Ukwelimtupu
Member
- Nov 21, 2011
- 36
- 13
Nimekuwa nikijiuliza hivi haya maandamano ya KITAIFA yaliyopangwa na CHADEMA kufanyika tarehe 1 Septemba 2016 yana tija ipi kwa TAIFA?
Je bunge kutorushwa LIVE inasababisha madhara yapi kwa CHADEMA?
Kwenye demokrasia yeyote anayeshindwa uchaguzi aidha hukubali kushindwa au hukataa kushindwa. Ukikubali kushindwa unatulia na kumwacha mshindi achape kazi. Mshindi akichapa kazi vizuri na kutekeleza mambo yaliyopo kwenye ilani yako, unampongeza na siyo kufanya maandamano nchi nzima.
Binafsi naona kama mikutano nchi nzima na mbwembwe za CHADEMA kwa sasa zinatokana na hofu ya kukosa umaarufu baada ya matatizo yaliyokuwa sugu na kukipa CHADEMA sifa kuanza kushughulikiwa na JPM.
Nawaomba CHADEMA watulie, wajenge CHADEMA kwanza kabla ya kulalamika kuhusu udikteta wa JPM. Siamini kama waanachama wa CHADEMA walishirikishwa kumchagua Lowassa kama mgombea wa UKAWA. Shurti ilitumika. Freeman Mbowe alitumia ubabe kumsimika Lowassa kama mgombea wa Rais. GIA ILIGEUZIWA ANGANI. Iweje leo CHADEMA walalamike kuhusu udikteta?
Je bunge kutorushwa LIVE inasababisha madhara yapi kwa CHADEMA?
Kwenye demokrasia yeyote anayeshindwa uchaguzi aidha hukubali kushindwa au hukataa kushindwa. Ukikubali kushindwa unatulia na kumwacha mshindi achape kazi. Mshindi akichapa kazi vizuri na kutekeleza mambo yaliyopo kwenye ilani yako, unampongeza na siyo kufanya maandamano nchi nzima.
Binafsi naona kama mikutano nchi nzima na mbwembwe za CHADEMA kwa sasa zinatokana na hofu ya kukosa umaarufu baada ya matatizo yaliyokuwa sugu na kukipa CHADEMA sifa kuanza kushughulikiwa na JPM.
Nawaomba CHADEMA watulie, wajenge CHADEMA kwanza kabla ya kulalamika kuhusu udikteta wa JPM. Siamini kama waanachama wa CHADEMA walishirikishwa kumchagua Lowassa kama mgombea wa UKAWA. Shurti ilitumika. Freeman Mbowe alitumia ubabe kumsimika Lowassa kama mgombea wa Rais. GIA ILIGEUZIWA ANGANI. Iweje leo CHADEMA walalamike kuhusu udikteta?