Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Jana wakati nimemaliza kuangalia mechi tamu kati ya Man untd na Everton,tulijikuta tumekaa nje nyumbani vijana kama wa-4 hivi,kiumri wote tuko kwenye 30's,kati yetu aliyekua ameoa ni mmoja na mkewe amesafiri.Ulizuka mjadala na nilikuta ninachotetea niko peke yangu.Mjadala wenyewe ulikua kati ya mke wa mtu,wanawake wenye umri mkubwa na mabinti walioko single ni yupi ukiwa na uhusiano nae unapata raha?Binafsi niliwaambia,mke wa mtu unaweza kuenjoy lakini unakua hatarini hivyo huwezi kufurahi 100% na siyo sahihi.Mabinti wana changamoto zao ambazo zimekua zikitushinda vijana wengi,lakin still hao ndo tutawaoa na hatutakiwi kuziogopa changamoto hizi za mabinti.Wanawake wenye umri mkubwa na walioko single(37-50)hawa ni kweli wanajua kujali,wakweli n.k,lakini vp ukitaka kuoa?Sidhani kama hawa nao ni sahihi kwetu vijana.Wenzangu katika kuchangia walionekana kuvutiwa zaidi na wake za watu na hao wamama.Kabla ya kulala nilijaribu kuchat kwa sms na jamaa zangu kama wa 5 hivi nao walisema yaleyale.Ndipo katika tafakuri nikagundua hatari iliyopo.Kwanza uaminifu kwenye ndoa za sasa unazidi kushuka na muda si mrefu utafikia 0.Pili,tatizo la vijana kuogopa changamoto na kutopenda kuwajibika ni janga kwa taifa,tusipowajibika na kusubiri kuliswa na wake za watu na wamama,tutakua taifa la hovyo sana.Pia wakina dada walioko single (ambao hawajaolewa)nao wameingia kwenye mbio za kiushindani na makundi haya ya wanawake,ambayo kimsingi wao (walio single) ndo hitaji la wanaume liko juu (kuolewa) Wewe unafikiri kifanyike?Je wadada wapunguze changamoto zao dhidi ya vijana wa kiume au ukali wa maisha nao unachangia vijana kukimbilia hao wanaoonekana kutokua na gharama?