Machinjio kufungwa mashine maalum

Machinjio kufungwa mashine maalum

Mnasema mashine za kuendeshwa kwa UMEME??
hahahahahaaa.......kuna siku mtakosa Nyama Dar nzima.

Ngoja tuone!
 
Logically...operator wa hiyo mashine ndiye mchinjaji.

Sijui atakuwa na sifa gani kwenye Job description yake.
na je machine itafungwa kuelekezwa Kibra?
Na operator akiwa Mkristo, je waislamu watakula na kinyume chake je?

Maana ugonjwa huu wa uchinjaji umeshakuwa sugu sasa, kuuponya ni kazi kwelikweli.
 
Mnasema mashine za kuendeshwa kwa UMEME??
hahahahahaaa.......kuna siku mtakosa Nyama Dar nzima.

Ngoja tuone!

Ina maana machine hii inafungwa Dar peke yake? wale wa mfaranyaki na Tunduma vipi?
Tunaiga mambo ya ulaya huku hata mambo ya Nishati hatujajitosheleza nchi nzima.
Tunataka kuchinja kwa umeme wa Mgao, kama si kutaka kutesa wanyama ni nini?
 
hivi inawezekana shehe akachinja ng'ombe mzima alafu asiondoke hata na kilo moja au walau pesa za ujira? kama wanafanya ibada, kwanini watake na ujira? na kama kuna ujira, basi hiyo ni kazi kama kazi zingine tu ambayo haitakiwi kuwa ya kibaguzi wafanye watu wa dini fulani tu. hivi shehe anayepata nyama ya bure karibia kila siku au anapata hela, inawezekana akakubaliana na kuchinja kwa machine ili akose kipato hapo kweli?..na je, VIPI SIKU ZILE WANAZOGOMA KUCHINJA, MFANO MWANZA NA SINGIDA MWAKA JANA, HATA HAPA DSM WALISHAWAHI KUGOMA KUCHINJA, watu tukakosa nyama, ni kama utumwa fulani hivi wanatutumikisha kutufanya wapendavyo....mi naona mashine zije. na pale wafanye watu application za kazi kabisaaa, wapigwe interview watu wa dini zote na waajiriwe na taasisi ya uchinjaji tz,..sio kuachia watu wa dini moja.
 
Suala la kuchinja mbona linakuzwa kiasi hiki? Hivi hawa ndugu zetu wakienda hotelini huwa wanauliza ni nani aliyechinja? Na wakitembelea nchi za kikristo ambazo waislamu hawana sauti huwa hawali nyama mpaka wanarudi nyumbani? Wakumbuke Tanzania siyo nchi ya kiislamu wala kikristo na kutaka kufuata sheria za dini yako 100% juwa utamkosea mwenzio wa imani nyingine.
 
...hizo mashine zitawekwa na dini gani?maana watu wanataka wachinje kwa imani zao.
 
hizo mashine zimetengenezwa nchi gani ya kikristo au ya kiislamu na je operator wake atakuwa wa dini gani
huu ni upuuzi kama zinaletwa kwa kutafuta ufumbuzi wa hii sintofahamu kwa ni vyema kila mtu akaishi kwa imanii yake
 
Mmekalia kuchinja, muda c mref itakuja hoja ijumaa watu wapumzke coz j'moc na pil n mapumzko je na hili nalo? Mtaanza ooh, mbona toka zaman ilkua hvyo, kwan na hil la kuchinja c toka zaman?! Mkae mkijua kna mambo meng ya mcng mmekalia upuuz!
 
wonderful..tukifuata vile mungu anatuagiza tu ndo tutaepuka chuki zote izi...tuepushe Rabi!
 
Back
Top Bottom