Mabasi ya 'Luxury'

Mabasi ya 'Luxury'

Umuhirindahu

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2014
Posts
349
Reaction score
170
Wana JF naomba kuuliza,

Ili basi la abiria likidhi vigezo vya kuitwa "luxury" inatakiwa liweje? Nauliza kwa kuwa jana nilisafiri kwa basi kutoka Arusha kuja Dsm kwa basi linalojinadi ni luxury, ndani lina "seat-two by two", tatizo ni mvua ilipoanza kunyesha tulilowa njia nzima, gari halina mziki wala nini, TV zipo za kichovu na hazikuwashwa safari yote, nauli tuliyolipishwa ni ya Luxury, mdada ambaye ni konda/mhudumu majibu yake ni ya nyodo mwanzo hadi mwisho wa safari, jina la basi linaanzia D...........s!!!
 
Waulize Sumatra ndio wanaotoa vibali vya aina za magari...
 
binafsi nakerwa na tabia ya wahudumu wa mabasi kukagua tiketi mara mbili au zaidi. acheni ushamba bwana!
 
Wana JF naomba kuuliza, ili basi la abiria likidhi vigezo vya kuitwa "luxury" inatakiwa liweje?nauliza kwakuwa jana nilisafiri kwa basi kutoka Arusha kuja Dsm kwa basi linalojinadi ni luxury,ndani lina "seat-two by two" tatizo ni mvua ilipoanza kunyesha,tulilowa njia nzima,gari halina mziki wala nini,TV zipo za kichovu na hazikuwashwa safari yote,nauli tuliyolipishwa ni ya Luxur,mdada ambaye ni konda/mhudumu majibu yake ni ya nyodo mwanzo hadi mwisho wa safari,jina la basi linaanzia D...........s!!!!

Taja jina tulishughulikie.
 
Luxury Buses zilikufa na SCANDINAVIAN EXPRESS ,Now days hakuna tena Luxury Buses Bali tuna Two setter buses zilizo batizwa jina la luxury
 
Luxury Buses zilikufa na SCANDINAVIAN EXPRESS ,Now days hakuna tena Luxury Buses Bali tuna Two setter buses zilizo batizwa jina la luxury

nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%,,,wasafiri tunaibiwa sana ...basi kuwa na "seat za two by two" siyo kigezo tosha cha basi kuwa "luxury",,,wizi mtupu!!
 
This was a really luxury bus
 

Attachments

  • 1427136081657.jpg
    1427136081657.jpg
    3.4 KB · Views: 1,297
Usafiri wa Dar-Mbeya-Dar kuna Ndenjela Jet...kuanzia makonda wao wa kike na madereva utafikiri wamepitia kozi za huduma kwa wateja...Huwezi juta kutumia usafiri wao...kwao mteja ni mfalme, wanamheshimu, wanamjali na kumsikiliza...
 
Usafiri wa Dar-Mbeya-Dar kuna Ndenjela Jet...kuanzia makonda wao wa kike na madereva utafikiri wamepitia kozi za huduma kwa wateja...Huwezi juta kutumia usafiri wao...kwao mteja ni mfalme, wanamheshimu, wanamjali na kumsikiliza...

Hao jamaa miaka yote toka wameanza business makonda wao ni 'mademu' tu
 
Scandinavia it was a luxurious thing from unapo nunua tiketi..aina ya tickets. Passengers lounge..kila kitu ulikuwa classic.... Bus zako zilikuwa ni luxury za sina 3 Marcopolo Andare ulikuwa ya chini na Parradisso was the most luxurious with Frige.coffee maker..toilet..full AC na kwa like la Dar-Nairobi.ilikuwa ukifika Kibaha wapatiwa breakfast ndani ya bus,ukifika Chalinze pili,biscuits na soda.tena zikiwa na nembo ya Scandinavia.. Baada ya kula korogwe. .wapewa pili Maji soda na napkins za Scandinavia... Hata km mko watano kwa bus halipakii njiani na mtaawachiwa AC to Nrb..Those were luxurious buses si sasa!!!!!!
 
Scandinavia it was a luxurious thing from unapo nunua tiketi..aina ya tickets. Passengers lounge..kila kitu ulikuwa classic.... Bus zako zilikuwa ni luxury za sina 3 Marcopolo Andare ulikuwa ya chini na Parradisso was the most luxurious with Frige.coffee maker..toilet..full AC na kwa like la Dar-Nairobi.ilikuwa ukifika Kibaha wapatiwa breakfast ndani ya bus,ukifika Chalinze pili,biscuits na soda.tena zikiwa na nembo ya Scandinavia.. Baada ya kula korogwe. .wapewa pili Maji soda na napkins za Scandinavia... Hata km mko watano kwa bus halipakii njiani na mtaawachiwa AC to Nrb..Those were luxurious buses si sasa!!!!!!

asante kwa kuufahamu ukweli
 
Luxury Buses nyingi ambazo nimezoea zipo Nrbi-Mombasa,Kenya.

1/Leg-space ama allowance iwe ya kutosha.

2/Viti viwe adjustable. Sijui nielezeje ili nieleweke……Alafu kuna baadhi ya buses ina VIP seats ambazo ni pana sana.

3/Ziweze kuserve vitafunwa,maji,juice,biscuits.

4/Hamna kusimamasimama barabarani. Kama mchangiaji mmoja alivyosema,hata kama wamebook watu watano au kumi,hamna kuchukua abiria barabarani.

5/Entertainment ni kama kawa. Either music au movies.

6/Charging sockets kwa ajili ya kucharge simu ama laptops.

7/A/c kwa safari za maeneo yenye joto. Obviously you don't need an a/c in Kilimanjaro.

8/Kuna baadhi ya buses to be specific inaitwa Spanish Coaches,ina Tablets na wi-fi kwenye buses kwenye kila seat.



Ni hayo tu kwa sasa.
 
Back
Top Bottom