Mabasi ya mikoani na vikapu vya takataka

JT2014

JF-Expert Member
Jan 18, 2014
1,863
1,367
Niwapongeze wanajf wote kwa kuingia mwaka mpya 2018. Pia niwape pole/hongera na kazi za kulijenga taifa.

Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu iliyonisukuma kuanzisha uzi huu. Katika safari zangu za mapumziko ya sikukuu za Christmas na mwaka mpya,nilisafiri katika mojawapo ya mabasi ya kwenda mikoani(kanda ya ziwa)

Nilishangazwa sana na wahudumu wa mabasi hayo. kumwaga takataka wanazozikusanya kwenye mabasi kutoka kwa wateja wao wanaosafiri mfano,mabox ya biscuit chupa za soda/maji n.k. wakisimama porini kwa lengo la watu kuchimba dawa wanamwaga taka taka hizo kwenye mapori na hivyo kupoteza maana ya kuweka vikapu hivyo kwenye mabasi ambapo lengo lilikuwa kuzuia abiria kutupa taka ovyo njiani.

Rai yangu kwa mamalaka husika ni kuweka udhibiti wa tabia hii, ili kuhakikisha mabasi yana mifuko ya kutunzia taka taka kwenye buti za magari yao mpaka mwisho wa safari au mpaka sehemu sahii yenye kuhusika na takataka hizo ili kuepuka uharibifu wa mazingira kwa kiasi kikubwa.

Karibu kama una wazo mbadala au la ziada ili kuhakikisha hali ya mazingira inatunzwa.
 
Kwanza kabisa nataka niwachane wale wote wanaotumia vitu kama maji, soda, biscuits e.t.c na kisha kutupa mabaki dirishani..

Imagine mtu anatupa kopo la soda zile "cans" katikati ya barabara. Hujui unaweza kusababisha ajali na kuondoa roho za binadamu wenzio?

Tustaarabike wa Tanzania.. Tusiwe wapuuzi kiasi hicho, huwa nashindwa kuvumilia nikikutana na watu wa aina hii yano roho huwa haitulii mpaka niwachane live..

Hata kama kwenye basi/daladala hakuna trash bin we tupa humo chini ndani ya gari watasafisha wenyewe maana ni wajibu wao ku supply hizo facilities

Tuache uchafuzi wa mazingira na kuhatarisha maisha ya wengine bila sababu maalum
 
Kwanza kabisa nataka niwachane wale wote wanaotumia vitu kama maji, soda, biscuits e.t.c na kisha kutupa mabaki dirishani..

Imagine mtu anatupa kopo la soda zile "cans" katikati ya barabara. Hujui unaweza kusababisha ajali na kuondoa roho za binadamu wenzio?

Tustaarabike wa Tanzania.. Tusiwe wapuuzi kiasi hicho, huwa nashindwa kuvumilia nikikutana na watu wa aina hii yano roho huwa haitulii mpaka niwachane live..

Hata kama kwenye basi/daladala hakuna trash bin we tupa humo chini ndani ya gari watasafisha wenyewe maana ni wajibu wao ku supply hizo facilities

Tuache uchafuzi wa mazingira na kuhatarisha maisha ya wengine bila sababu maalum
kwani dar sio mkoa
 
Tupiamo na tupicha wengine hatujawahi safiri tuone namna wanavyoyachafua mazingira tunayotaka kujenga viwanda........
Duh! bahati mbaya simu yangu ya kitochi
na sikuwa na kamera.Ila amini nisemalo nimeliona.
ila tabia hii kama haitaisha basi nikienda mapumziko
ya pasaka nitapiga picha.Asante kwa ushauri.
 
Duh! bahati mbaya simu yangu ya kitochi
na sikuwa na kamera.Ila amini nisemalo nimeliona.
ila tabia hii kama haitaisha basi nikienda mapumziko
ya pasaka nitapiga picha.Asante kwa ushauri.

Duh!!!! mpaka pasaka hahaha hiyo njia itakua inapitika kweli??
 
Kwanza kuchimba dawa porini ni uchafuzi wa mazingira, serikali ilishakataa hili suala.
 
Mimi kama Gari haina dust bin basi ujue uchafu ntauacha humo humo ndani ya Gari, Ata iwe porini siwezi kutupa taka taka nje
 
Ni kwa baadhi ya mikoa nahisi au pia baadhi ya mabasi

Sisi huku lile dustbin linakuwamo mlemle na matakataka yake had mnafika nahisi hua wanatupa wakifika waendako sijawah kuona yakimwagwa njiani hata siku moja

Lakini pia sio ustaarabu hata kuchimba dawa porini hii sio sahihi kabisa
 
Hata mi hua nashangaa sana Na ninatumia sana njia hiyo ya kwenda mwanza from Dar,kuna siku kondakta alimwaga uchafu sehemu ambayo sio pori sana,wakati tunapanda kutoka kuchimba dawa ghafla nikawaona watoto wakaja kukagua hayo mauchafu huku wanacheka,sisi tunapanda bas tukaondoka.hua nashangaa maana sioni mantiki ya kuweka uchafu kwenye dustbin
 
hili,ni..tatizo..mkuu,ishu..ya..kutunza..mazingira,acha..tu..kwenye..mabasi..mtaani,nako..ni..shida..pia..hata,sisi..abiria
hatuthamini,mazingira..unakuta..mtu..anatupa..taka..kupitia,kioo..cha..gari..katika..mbuga..ya..wanyama.
lada,dawa..ni..kuweka..dustbin,kubwa..katika..gari..mwisho..wa..safari..awepo..askari..ambaye..ataona,taka..hizo..then..
ndipo,zikamwagwe..sehemu..sahihi..pia,kuwepo..na..by..laws..kudhibiti..hali..hiyo.
 
Sisi huku lile dustbin linakuwamo mlemle na matakataka yake had mnafika nahisi hua wanatupa wakifika waendako sijawah kuona yakimwagwa njiani hata siku moja
Nadhani hii inategemea umbali wa safari.kuna safari za mbali makapu hayo yanajaa
sasa unakuta makondo hawana mpango wa kuhifadhi takataka hizo
wanaamua kuzimwaga ovyo sehemu wanazoona siyo makazi ya watu
lakini tukumbuke takataka za plastic haziozi hata ikipita miaka mingapi.
 
Niwapongeze wanajf wote kwa kuingia mwaka mpya 2018. Pia niwape pole/hongera na kazi za kulijenga taifa.

Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu iliyonisukuma kuanzisha uzi huu. Katika safari zangu za mapumziko ya sikukuu za Christmas na mwaka mpya,nilisafiri katika mojawapo ya mabasi ya kwenda mikoani(kanda ya ziwa)

Nilishangazwa sana na wahudumu wa mabasi hayo. kumwaga takataka wanazozikusanya kwenye mabasi kutoka kwa wateja wao wanaosafiri mfano,mabox ya biscuit chupa za soda/maji n.k. wakisimama porini kwa lengo la watu kuchimba dawa wanamwaga taka taka hizo kwenye mapori na hivyo kupoteza maana ya kuweka vikapu hivyo kwenye mabasi ambapo lengo lilikuwa kuzuia abiria kutupa taka ovyo njiani.

Rai yangu kwa mamalaka husika ni kuweka udhibiti wa tabia hii, ili kuhakikisha mabasi yana mifuko ya kutunzia taka taka kwenye buti za magari yao mpaka mwisho wa safari au mpaka sehemu sahii yenye kuhusika na takataka hizo ili kuepuka uharibifu wa mazingira kwa kiasi kikubwa.

Karibu kama una wazo mbadala au la ziada ili kuhakikisha hali ya mazingira inatunzwa.


Kwanini wasifanye kama kwenye air transport, kila stand nchini iwe na kampuni ya usafi kwa magari yanayofika hapo na kuondoka, hii inaweza kurejesha nidhamu kwa maana kwamba bus ambalo halitafika na uchafu liwajibike kueleza uchafu umetupwa wapi kama si kwenye kituo husika
 
Kwanini wasifanye kama kwenye air transport, kila stand nchini iwe na kampuni ya usafi kwa magari yanayofika hapo na kuondoka, hii inaweza kurejesha nidhamu kwa maana kwamba bus ambalo halitafika na uchafu liwajibike kueleza uchafu umetupwa wapi kama si kwenye kituo husika
Safi sana,naona huu ni ushauri mzuri.Kuna sheria za halmashauri mabasi yote
ni lazima kuingia kwenye vituo hata kama hayana abiria wa kushuka/kupakia
sasa ni vema wakaongeza na hili la taka maana mabasi yanalipia ushuru
wa vituo hivyo.
 
Back
Top Bottom