Mabere Nyaucho Marando alikuwa mwajiriwa wa UWT tangu enzi za Mwl Nyerere.Mabere Marando alikuwa ni miongoni mwa watu wa mwanzo kudai mfumo wa vyama vingi kabla ya mfumo huo kuruhusiwa rasmi.
Marando alikuwa mwenyekiti wa mwanzo wa NCCR Mageuzi kabla hajampisha A L Mrema mwaka 1994.Marando alibakia na nafasi ya katibu mkuu wa NCCR Mageuzi na mbunge wa Rorya na baadae mbunge wa Afrika mashariki.Marando alishiki kwa kiasi kikubwa kuisambaratisha NCCR Mageuzi kwa kuhakikisha mkutano mkuu wa NCCR Mageuzi unashindwa kufanyika,alishikiri kuandaa vijana kuanzisha vurugu ndani ya mkutano hali iliyosababisha Mwenyekiti wake Mzee wa Kiraracha kujificha chini ya meza.Marando alizawadiwa ubunge wa EAC na CCM kama malipo ya kuisambaratisha NCCR Mageuzi.
Mabere Nyaucho Marando mwanasheria na kachero wa juu alishiriki vita vya kumwangusha idd Amin wa Uganda.Alitumia taaluma yake ya ukachero kuingia ndani ya nchi ya Uganda kabla majeshi yetu yaliyokuwa yakiongozwa na kamanda David Musuguri hayajatia mguu Kampala.
Taaluma ya ukachero si mbaya kama baadhi ya watu wanavyodhani inategemea inavyotumiwa na watawala.Tanzania ukachero enzi za Mwl Nyerere ulijikita zaidi kwenye mambo ya ulinzi na usalama wa nchi,wakati huo Tanzania ilitumia rasilimali zake nyingi kuzukomboa nchi zilizokuwa zinatawaliwa na wakoloni [Waingerezera,Wareno na nk].Bahati mbaya baada ya vita vya ukombozi kumalizika kwa mafanikio makubwa usalama wa taifa [UWT] wamejikita kulinda viongozi walioko madarakani kwa kutumia mbinu haramu.
Nchi zilizoendelea na zinazoinukia kiuchumi kitengo cha ukachero pamoja na mambo ya usalama kinatumiwa kuangalia maslahi ya kiuchumi zaidi.Dunia ya leo uchumi mzuri na wenye nguvu ni usalama tosha kwa taifa lolote makini.UWT haina habari ya uchumi wa nchi ndiyo maana baadhi ya maofisa wake walishiriki bila hofu yoyote kwenye ufisadi uliofanyika BOT.UWT haioni ubaya madini yetu ya Tanzanite yakiuzwa kama malighafi India.UWT haina hofu raia wa nchi za kigeni wakiajiriwa kwenye makampuni mabali mbali nafasi ambazo zingekuwa za raia wa Tanzania.UWT imeshindwa kuishauri serekali kwamba ingetakiwa kuwa mbia wa migodi yote ya madini ya dhahabu.UWT imeshikilia kazi moja kubwa ya kulinda serekali ya CCM isiondoshwe madarakani.