The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 4,780
- 8,155
.
Hebu angalieni hii picha, lakini msiishie kuiangalia, itazameni na mnapoitazama, itazameni kwa makini.
Kisha tafakari ujumbe ufuatao👇👇👇
Hivi unajua kwamba kila mmoja wetu hapa duniani amefanikiwa?
Yaani hakuna mtu duni, maskini, fukara, boya, lofa wala kenge.
Uduni, umaskini na ufukara tulio nao, huu uboya na ulofa mpaka tunaonekana kenge machoni pa watu, ni matokeo ya KUKOSA MAARIFA!
Maarifa ni nini?
Ni elimu sahihi, iliyodhibitika kuwa ni sahihi.
Hii elimu ikiingizwa kwenye matendo inakuwa maarifa na haya maarifa yakiendelezwa yanatupatia ufahamu na ufahamu ukiendelezwa unageuka uzoefu.
Mtu mwenye uzoefu katika kazi, taaluma, fani au jambo lolote, uwa anatumia nguvu kidogo sana kufanikiwa.
Mtu asiye na maarifa, hana ufahamu na bila ufahamu hakuna uzoefu na bila uzoefu basi katika kila jambo utatumia nguvu kubwa sana bila mafanikio au kwa mafanikio kidogo sana.
Ndio maana msingi wa mafanikio yoyote ni maarifa.
Jipatie maarifa ufanikiwe.
Pasipo maarifa hakuna mafanikio.
Darasa hili ni mahususi kwa ajili ya kupeana maarifa ya kiroho ambayo yakiendelezwa kwa kuyafanyia kazi yatainua kizazi cha watu waliofanikiwa kwenye nyanja mbalimbali za maisha.
"Knowledge is power" 👊🏻💪🏻👍👍👍
Kisha tafakari ujumbe ufuatao👇👇👇
Hivi unajua kwamba kila mmoja wetu hapa duniani amefanikiwa?
Yaani hakuna mtu duni, maskini, fukara, boya, lofa wala kenge.
Uduni, umaskini na ufukara tulio nao, huu uboya na ulofa mpaka tunaonekana kenge machoni pa watu, ni matokeo ya KUKOSA MAARIFA!
Maarifa ni nini?
Ni elimu sahihi, iliyodhibitika kuwa ni sahihi.
Hii elimu ikiingizwa kwenye matendo inakuwa maarifa na haya maarifa yakiendelezwa yanatupatia ufahamu na ufahamu ukiendelezwa unageuka uzoefu.
Mtu mwenye uzoefu katika kazi, taaluma, fani au jambo lolote, uwa anatumia nguvu kidogo sana kufanikiwa.
Mtu asiye na maarifa, hana ufahamu na bila ufahamu hakuna uzoefu na bila uzoefu basi katika kila jambo utatumia nguvu kubwa sana bila mafanikio au kwa mafanikio kidogo sana.
Ndio maana msingi wa mafanikio yoyote ni maarifa.
Jipatie maarifa ufanikiwe.
Pasipo maarifa hakuna mafanikio.
Darasa hili ni mahususi kwa ajili ya kupeana maarifa ya kiroho ambayo yakiendelezwa kwa kuyafanyia kazi yatainua kizazi cha watu waliofanikiwa kwenye nyanja mbalimbali za maisha.
"Knowledge is power" 👊🏻💪🏻👍👍👍