Mabaki ya aliens yafanyiwa tafiti Mexico, Marekani watoa ripoti ya kwanza ya UFO's

Eugen TZA

Member
Aug 7, 2023
61
98
#KashindeUpdates Stori za viumbe wa angani (Aliens ) na UFO's zimerejea tena kwa kasi katika vyombo mbalimbali vya habari Duniani wiki sio kwamba (Mothership) au chombo chao kimetua White House ikulu ya Marekani hapana bali ni kwasababu NASA wiki hii wametoa ripoti yao kuhusu UFO's wakielezea kuhusu tafiti zao katika anga za mbali, chini ya maji Duniani na hata angani n.k

Ripoti hiyo ya kwanza kabisa kutolewa na NASA Wakishirikiana na watafiti huru wa umma na wachunguzi wa vitu visivyo vya kawaida (Unidentified Anomalous Phenomena) (UAP) imehashiria hatua za awali watu Duniani kuelezwa ukweli wote, Sasa baada ya tukio hilo kuzua Gumzo, Mexico wamefuata wakitangaza uchunguzi wao wa kile walichokiita uchunguzi wa mabaki ya Aliens Duniani.

Picha za uchunguzi huo zimetolewa na mwandishi wa maswala ya Anga nchini humo Jaime Maussan ambaye katika ripoti yake ameelezea kuwa mabaki ya viumbe hao wawili wa angani (Ambayo watu wengi wamedai ni feki) yaligunduliwa huko Peru karibu na Columbian Nazca Lines mwaka 2017 kwa mujibu wa Reuters wameripoti, Ambapo baada ya uchunguzi wamegundua mabaki hayo yana umri wa miaka 1,000 na ni ya kipekee tofauti na viumbe wa sayari yetu ya Dunia.

Mabaki hayo ya miili au mifupa ya Aliens wa mchongo wa Mexico mmojawapo ni mwili wa kike ambapo madaktari wanesema wamegundua mayai ndani yake, Wana macho mawili, mdomo, mikono miwili na miguu miwili, Katika kufananisha mabaki hayo na viumbe wa Dunia hii takribani milioni madaktari wanesema kuwa hawajapata kuelewa vyema miili hiyo kutokana na kuwa na utofauti mkubwa mbali sana na uelewa wa binadamu.

Hata hivyo baada ya kuenea kwa taarifa hii Mwandishi wa habari wa BBC, Sam Cabral amewauliza NASA kama wamewasilia na Mexico kufuatilia uchunguzi huo, David Spergel kiti wa NASA's UAP Study Team amemjibu akisema kuwa kama yamepatikana mabaki ya Aliens walipaswa kuweka wazi kuruhusu watu wengine kutafiti kama wanavyofanya NASA kualika watafiti kuchangia kuchunguza kabla ya kuweka wazi kwa umma.

Stori za viumbe wa angani (Aliens) UFO's zimekua zikiripotiwa katika maeneo mbalimbali Duniani kwa muda sasa, Nchi za Urusi, Uchina, na America wamekua wakichunguza kile kinachoitwa vyombo vya ajabu vinavyonaswa na camera angani, kwenye Space, mwezini au chini ya maji baharini Duniani bila kupata majibu, Kwa sasa watafiti wengi wameendelea kuwekeza muda wao kuchunguza kuhusu vyombo hivyo na huenda mbeleni tukapata majibu.

#PeaceOverInterest
 
Hata ulivyoandika tu iko juu kiwango cha nje wa uelewa wangu.

Nimeelewa tu kuwa walivichunguza viumbe vilivyo juu, kimaumbile ni sawa na binadamu ila vina uelewa mkubwa zaidi.

Tuseme Mungu alienda akaumba tena binadamu mwingine baada ya kuona ile kashikashi la wana wa Yakobo ?

Tuseme hayo ndiyo yale majitu yaliyokuwepo kabla ya historia ya uumbaji ?

Tuseme kuna maisha pia yanaendelea huko sayari nyingine, ndiyo maana kuna na vyombo vingine according to you?
 
watahangaika sana+uongo mwingi.
kumbuka haowanaochunguza wametuambia binadamu wakwanza ametokana nanyani Hadi leo hawajaungama uongo huu.
Sio kwamba wametokana na nyani kwa unavofikiri wewe..., ni kwamba tuna ancestry moja, ila kupitia mabadiliko ya evolution (adapation na natural selection) binadamu tuka branch out na kubadilika kulingana na mazingira yetu hadi kuwa hivi tulivyo leo
 
Sio kwamba wametokana na nyani kwa unavofikiri wewe..., ni kwamba tuna ancestry moja, ila kupitia mabadiliko ya evolution (adapation na natural selection) binadamu tuka branch out na kubadilika kulingana na mazingira yetu hadi kuwa hivi tulivyo leo
nawewe ukaamini hivyo?
kabla yakuwa hivi binadamu alikuwaje mwanzo?
 
nawewe ukaamini hivyo?
kabla yakuwa hivi binadamu alikuwaje mwanzo?
Nakupa mfano hai wa jinsi evolution inavyo shape viumbe kwa kutumia ‘Artificial selection ya binadamu’.

Kuna WaJapan waikuwa wanaamini kwamba kuna kaa wana kama mfano hivi na MaSamurai wa kale waliojitoa Muhanga, basi wavuvi kila wakivua kaa mwenye dalili za huo mfanano wakawa wanamrudisha kwenye maji, wale wasiofanana na masamurai wakawa wanawekwa mtumbwini na kwenda kuliwa.

Mwisho wa siku wale wenye mfanano na masamurai wakawa wanaendelea kuazaliana na wao kwa wao na hivyo zile sura za masamurai kwenye magamba yao zikwa zinazidixkuwa reinforced, maana ni mbegu zile zile zinazaliana, mwishowe baada ya mamia ya miaka wakabadilika kabisa na kuwa na hizo sura kwenye magamba yao.

Ona video...


View: https://youtu.be/dIeYPHCJ1B8?si=ny-fJTXJZOF2XUdu



View: https://youtu.be/I9ABRsOK6IY?si=e8ppnh7q71C9GO2U
 
Nakupa mfano hai wa jinsi evolution inavyo shape viumbe kwa kutumia ‘Artificial selection ya binadamu’.

Kuna WaJapan waikuwa wanaamini kwamba kuna kaa wana kama mfano hivi na MaSamurai wa kale waliojitoa Muhanga, basi wavuvi kila wakivua kaa mwenye dalili za huo mfanano wakawa wanamrudisha kwenye maji, wale wasiofanana na masamurai wakawa wanawekwa mtumbwini na kwenda kuliwa.

Mwisho wa siku wale wenye mfanano na masamurai wakawa wanaendelea kuazaliana na wao kwa wao na hivyo zile sura za masamurai kwenye magamba yao zikwa zinazidixkuwa reinforced, maana ni mbegu zile zile zinazaliana, mwishowe baada ya mamia ya miaka wakabadilika kabisa na kuwa na hizo sura kwenye magamba yao.

Ona video...


View: https://youtu.be/dIeYPHCJ1B8?si=ny-fJTXJZOF2XUdu



View: https://youtu.be/I9ABRsOK6IY?si=e8ppnh7q71C9GO2U

Wao walikua wanaamini tuu lakini haikuwa hivyo.


wewe unaambiwa binadamu alikuwa nyani sijui sokwe.mbona Sasa hivi hawabadiriki nakuwa binadamu?

nahao wazungu pia wanaamini nawao walitokana na nyani/sokwe? acheni ujinga/kudanganywa.
 
Wao walikua wanaamini tuu lakini haikuwa hivyo.


wewe unaambiwa binadamu alikuwa nyani sijui sokwe.mbona Sasa hivi hawabadiriki nakuwa binadamu?

nahao wazungu pia wanaamini nawao walitokana na nyani/sokwe? acheni ujinga/kudanganywa.
Nani kakwambia binadamu wa sasa hatubadiliki kulingana na mazingira?

Kuna mabadiliko ya aina mbili

1.) (Genotypic changes) ambapo ni mabadiliko yanayotokea ndani ya vinasaba vya binadamu, na chanzo chake kikuu ni mutations zitokanazo na sababu mbali mbali ikiwemo mionzi ya jua ya UV, au ulaji wa vyakula vyenye sumu na kemikali za aina mbali mbali za madawa zinazopelekea hitilafu katika uundwaji wa mtoto tumboni. Katika hili kwa mfano mama anaweza kutumia madawa makali wakati wa ujauzito, na hivyo kupelkea taarifa kuwa corrupted katika uundaji wa Zygote, mfano mtoto anaweza kuzaliwa na vidole 3 badala ya vi5.

Sasa mtoto huyu endapo kimuonekano ataonekana ana mvuto zaidi kwa mfano, akiwa mkubwa atapemdwa zaidi na jinsia ya tofauti na kuwa na chance ya kuzaa watoto wengine na kurithisha mbegu yake ya vidole vitatu, na hao watoto wake nao watawavutia zaidi kimapenzi watu wa jinsia tofauti na yao, hivyo wajukuu wengi zaidi watazaliwa na vidole vitatu, mwisho wa siku ndio ikankuwa trend, kila mtu atataka mpenzi mwenye vidole vitatu, baad aya miaka milioni 1 kupita ukaja kukuta nchi nzima wana vidole vitatu utashangaa?!!!

Halafu mtu unamwambia unajua zamani tulikuwa na vidole vitano, ila tukabadilika tukawa na vidole vitatu. Sasa hilo jitu lililoenda shule kusoma ila halikufanikiwa kuelimika litaanza kubisha, oooh, mbona sasa hivi vidole havibadiliki, jinga kabisa!!

Hata wanawake wenye makalio na mashape makubwa, wamekuja kuwa hivyo sababu ya artificial (/natural selection) ya binadamu. Binadamu tunajiumba wenyewe kwa matamanio yetu na mazingira yetu. Ndio maana tumachosema binadamu anaumba hata na viumbe wengine (mfano Samurai Crabs) kwa sababu tuna ‘Consiousness’, hii ndio inaumba, binadamu ana Mungu ndani yake na ndio anatumika kuumba pia, Mungu ni Consiousness yako, hii ndio inaumba.

Wewe umesoma, ila hujaelimika. Na usinijibu kitu, nyamaza, soma halafu kaa kimya!

2. ) Phynotypic changes, mabadiliko ya nje yasiyo ya kivinasaba...

Mabadiliko haya yanaweza kuja kwa sababu ya mazingira na mfumo tu wa maisha, mfano watoto wa kizazi cha blue band ni tofauti na wa enzi za Nyerere.., watoto wa sasa ni magiant, ila mabadiliko haya sio ya kudumu na hayarithishwi...
 
Wao walikua wanaamini tuu lakini haikuwa hivyo.


wewe unaambiwa binadamu alikuwa nyani sijui sokwe.mbona Sasa hivi hawabadiriki nakuwa binadamu?

nahao wazungu pia wanaamini nawao walitokana na nyani/sokwe? acheni ujinga/kudanganywa.
kumbe hujaelewa wana maana gani wakisema hivyo,.sayansi ina amini binadamu wa kwanza aliishi EAST AFRICA kutokana na mabaki ya kale.,
 
Nani kakwambia binadamu wa sasa hatubadiliki kulingana na mazingira?

Kuna mabadiliko ya aina mbili

1.) (Genotypic changes) ambapo ni mabadiliko yanayotokea ndani ya vinasaba vya binadamu, na chanzo chake kikuu ni mutations zitokanazo na sababu mbali mbali ikiwemo mionzi ya jua ya UV, au ulaji wa vyakula vyenye sumu na kemikali za aina mbali mbali za madawa zinazopelekea hitilafu katika uundwaji wa mtoto tumboni. Katika hili kwa mfano mama anaweza kutumia madawa makali wakati wa ujauzito, na hivyo kupelkea taarifa kuwa corrupted katika uundaji wa Zygote, mfano mtoto anaweza kuzaliwa na vidole 6 badala ya vi5.

Sasa mtoto huyu endapo kimuonekano ataonekana ana mvuto zaidi kwa mfano, akiwa mkubwa atapemdwa zaidi na jinsia ya tofauti na kuwa na chance ya kuzaa watoto wengine na kurithisha mbegu yake ya vidole vitatu, na hao watoto wake nao watawavutia zaidi kimapenzi watu wa jinsia tofauti na yao, hivyo wajukuu wengi zaidi watazaliwa na vidole vitatu, mwisho wa siku ndio ikankuwa trend, kila mtu atataka mpenzi mwenye vidole vitatu, baad aya miaka milioni 1 kupita ukaja kukuta nchi nzima wana vidole vitatu utashangaa?!!!

Halafu mtu unamwambia unajua zamani tulikuwa na vidole vitano, ila tukabadilika tukawa na vidole vitatu. Sasa hilo jitu lililoenda shule kusoma ila halikufanikiwa kuelimika litaanza kubisha, oooh, mbona sasa hivi vidole havibadiliki, jinga kabisa!!

Hata wanawake wenye makalio na mashaoe, wamekuja kuwa hivyo sababu ya artificial (/natural selection) ya binadamu. Binadamu tunajiumba wenyewe kwa matamanio yetu na mazingira yetu.

Wewe umesoma, ila hujaelimika. Na usinijibu kitu, nyamaza, soma halafu kaa kimya!

2. ) Phynotypic changes, mabadiliko ya nje yasiyo ya kivinasaba...

Mabadiliko haya yanaweza kuja kwa sababu ya mazingira na mfumo tu wa maisha, mfano watoto wa kizazi cha blue band ni tofauti na wa enzi za Nyerere.., watoto wa sasa ni magiant, ila mabadiliko haya sio ya kudumu na hayarithishwi...
bwege wewe.wazungu wamekuharibu.

wazungu Nao walikuambia wametokana nanyani?au nimtu mweusi tuu?

umesoma lakini hujaelimika mtukuzaliwa navidole vitatu huyó nimlemavu hajatimia.sasa binadamu wote watazaliwaje walemavu? unaakili kweli wewe ukiacha zile zakukalili darasani?
 
bwege wewe.wazungu wamekuharibu.

wazungu Nao walikuambia wametokana nanyani?au nimtu mweusi tuu?

umesoma lakini hujaelimika mtukuzaliwa navidole vitatu huyó nimlemavu hajatimia.sasa binadamu wote watazaliwaje walemavu? unaakili kweli wewe ukiacha zile zakukalili darasani?
Hoja hujibiwa kwa hoja. Toa hoja kuonyesha ubwege wangu.

Halafu ndio maana nikasema ‘endapo ‘ vidole vitatu vitaonelana ni’desirable! , nimetoa mfano tu kuonyesha jinsi mabadiliko hutokea. Ningeweza kutoa mfano wa makalio makubwa kwa muktadha huo huo.., kwamba makalio makubwa yanayoning’inia yalikuwa ni ulemavu , ila ukemavu wenye kuvutia, wanaume walipenda kuyabonyeza na walienjoy ya piga piga na yanavyotikisika kiasi cha kuamsha hisia za ngono, mwishowe hiyo mbegu imesambaa sana hasa Afrika.
 
Uwepo wa aliens ni jambo la kufikirika hao viumbe hawapo
kuna mandezi yanaokotwa nawazungu humu sio kitoto.hawajui wenzako wanataka kuweka tuu historia kama za babu zao waliosema waafrika tumetokana nanyani ikiwa hawajatuambia wazungu wametokana nanini🤣
 
Back
Top Bottom