Nimeyaona hayo mabango, mimi naifahamu gharama ya kutengeneza kila bango, yaani production cost, kutokana na size ya bango, halafu pia nafahamu rental fees za kubandika kila bango according to size and location, hivyo kupitia sheria ya gharama za Uchaguzi, the public has the right to know, CCM sio tuu kwa nini imetumia gharama kubwa kuliko zilizoainishwa kisheria, bali pia vyama vinawajibika kuwataja wafadhili wao na kiasi walichofadhili, lazima itaje source ya hizo fedha, na kama imepewa offer kutoka kampuni ya A1, then ipigwe hesabu yote ya hiyo offer, then tufuatilie TRA kama hao AI wamelipa kodi stahiki kwa offer zake kwa CCM, ili isije kuwa this time CCM imeishatafuta kichaka kingine kama cha Kagoda kilichomuingiza Mukulu Ikulu, na ufadhili kwa CCM kisije kuwa ni kichaka cha ukwepaji kodi, vinginevyo kama wafanya biashara wako huru kuchangia chama chochote cha siasa, alimradi kwanza michango hiyo ionekane wazi kwenye mahesabu, pili vyama vitaonyesha source za pesa hizo, na mwisho pesa zote zitalipiwa kodi stahiki!.
Pasco