Nilikuwa sijakwambia mtoa mada enhee, hizo Dar express uwe unapanda kipindi cha kiangazi tu, ila kipindi cha mvua kama sasa utakiona cha mtema kuni. Yaani kwa kweli hayafai. Gari linavuja kama pakacha bwana kwa kweli Dar Express mnatia aibu kabisa.
Ukija upande wa hao madada kuwa na nyodo ndio kawaida yao yaani kama kuna mmoja yuko pale arusha ndio mkata ticket mweupe hivi, yule dada anakiburi mpaka anatia kiny'aa.
Jirekebisheni bwana, sikatai mmejipa sifa kubwa sana kwa safari za Dar-Arusha, Dar-Karatu, Dar-Nairobi, lakini onyesheni thamani yenu kwa kujali abiria zenu na sio kuwafanyia nyodo. Kuna magari maziri tu ya kwenda kaskazini ambayo yako vizuri kwa sasa.