Dennis Robert Shughuru
JF-Expert Member
- May 30, 2024
- 4,155
- 6,169
Ni ukweli kwamba kuna-sintofahama kubwa sana inayoendelea nchini kwa sahivi,
NIKIWA RAIS WA TANZANIA mambo ambayo ntayafanya na yataiponya nchi na ni kama yafuatayo;-
www.jamiiforums.com
- Wananchi walio wengi hawana imani na mahakama
- Wananchi walio wengi hawaamini mchakato wa uchaguzi
- Wananchi walio wengi hawaamini kwenye bunge
- Viongozi walio wengi sio wote hawawatumikii wananchi inavyotakiwa
NIKIWA RAIS WA TANZANIA mambo ambayo ntayafanya na yataiponya nchi na ni kama yafuatayo;-
- Msajili wa vyama vya siasa kutokuchaguliwa na Rais bali na vyama vya siasa vitakaa na kuamua namna ya kumchagua msajili wa vyama vya siasa kazi ya Rais ni kumuapisha
- Mkurugenzi wa tume ya uchaguzi na wajumbe kutokuchaguliwa na Rais, bali na vyama vya siasa wataangalia namna ya kumteua mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na wajumbe wake, wakishachaguliwa kazi ya Rais ni kuwaapisha
- DPP kuchaguliwa na wananchi na hatikwi kuwa na historia ya kuwa affiliate na chama chochote na akimaliza mda wake hatakua eligible kugombea Urais wa Tanzania
- Jaji mkuu kuchaguliwa na wananchi hatakiwi kuwa affliated na chama chochote-Majaji wa mahakama kuu kutochaguliwa na Rais bali na mchakato wa ndani wa mahakama kazi ya Rais ni kuwaapisha na akimaliza mda wake hatakua eligible kugombea Urais wa Tanzania
- Deni la taifa kukaguliwa na dpp ili kujua namna lilivyotumika
- Mkuu wa takukuru kuchaguliwa na wananchi na hatakiwi kuwa affiliate na chama chochote, na akimaliza mda wake hatakua eligible kugombea Urais wa Tanzania
- Mkaguzi wa miradi ya serikali huyu atakua anachagulia na wananchi na atakua ni engeineer na atakagua miradi yote iliyofanywa na kutathmini kama inaendana na thamani ya fedha iliyotengwa na inaubora uliokusudiwa na hatakuwa eligible kugombea Urais akimaliza mda wake
- Mbunge ni lazima aishi kwenye jimbo lake sio haki hata kidogo na ni ukatili mkubwa sana mbunge tunakuchagua alafu unaenda kuishi dar jimboni unakuja kama mtalii
- Mawaziri kutokuwa wabunge sababu mawaziri wengi wanapwaya kwenye majimbo yao
- Wakuu wa mikoa kuchaguliwa na wananchi
- Mchakato ndani ya vyama waamuzi wa mwisho ni wanachama wagombea hata wawe 100 wote watapigiwa kura na wanachama wa chama husika kwenye uchaguzi wa ndani wa kwanza ndo atepewa ridhaa
- Mchakato wa kumpata Rais wa ndani utafanyika kwa kupigiwa kura za wanachama wa chama husika kwenye kila mkoa na sio kuteuliwa na kikundi cha watu wachache
- Kutakuwa na chaguzi mbili;- ya Urais, wabunge na madiwani na utafanyika kwenye miaka inayogawanyika na 5, baada ya miaka 2 kupita uchaguzi mkuu kutafanyika uchaguzi wa wakuu wa mikoa, DPP, JAJI MKUU, MKUU WA TAKUKURU, MKAGUZI WA UBORA WA MIRADI YA SERIKALI, na wenyeviti wa mtaa
- Vyombo vya habari kuwa huru hata kuikosoa serikali
- Vyuo vikuu kurusiwa kufanya midahalo na kuikosoa serikali pale wanapoona imekosea
Support hustle zangu mimi Rais mtarajiwa wa Tanzania
Maandalizi na mchakato wa kuwa Rais wa Tanzania yanaendelea at the same time harakati za kutafuta rizki zinaendelea in-short maisha lazima yaendelee JAMANI NAOMBA MNIUNGISHE Historia nzuri ni ile inayoandikwa in an ugly way, and awkward way 👇👇👇👇👇👇👇👇 Kwenye historia ya Tanzania ntakumbukwa kuwa...