Macho makavu - aibu tena ya kike hakuna?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995



Sijui ndio uzee wenyewe au ni mimi tu. Zamani (sasa hapa msianze kuniuliza zamani ya lini) watu walikuwa wanazungumza mambo ya mapenzi kwa staha, heshima, na kujali nani anasikiliza. HIvyo, kuna mambo ambayo dada zetu hasa wasingeweza kuyazungumza mchana kweupe namacho makavu. Walikuwa na haya au soni fulani hivi ambazo kwa kweli zilikuwa zinawafanya waonekane very sexy.

Isipokuwa tu wakishazoeana basi zile soni zinahamia hata chumbani kidogo na kama ni utundu basi ni wa wao wawili huko ndani na hata maneno ya kuchombezana yanafanywa wakiwa wao wenyewe. Lakini siku hizi - sasa msiniulize hizi nazo zimeanza lini - dada zetu ni kama hawana tena soni. Iwe ya hadharani au chumbani. Wanaweza kuzungumza mambo fulani ya kiutuuzima hadi ukashangaa. Tena wengine wanazungumza bila hata kujali kama baba, kaka au mume anaweza kujua anazungumza lugha hiyo. Yaani, kuna lugha fulani ya matusi matusi ambayo siwezi kushangaa inaweza kuwa ni turn off kwa wanaume wengi kwani pamoja na ujanja wote wanaume bado wanapenda msichana au binti mwenye staha kidogo, soni za kuchombezea na aibu fulani fulani za kike.

Kwa mfano, msichana anayepita halafu sketi ikapeperuka kidogo kujiachia akafanya haraka kujifunika au kuvuta kanga anaweza kuwa na mvuto mkubwa kuliko msichana ambaye anaweza kuwa na hilo hilo lakini akajiachia na kujisikia watu wanampigia miluzi. Yule wa pili anaweza akawa ni wa kuchukuliwa kwa kustarehe lakini yule wa kwanza akaonekana anafaa kuwa mke (wife and motherly material).

Sasa najiuliza ni wakati gani dada zetu wawe na zile soni zao za kike na aibu fulani fulani? Ni kweli wanaume hatutaki tena wanawake wenye aibu aibu au tunawaombea watokee tena? Je ni kweli wanawake wanafikiri wanaume wanafurahia msichana ambaye ana macho makavu na hana aibu kabisa? Na hasa hili la siku hizi la baadhi ya dada zetu kwenda "commando" kwa kisingizio cha "joto" kweli siyo la kuonea soni kidogo!?


Au ndio karne ya ishirini na moja yenyewe?
 
Last edited by a moderator:
Ukiuliza utaambiwa: Tunaenda na wakati mzee. lol
Binafsi I think like you, it is not proper kwa mwanamke kua too comfortable kuongea matusi hadharani au kukaa mkao ambao hauonekani wa kidesturi pale alipo... but this is just me :A S embarassed:
 
MMM salute you mkuu. Mm kuna staffmate wangu wa kike aliwahi kutamka mbele yetu wafanyakazi wa kiume eti siku hiyo ana hamu anataka wa kumkuna. Kwakweli nowdays aibu hakuna kabisaa.
 
Mie nilikutana na binti mahali, sikuwa na uhakika kama ni yule niliedhani nilikuwa namfahamu au ni kufananisha tu. Yule binti akaniambia "kama umenipenda wee sema tu". Na wala sikuwa na hilo wazo!
 
asiyekuwa na staha wanaume wengi huamua kuyeya kimya kimya
595.gif
 
MMM salute you mkuu. Mm kuna staffmate wangu wa kike aliwahi kutamka mbele yetu wafanyakazi wa kiume eti siku hiyo ana hamu anataka wa kumkuna. Kwakweli nowdays aibu hakuna kabisaa.

Kweli kabisa anaweza kupata mtu wa kumkuna lakini anafikiria anaweza kuvutia mume material? Halafu wa namna hiyo wanaume wanampenda kweli!!
 
Binafsi nafikiri mwanamke anapaswa kuwa na soni na mwenye kuangalia anaongea vipi,wapi na akiwepo nani....ila kwa upande mwingine nafikiri wanaume wapo wanaoongea hovyo na mwanamke anapokuwa na soni wanamkejeli na kumuona kama vile anajidai mtakatifu..!

Ila pia kwa uzoefu wangu,baadhi ya marafiki zangu wenye tabia hizo wapo kwenye ndoa na siku zinaenda tu,sijui undani....nachoamini,kila mtu ana taste yake na vipaumbele vyake kwa mwanamke anayemtaka....na wapo wasiojali kile kinachotoka kinywani kwa wapenzi wao. sitamani wifi wa aina hiyo though.....:A S embarassed:
 
Mwanamke akivaa na kuacha mapaja au maziwa nje anapendeza sana kumtazama lakini hutatamani awe mkeo wala nduguyo hutopenda amwoe.
Mwanamke yake staha,
 
Cku hizi mambo yamebadilika sn,hata zile aibu za kutafuna kucha wakati wa kutongozwa hakuna tena,cku hizi kuna wenye ujacri wa kumtokea mwanaume!mie nafikiri hata malezi hasa ya huku mjin yamechangia sn,ila kale kaibu ka kike ni muhimu kuwa maintained!cku moja kwenye daladala mdada alipokea cm anaongea na buzi lake nilitaman kujificha bila haya anamsifia jamaa kwa gemu aliyompa mpaka na maumbile ya jamaa haki ya nani watu walibaki kuguna na kutizamana tu!
 
Cku hizi mambo yamebadilika sn,hata zile aibu za kutafuna kucha wakati wa kutongozwa hakuna tena,cku hizi kuna wenye ujacri wa kumtokea mwanaume!mie nafikiri hata malezi hasa ya huku mjin yamechangia sn,ila kale kaibu ka kike ni muhimu kuwa maintained!cku moja kwenye daladala mdada alipokea cm anaongea na buzi lake nilitaman kujificha bila haya anamsifia jamaa kwa gemu aliyompa mpaka na maumbile ya jamaa haki ya nani watu walibaki kuguna na kutizamana tu!
Hahahahaha, hii kali!
 
Hahahahaha, hii kali!

Mwenzangu,yan kila mwanamke mle ndan tulibaki macho yametutoka na hv vicm vyetu ya nokia tochi mtu akiongea unamsikia mpaka wa upande wa pili dah!ni aibu mwanzo mwisho bidada yeye wala ndio kwanza kanogewa anamwaga misifa tu!
 
Mwenzangu,yan kila mwanamke mle ndan tulibaki macho yametutoka na hv vicm vyetu ya nokia tochi mtu akiongea unamsikia mpaka wa upande wa pili dah!ni aibu mwanzo mwisho bidada yeye wala ndio kwanza kanogewa anamwaga misifa tu!
Stop it please, sina mbavu huku!
Yani unavo hadithia naona kama nilikuwepo na najiskia vibaya kuliko hata wewe. hahahahaha
Dada alikua ofisini hapo, kikazi zaidi. lol
 
Mwenzangu,yan kila mwanamke mle ndan tulibaki macho yametutoka na hv vicm vyetu ya nokia tochi mtu akiongea unamsikia mpaka wa upande wa pili dah!ni aibu mwanzo mwisho bidada yeye wala ndio kwanza kanogewa anamwaga misifa tu!

Duh! hakuna hata mtu aliyeamua kumsemea hovyo huyu binti!?
 
Duh! hakuna hata mtu aliyeamua kumsemea hovyo huyu binti!?
Mkuu, sometimes watu kama hao ni kuwapotezea tu. Ukijaribu kumwambia atakuporomoshea matushi makali, na usipo tulia hata mama yako atatukaniwa viungo vyake vya uzazi pia. Sasa hapo aibu ya nani?
 
Back
Top Bottom