshinda?? ( sidhani kama ni wajinga kiasi hicho, kama hatujifunzi kwa walimu na ubora wa elimu, ngojea tuone kwa ukimya wa madaktari kwa wagonjwa, labda itatushtua maana inahusisha uhai!

Najisikitikia kuwa Mtanzania mnyonge maana sina mtetezi.


mpendwa, mbona unataka kunivunja mbavu bila sababu?

mimi nikanywe takataka za loliondo? hahahaaaa....

hayo ya TRA, BOT, TANAPA etc, soma nilinyomjibu Nguruvi3 hapo juu

mbarikiwe sana wapendwa

Glory to God!
 
  • Thanks
Reactions: Tom
Ukweli ma-dr wameitia doa taaluma/weledi wao. Ma-dr wa tz wamegeuka kichekesho cha dunia.

Wamekosa busara na hekima za kawaida kabisa ambazo hata konda na wasukuma mikokoteni wanazo.

Wamekalia tamaa na ulafi wa pesa, hata kama watz wenzao watakufa.

Wanatukuza taaluma yao kana kwamba wao ni miungu watu. Hawajui kuwa mkulima asipolima na kuwauzia chakula hawataishi.

Mtumishi wa DAWASCO akigoma kuwapa maji wanajua hali itakavyokuwa. Fundi wa TANESCO akigoma kumpa umeme anajua matokeo yake. Hata mzoa taka pale hosp akigoma dr hawezi kufanya kazi.

Wamekosa uelewa mdogo ....kwamba tunategemeana sana kila mtu kwa fani yake. Kwa kifupi uwezo wao wa kufikiri ni kichekesho na wamegeuka vilaza wanaokimbizana na pesa.

SB na Ms Judith;
Unayoongea yana ukweli, lakini siyo practical. Hao wote wanafanya hayo si kwa faida ya madaktari, kila mtu ni kwa faida yake, we unadhani huyo mkulima asipouza mazao yeye atapata wapi mahitaji mengine? na atalimaje kama anaugua bila kupata matibabu? Unaleta mambo ya kufikirika ambayo hayawezekani. Unayajua kwa kina madai yote ya madaktari au unalijua hilo tu la kusimamishwa kazi mawaziri?
 
mis judith, nimekuambia miaka sita ya kumaliza na internship. Degree ya sociology ni three yrs, mph one yr na phd 3 years. Mpaka daktari anahangaikia mambo ya usajili miaka saba imeshakwisha. Ndo maana nikakwambia tafuta na nchi nyingine madaktari wanalipwaje na hao wengine wanalipwaje. Lawyer ni miaka mitano kwa ud na minne kwenye vyuo vingine pamoja na law school ambayo ilikuwa ni internship zamani.Ndo maana hizo profession wanafundishwa in international standards. Madaktari walijua kugoma ni kinyume na sheria ndo maana wakaamua kugoma ili kushinikiza mambo yao yasiyotatuliwa kwa miaka mingi yafanyiwe kazi. Hii ilikuwa ndo option ya mwisho. Unajua kwamba sheria ya kazi ya mwaka 2004 inataka kila mtu anayekuwa kazini kwa muda wa ziada anatakiwa alipwe 50 percent ya mshahara wake? Mbona haifanyiwi kazi na doctors wanalipwa elfu kumi for 24 hours? Hizo ofisi unazosema zinafungwa hospitali ni za wale co-workers wa sekta ya afya kama wahasibu, sekretaries na outpatient departments. Ofisi ya daktari na nesi haifungwi,ndo maana kuna watu wanaitwa on call workers. Hivi hao watu wa maji, umeme unaowazungumzi uliwahi waita kwako usiku kuja kurekebisha kitu wakaja? Ofisi zao umewahi kuhudumiwa usiku? Mpaka transfoma zilipuke ndo wanakata umeme wa eneo hilo ili kesho waje warekebishe.
 
SB na Ms Judith;
Unayoongea yana ukweli, lakini siyo practical. Hao wote wanafanya hayo si kwa faida ya madaktari, kila mtu ni kwa faida yake, we unadhani huyo mkulima asipouza mazao yeye atapata wapi mahitaji mengine? na atalimaje kama anaugua bila kupata matibabu? Unaleta mambo ya kufikirika ambayo hayawezekani. Unayajua kwa kina madai yote ya madaktari au unalijua hilo tu la kusimamishwa kazi mawaziri?

eti tanesco wasipoleta umeme, dawasco wasilete maji. Khaa! Mbona hospitali nyingi na vituo vya afya havina umeme? Doctors walishazoea kufanya kazi kwa tochi na kandili, wananawa normal saline, nguo zinafuliwa kwa maji ya visima, sterilization inafanyika kwa moto wa mkaa. Sasa unadhani daktari ataona umuhimu wa hao watu? Kwa lipi? Ofisi ya daktari haihitaji computa kwamba ikizima information zinakuwa hazipo!
 
  • Thanks
Reactions: Tom
Pretoria - Health Minister Aaron Motsoaledi announced major wage increases for medical professionals at a media briefing at the Union Buildings on Wednesday, in a bid to stall further strike action.

Government has agreed to raise some salaries to about double what was offered in April, meaning some of the country's lowest-paid doctors will get up to a 53% pay increase.

Motsoaledi said however that the government did not have enough money to increase doctors' salaries by 50% across the board.

The new packages will cost the state more than R1bn, and will be implemented as of July 1, if accepted by the SA Medical Association (Sama).

Motsoaledi apologised for the 11-month delay in meeting the demands of doctors and other medical professionals. "We were wrong in this case," he said, speaking at an "extraordinary" media briefing, taking place outside the Public Service Bargaining Council.

Discrepancies in salaries

He said the briefing was necessary as much of the negotiations seemed to be taking place through the media in the highly publicised issue, with incorrect figures being bandied about.

One of the major challenges was the major discrepancies in salaries for the same position. "For instance in an attempt to retain skills, provinces and institutions ended paying medical professionals different salaries in a desperate bid to retain and recruit especially in rural areas. For example, some provinces advertise positions at higher levels and end up appointing junior doctors in those positions."

Thus doctors across the board received varying increases to bring particular ranks to a single salary structure.

However rural allowances would still remain.

Summary of raises

Interns will receive a total package of R 314,023 pa. This represents an increase ranging from 31% to 53%, with the lowest-paid receiving a 53% increase and the highest-paid receiving a 31% increase to arrive at the same package.

The proposed salary package for medical officers (community service) who are contracted for a year, will move from a range between R330 226 – R357 524 to a total salary package of R392 599. This represents a differentiated increment ranging from 9.8% to 18.9% to address the inequalities.

"Principal and chief specialists (professors) have been very difficult to retain in the system due to their high level skill, " Motsoaledi said.

Packages for principal specialists move from R769 271 to R962 174, which represents a 25.1% increase. Chief specialist (professor) packages move from R932 399 to R1.2m, which represents a 29% increase.

He pointed out that one of the most problematic areas of the present salary structure is that those who decide to study further and specialise (registrars), took a major drop in salary. "In order to address this disincentive to study, we are increasing registrar salaries from 18.3% to 60.1% to arrive at a salary package of R528 770, from a low of R330 226 to a high R446 853."

The government dealt with Sama, an affiliate of Cosatu, in the negotiations. Sama did not condone the strike action carried out in parts of KZN and Free State, by some doctors.

Motsoaledi called the threatened strike action - illegal for doctors - a "highly abnormal" situation, which he hoped the country would never experience again.

He said he hoped the revised offer would halt further protests by doctors.

1Rand=TZS 207
 
Inakuwaje wanakosa cha kusema na walishajiwekea masharti ya kuacha mgomo? Tatizo haliko kwa waziri wala naibu wake....it is the system in the ministry...kuwatoa na kuweka wengine will not solve the problem but can make it more worse than before....THINK BEFORE U ACT DO N'T BE LIKE NARROW MINDED GUYS.....this is just a comment and challenge 2 people...

Kuamua kusema au kutosema wao ma drs ndio wanaojua lipi litaleta matokeo mazuri kwao, kama wameamua kutosema basi ni kwa sababu wameona faida ya hilo ni kubwa.
Mimi naona tatizo kubwa liko kwa hao Mawaziri ambao tokana na UONGOZI ama DESTURI mbaya za serikali ya CCM basi wamejaa majibu ya kejeli na kutowajibika kwa RAIA - pamoja na hao madaktari. Kama ukiondoa hao mawaziri, na wengine wasiofaa basi utakua umeshabadilisha system kwa kiasi - kila kitu kina mwanzo.
 
yaani mis judith nahisi una matatizo au ni bifu la kukosa kusoma udaktari kama la blandina. Unalinganisha daktari na polisi? Wana vyeti gani hao mpaka wasimamie kwamba kulingana na elimu tuliyonayo tulipwe fedha kadhaa? Mimi nitaonaje umuhimu wa polisi wakati naibiwa kila siku, tunakabwa njiani na kubambikiwa kesi? Kazi yao ni ipi kwa profesion ipi waliyosomea? Ndo maana huko huko kuna makundi za wanaolipwa vizuri na kurubuniwa kuwakandamiza wale wasio na professions. Uliona msimamo wa madaktari kuanzia md mpaka professors? Unaweza kupata msimamo huo kwa polisi? We unataka kuniambia konda na daktari kazi yao sawa, kweli umedharau sana! Mtu mwenye gari lake ataonaje umuhimu wa konda? Ni utaratibu tu wa hii nchi kwa sababu ya wizi mlionao, nchi zingine gari hazina konda abiria mnajichangisha na kumkabidhi dereva nauli. Kwa wengine ni kama utaratibu wa kwenye kivuko, unalipa nauli kwanza ndo unaingia kwenye gari na wanaufuata.
 
wapendwa,

hawa madaktari ni watu wa ajabu sana na tena ni wenye dharau kupita kiasi, wauaji wakubwa! hivi wasingebahatika kusoma kabisa wangekuwa na uelewa wa kiwango gani?

sasa mbwembwe zole zooote hadi kuuua ndugu na wapendwa wetu bila hatia yoyote, dawa yao ilikuwa ni juice ya ikulu? kwani hawakujua kabisa kuwa hawana uwezo wala uhalali wa kupanga baraza la mawaziri? pinda laishawaambia ukweli, wakamdharau! hivi kama kitu kile kile pinda alichosema kikashindwa kuwaridhisha, kiliporudiwa na jk kimewaridhisha, sasa tuwaeleweje? mbona akili kidogo tu hata inayotosha kwenye kijiko cha chai ingetosha kujua kuwa kwa unyeti wa sekta ya afya, hawapaswi kugoma? hawa wenzetu wana akili yenye ukubwa gani?

mtu akisikia mgomo anadhani ni jambo la kihunihuni, kumbe mgomo ni suala la kisheria na limeainishwa kisheria sababu pamoja na taratibu zake. sasa watwambie mponda na nkya hawang'oki na hawapewa hata senti moja hadi hivi sasa, hicho walichoahidiwa na jk ndicho alichwaahidi pinda, kwa nini walimpuuza pinda na kuua watu wasio na hatia?

hebu angalieni, daktari anaanza na mshahara wa laki 9+, sekta nyingine mtu mwenye shahada anaanza na laki 4+! hivi hata hapo hawaoni kuwa serikali inawachukulia kwa uzito mkubwa zaidi ya kada nyingine? hayo majivuno yao na kujiona kada yao iko juu ya kada nyingine ndiyo ya kukemewa kwa nguvu zote. kila mtu anajua nchi ilipo kiuchumi, hiyo neema wanayolilia kila siku, wanategemea itatoka nchi gani? au kila mtanzania ageuzwe ng'ombe akamuliwe maziwa (kodi) na maziwa yote wanyweshwe madaktari pekee?

napenda serikali ichukue hatua kuimarisha sekta ya afya pamoja na sekta nyingine, lakini nimehuzunishwa sana na uelewa wa mambo wa madaktari wetu pamoja na viwango vya upendo na maadili ya kazi zao walionao.

kumradhi wote niliowaudhu kwa maoni haya,

mbarikiwe sana

Glory to God!
Tumeona uwezo wako wa kufikiri
 
mis judith, nimekuambia miaka sita ya kumaliza na internship. Degree ya sociology ni three yrs, mph one yr na phd 3 years. Mpaka daktari anahangaikia mambo ya usajili miaka saba imeshakwisha. Ndo maana nikakwambia tafuta na nchi nyingine madaktari wanalipwaje na hao wengine wanalipwaje. Lawyer ni miaka mitano kwa ud na minne kwenye vyuo vingine pamoja na law school ambayo ilikuwa ni internship zamani.Ndo maana hizo profession wanafundishwa in international standards. Madaktari walijua kugoma ni kinyume na sheria ndo maana wakaamua kugoma ili kushinikiza mambo yao yasiyotatuliwa kwa miaka mingi yafanyiwe kazi. Hii ilikuwa ndo option ya mwisho. Unajua kwamba sheria ya kazi ya mwaka 2004 inataka kila mtu anayekuwa kazini kwa muda wa ziada anatakiwa alipwe 50 percent ya mshahara wake? Mbona haifanyiwi kazi na doctors wanalipwa elfu kumi for 24 hours? Hizo ofisi unazosema zinafungwa hospitali ni za wale co-workers wa sekta ya afya kama wahasibu, sekretaries na outpatient departments. Ofisi ya daktari na nesi haifungwi,ndo maana kuna watu wanaitwa on call workers. Hivi hao watu wa maji, umeme unaowazungumzi uliwahi waita kwako usiku kuja kurekebisha kitu wakaja? Ofisi zao umewahi kuhudumiwa usiku? Mpaka transfoma zilipuke ndo wanakata umeme wa eneo hilo ili kesho waje warekebishe.

hapo penye bluu ndio panadhihirisha uhuni wao.


yaani mis judith nahisi una matatizo au ni bifu la kukosa kusoma udaktari kama la blandina. Unalinganisha daktari na polisi? Wana vyeti gani hao mpaka wasimamie kwamba kulingana na elimu tuliyonayo tulipwe fedha kadhaa? Mimi nitaonaje umuhimu wa polisi wakati naibiwa kila siku, tunakabwa njiani na kubambikiwa kesi? Kazi yao ni ipi kwa profesion ipi waliyosomea? Ndo maana huko huko kuna makundi za wanaolipwa vizuri na kurubuniwa kuwakandamiza wale wasio na professions. Uliona msimamo wa madaktari kuanzia md mpaka professors? Unaweza kupata msimamo huo kwa polisi? We unataka kuniambia konda na daktari kazi yao sawa, kweli umedharau sana! Mtu mwenye gari lake ataonaje umuhimu wa konda? Ni utaratibu tu wa hii nchi kwa sababu ya wizi mlionao, nchi zingine gari hazina konda abiria mnajichangisha na kumkabidhi dereva nauli. Kwa wengine ni kama utaratibu wa kwenye kivuko, unalipa nauli kwanza ndo unaingia kwenye gari na wanaufuata.

mpendwa,

mi sikjui unafanya kazi gani na wapi. mimi kazini kwangu ni mkuu wa kitengo changu, nina katibu muhtasi na kitengo changu kina gari moja kwa ajili ya shughuli za kiofisi. mimi simu yangu haipaswi kuishiwa credit wala chaji manake naweza kutakiwa kazini wakati wowote hata usiku au nikiwa likizo. katibu wetu na dereva wa gari letu nao hawatakiwi kuzima simu zao wala kuishiwa chaji kwa kuwa nao wanaweza kuatakiwa ofisini wakakti wowote na siku yoyote!

ninachosema hapa ni kuwa kuna wafanyakazi wengi sana sehemu mbalimbal;i wanaoweza kuitwa on call workers na si madaktari pekee. jaribu kupiga simu tanesco, polisi, fire nk usiku, itapokelwa na mtu! hata hapo nyumbani kwako ukimwamsha mfanyakazi wako ataamka! utumishi wa umma umeweka utaratibu wa malipo ya masaa ya ziada kazini kwa kada zote kwa kuzingatia ukweli huu. hivyo daktari naye anapata masaa ya ziada kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa kwenye kada yake. kama kuna mapungufu, zipo pia taratibu za majadiliano yanayolenga kuboresha maslahi, taratibu ambazo madaktari hawakutaka kuzifuata.

acha kudharau kazi za wengine. dharau ni mwiba mkali sana wa maendeleo. hakuna nchi iliyoondelea kwa jitihada za madaktari pekee bali kwa ushirikiano wa wafanyakazi wote wa maofisini, mashambani na kwingineko. pia uache tabia ya kutukuza vyeti, heshimu kila mtu, msomi na asiyekuwa msomi. hapo ndipo tutakapoiendeleza nchi yetu!

asante na ubarikiwe sana mpendwa

Glory to God!

 
Back
Top Bottom