Ndege kongwe zaidi aina ya Boeing 747 ambayo bado inatoa huduma za usafiri wa anga hadi sasa ni ya Mahan Air ya Iran.
Ndege hiyo yenye usajili EP-MEE, ilianza kufanya kazi kwa mara ya kwanza mnamo Septemba 1990 na kuifanya kuwa na umri wa zaidi ya miaka 35.
Ndege hiyo ambayo hapo awali iliwasilishwa kwa United Airlines, sasa inaendesha njia za kikanda katika Mashariki ya Kati na Asia.
Air China inashikilia nafasi ya pili ya kuwa na ndege ya Boeing 747 inayotoa huduma ya abiria.
Ndege yake aina ya Boeing 747-400, iliyosajiliwa B-2447, ilitolewa mpya mwaka wa 1995. Tofauti na ndege ya Mahan, Air China hutoa mchanganyiko wa njia za ndani na kimataifa, ikiwa ni pamoja na safari za ndege kati ya Beijing, Shanghai, na Shenzhen.
Wakati mashirika mengi ya ndege ya kimataifa yamestaafisha ndege zao za B747, wachache wamesalia katika matumizi ya abiria.
Lufthansa, Rossiya, Korean Air, na Air China zinaendelea kurusha B747-400 au toleo jipya zaidi la B747-8.
Lakini kadri ndege zinavyokuwa za kisasa na shinikizo la ufanisi wa mafuta kuongezeka, ndege hizi za jumbo zilizobaki zinaweza kutoweka hivi karibuni.