Maandamano ya kudai Ndege ni fedheha kwa Nchi

kluger

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
2,093
1,894
Salaam,

Nimefuatilia tu maandamo yaliyofanyika jijini Dar es salaam, nje ya ubalozi wa Africa kusini kushinikiza au kudai ndege ya Tanzania iliyokamatwa huko nchi Africa kusini ni aibu kubwa kwa Taifa.

Safari hii jeshi la polisi limeonyesha udhaifu wa kintelijensia kwa kushindwa kubaina mpango huu wa maandamano mpka yakafanikiwa, lakini kwa upande mwingine tunawapongeza kwa kutumia fimbo tu kutawanya waandamanaji na si mabomu kama ilivyoada.

Jambo hili lipo kisheria huko mahakamani Africa ya kusini na lilianzia hapa hapa Kwnye mahakama zetu, iweje leo kutumia nguvu ya umma/maandamano kushinikiza maamuzi ya jambo hili?
Je maandamano haya ni kundi gani la jamii?
Polisi tusaidieni kujua waratibu wa maandamano haya ni kina nani hasa?

Ni aibu sana kuona jambo hili limetoka mbali toka serikali ya awamu ya kwanza mpka leo hakuna ufumbuzi uliowahifikiwa.
Hii inaonyesha ni jinsi gani waafrica tulivyo kitabia na namna ambavyo tunapuuza mamlaka tulizoanzisha sisi wenyewe.

Ubabe na kulewa madaraka vinafanya watu na baadhi ya viongozi wetu kukosa utu na kutii sheria, ni kama wapo juu ya sheria za nchi.
Hapa wanatakiwa kufahamu hilo ni ndani tu ya mipaka yetu ya nchi. Huko nje watu wanatii sheria na kupambana kisheria.

Jambo hili limeumbua sana nchi na kuonyesha dunia ni namna gani tunashughulika na mambo ya kisheria.
Kuna baadhi ya watu kwa uelewa mdogo au kwa maksudi wanaunga mkono serikali mapungufu haya yaliyosababisha ndege kukamatwa.
Tuache ushabiki, tuelewe mambo na tuishi katika misingi ya kuheshimiana na kusikiliza wengine, TUACHE UBABE, USHABIKI, UNAFIKI NA TUMUOGOPE MUNGU katika maamuzi na uongozi.

Hili liwe funzo, kwa wote waliokosea katika utendaji.


NB: Kibaya zaidi waliondamana sioni abiria kabisa wa kupanda ndege nauli laki 3.5 kwenda Mwanza tu
 
Kuwepo kwa maandamano nk, kwangu siyo tija kabisa ila dhana ya watu wengi kuitupia lawama serikali iliyopo madarakani kama ndiyo iliyosababisha kukamatwa jet yetu, Siyo sahihi kabisa.

But kubwa nafaham siyo leo au jana, watanzania huwa hatuna uzalendo kwa baadhi ya mambo ya nchi yetu ila ni full lawama kwa kiongozi fulani.
 
Sasa ndugu yangu, serikali ya awamu hii ikiwa na nakala za hukumu ya kesi hii na historia nzima ya mwenendo wa kesi, na mbali ya kuona awamu ya nne ilijitahidi kulipa deni. Awamu hii wakaamua kumfukuza nchini Mdai na kugoma kuendelea kufanya malipo, mpka wameshtakiwa Kwnye mahakama za nje/ south Africa bado tu huoni serikali hii ina lawama ya kujibu?
Kuwepo kwa maandamano nk, kwangu siyo tija kabisa ila dhana ya watu wengi kuitupia lawama serikali iliyopo madarakani kama ndiyo iliyosababisha kukamatwa jet yetu, Siyo sahihi kabisa.

But kubwa nafaham siyo leo au jana, watanzania huwa hatuna uzalendo kwa baadhi ya mambo ya nchi yetu ila ni full lawama kwa kiongozi fulani.
 
Kosa kubwa la kwanza na la wazi kabisa kwa aliyeandaa haya maandamano ni kwamba alitaka kufananisha na maandamano ya kupinga ubaguzi na uonevu wa mabeberu yaliyokua yakifanyika huko nyuma hasa kwenye serikali ya awamu ya kwanza

Pengine hakujua kama hali ya kisiasa na hata kiuchumi duniani imebadilika sana. Kama alikua anajua hivyo na bado akayaandaa basi alikua anataka ku divert jambo lilikua limebamba attention za wabongo(kesi ya Lisu?)

Kama alikua hajui ajaribu kutafuta clips au aingie YouTube za vikao vya bunge la SA aone rais anavyosulubiwa au hata kukosewa adabu na wabunge ndipo ataelewa kama Ramaphosa anaweza kutoa tu amri ndege iachiwe au vipi

Kwa kifupi kule wenzetu vyombo vyao vya kikatiba sio tu kwamba vina nguvu bali vipo huru kabisa na hata polisi au mamlaka za kupambana na ufisadi zinaweza kumchunguza hata Rais na Bunge kuchukua hatua

Zuma aliwahi kutiwa msukosuko baada ya kufanya hila na kumtorosha kutumia uwanja wa ndege wa Jeshi Rais Al Bashir wakati mahakama ya South Africa ilishatamka akabidhiwe kwa ICC iliyokua na warranty ya kimataifa ya kumkamata ili apelekwe The Hague kujibu mashtaka ya uhalifu wa kivita
 
ccn si ndio wenye nchi hii jamani, wao ndio wamepanga na kuandamana, wameona haitoshi kumtimua madai na kusitisha malipo yake, wameongeza na aibu hii tena...hawa watu watamfanya rais aaibike sana, maana haya mambo ya kipuuzi nae hayakemei kabisa.
 
Sasa ndugu yangu, serikali ya awamu hii ikiwa na nakala za hukumu ya kesi hii na historia nzima ya mwenendo wa kesi, na mbali ya kuona awamu ya nne ilijitahidi kulipa deni. Awamu hii wakaamua kumfukuza nchini Mdai na kugoma kuendelea kufanya malipo, mpka wameshtakiwa Kwnye mahakama za nje/ south Africa bado tu huoni serikali hii ina lawama ya kujibu?
Hebu soma ulichoandika mwenyewe kwanza, mimi sielewi unamaanisha nini!.
 
Back
Top Bottom