Maandamano Dar kupinga kudhalilishwa kwa viongozi wakuu wa serikali ya Tanzania...

Labda ni trick ya waandamanaji ili na madudu mengine tuyafaham bila shaka hayo aliyoyasema mama huyu ni Tips tu ya Iceberg -Mi naunnga mkono maandamano
 
Nini tene? Huseta na dagan kimbwereza? He watu wanatafuta ulaji mapema kabla jua halijachwa. Hata mwanangu wa std 3 anajua uozo wa nchi yake, sembuse sisi watu wazima. Jk sijui utawaridhishaje hawa watu, kila mmoja anatafuta singo ya kutokea. Ifike wakati mh. Rais wengine uwapotezee, maana wanaibuka tu ka wehu na kutangaza sera
 
Kupoteza muda tu, mbona hapa nchini pana kauli nyingi tu dhidi ya mheshimiwa rais toka kwa wananchi au kwa kuwa ni mzungu?
 
Kama wewe sio mtanzania mnafiki, bali unapenda nchi yetu iwe na maendeleo ya dhati, basi utakubaliana na mimi kuwa huyu raia wa kigeni anastahili kuungwa mkono kwa kufanya maandamano. Hakuna kilichofichika, na wala huhitaji kuwa na Phd ili kujua kuwa utawala wa nchi yetu ni mbovu, na nchi yetu inazidi kudidimia kila kunapokucha. Viongozi wa Mamlaka nyingi wanaendesha mambo kiholela, na kwa kujali maslahi binafsi, na si kwa manufaa ya nchi na wananchi wake.

Mambo mengi maovu yanayotokea kwa sasa wengi tumekuwa tukiyasikia yakitokea katika nchi zingine, lakini hatukuwahi kudhani yangeweza kutokea ndani ya kisiwa cha amani, namaanisha Tanzania.

Kibaya zaidi ni kwamba sisi watanzania hatuna uthubutu wa kuongea ukweli. Nahisi tamaduni zetu za kusema Baba akikosea jambo hupaswi kumkosoa. Hili ndio kosa kubwa alilofanya ''Huyu raia wa kigeni'' Amethubutu kusema ukweli. Sasa wahusika wanakasirika kwasababu hawajazoea kusemwa. Si utamaduni wao kusemwa.

Tusipokubali kuwakosoa watendaji wanaohujumu mali za umma, wasiowajibika, na wasiojali maendeleo ya nchi yetu, basi hali itazidi kuwa tete zaidi ya ilivyo kwa sasa. Tuache unafiki, tuwe wakweli, tuandike, tuwaseme bila kukata tamaa.

Lakini kwa upande mwingine mtu unajiuliza:


1. Shinikizo la kumshambulia huyu Raia wa kigeni linatoka wapi?

2. Kwanini watanzania hatuandamani kwa mambo kama EPA, Tanesco, Richmond, wabunge kupandishwa mishahara, matokeo mabovu ya form 4, na mengine mengi ambayo orodha yake ni ndefu; ili kushinikiza wahusika waachie ngazi, na tupate watendaji bora?


Nawasilisha.
 
Kama wewe sio mtanzania mnafiki, bali unapenda nchi yetu iwe na maendeleo ya dhati, basi utakubaliana na mimi kuwa huyu raia wa kigeni anastahili kuungwa mkono kwa kufanya maandamano. Hakuna kilichofichika, na wala huhitaji kuwa na Phd ili kujua kuwa utawala wa nchi yetu ni mbovu, na nchi yetu inazidi kudidimia kila kunapokucha. Viongozi wa Mamlaka nyingi wanaendesha mambo kiholela, na kwa kujali maslahi binafsi, na si kwa manufaa ya nchi na wananchi wake.

Mambo mengi maovu yanayotokea kwa sasa wengi tumekuwa tukiyasikia yakitokea katika nchi zingine, lakini hatukuwahi kudhani yangeweza kutokea ndani ya kisiwa cha amani, namaanisha Tanzania.

Kibaya zaidi ni kwamba sisi watanzania hatuna uthubutu wa kuongea ukweli. Nahisi tamaduni zetu za kusema Baba akikosea jambo hupaswi kumkosoa. Hili ndio kosa kubwa alilofanya ''Huyu raia wa kigeni'' Amethubutu kusema ukweli. Sasa wahusika wanakasirika kwasababu hawajazoea kusemwa. Si utamaduni wao kusemwa.

Tusipokubali kuwakosoa watendaji wanaohujumu mali za umma, wasiowajibika, na wasiojali maendeleo ya nchi yetu, basi hali itazidi kuwa tete zaidi ya ilivyo kwa sasa. Tuache unafiki, tuwe wakweli, tuandike, tuwaseme bila kukata tamaa.

Lakini kwa upande mwingine mtu unajiuliza:


1. Shinikizo la kumshambulia huyu Raia wa kigeni linatoka wapi?

2. Kwanini watanzania hatuandamani kwa mambo kama EPA, Tanesco, Richmond, wabunge kupandishwa mishahara, matokeo mabovu ya form 4, na mengine mengi ambayo orodha yake ni ndefu; ili kushinikiza wahusika waachie ngazi, na tupate watendaji bora?


Nawasilisha.

Shinikizo linatoka kwa Reginald Mengi. hii inatokana na mgogoro aliokuwa nao huyu mama dhidi ya mdogo wa Mengi Bw Benjamini Mengi kuhusu shamba alilokodo huyu mama kama mwekezaji wa kigeni.
 
huo nao utakuwa unafiki mwingine mbona doctor Slaa alipotaja list of shame na kila mtu na kosa lake kwenye ile first 11 kwa nn hamkuandaa maandamano kuunga mkono? ikaja kashfa ya EPA kimya?? ikaja Richmond kimya? Radar kimya?? mabilioni ya uswiss kimya na nyingine nyingi kimya?? Huyu mzungu amesema kipi kipya ambacho hakijawahi kusemwa? Au kwa sababu ni mzungu? Nafikiri maandamano ya maana zaidi yangekuwa ya kujilaani sisi Watanzania wenyewe kwa kuwa goigoi kupigania taifa letu na kulinasua kutoka kwenye makucha ya mafisadi na wezi wa rasimali zetu!!
 
Umewasilisha vema.Hao wanafiki wanaotaka kuaandamana eti kwa sababu raia tena wa kigeni kasema nchi inanuka rushwawache kutumiwa.Hivi kweli kunahitaji kufikiria kujua nchi hii viongozi wananuka rushwa?kabla hawajaandama watujibu mwaswali yafuatatyo:Chenji ya radar,Pesa za EPA,DOWANS,RICHMOND,TAN GOLD,mikataba ya madini nk.Halafu ina maana wanampinga mzee Makamba aliyeamua kuwa wazi na kusema ufisadi na rushwa vitaingusha CCM?Nafikiri kwa hili yafaa tuandamane kumpngeza maana ametusemea sis waoga pamoja na nyie wanafiki mnaotaka eti kuandamana.Jamani tuandamane kwa mambo muhimu hali ya maoisha ngumu,bei za bidhaa ju,elimu inakufa,udini naa ukabila vinashika kasi tuandamane kwa haya
 
Ha! Ha! Ha! Haya sasa , hawa wanatoka Mashariki wanaandamana kupinga , wengine wanatoka West wanaandamana kuunga mkono ! Mbona Kazi !
 
Dawa yao ndogo tu: WAKIPITA NA MAANDAMANO YAO YA KIJINGA, WAZOMEWE NJIA NZIMA: NDIO WATAPATA AKILI!
 
Heri kuandamana kumpongeza mzungu msema kweli kuliko kuandamana kumpinga msema kweli.
 
Nasi tuliopo dar tukae barabarani kesho atakayeandamana azomewe. ni uendawazimu kuandamana huku tunalia ufisadi. Watanzania tusitolewe akili na huyo bwana mmoja mpuuzi. aandamane mwenyewe. Wapenda haki tungeungana kumpongeza huyu mama Sarah.
 
kuchanganyikiwa kubaya mtu unabuni vitu vya kishenzi.wewe tukupeleke mirembe kabla kichaa chako hakijalipuka.
 
Mimi naungana na maoni ya huyu mama wa uingereza kuwa kutuma PCCB kwenda kuchunguza kesi ya rada ni sawa na kutuma mwizi kwenda kuchunguza mwizi mwenzake. Kwanza napingana mia kwa mia na huyu mnafiki anayeitisha maandamano kwenda ubalozi wa uingereza kupingana na huyu mama.
Tunapaswa kujiuliza maswali ya fuatayo
1. Ni idara ipi za serikali ya ccm ambayo haijajaa ufisadi? PCCB, usalama, elimu, Afya, Police, miunombinu au ni ipi ambayo watazania hatuishi kwa kutegemea ufisadi? Ndivyo serikali ya ccm inavyotaka na inavyotupeleka.
2. Kama ni uongo, naomba huyo bwana anayeitisha maadamano atuambie kipato chake na naishi vipi? analisha watoto, anasomesha, analipa kodi, anawavisha, anagharimaia gari lake kwa matengenezo na mafuta (Tsh2300?- per liter), pengine anashinda baa, anatibu familia yake, anasaidia ndugu na majirani kwa dharura, analipa umeme na maji, analipa kodi ya mapato, kuna huduma ya ziada imeongezeka ya vigng'amuzi, ananunua vocha za simu... tena tatu na huyu ukifuatilia utagundua anajenga. Mshahara wake ni kiasi gani kwa mwezi?

nadhani huyu jamaa wa kuandamana kesho tena anastahili kuchunguzwa acounti zake zikiwemo za m-pesa kwani naamini 100% anavuta pesa kwa mafisadi ili ahamasishe maandamano ya kuwasafisha mafisadi.

Ni kweli huyu mama amekuja kama nabii na badala ya kuandamana tunapaswa kuitisha mdahalo wa kitaifa kujadili hii hali na hata kuona umuhimu wa kupata dira ya taifa ili tusikae tena kuongozwa na viongozi vipofi na wezi kama tulio nao.
 
kuna watu wanaudhi sana. Na huyu anaweza kukaa kwa wanaume akajiita mwanaume kweli?. bora kutokusoma kuliko kusoma na kua na akili kama za huyu mwenyekiti wa maandamano. mia
 
Published on 3 Mar 2013Taasisi ya Human settlement of Tanzania-HUSETA- imewataka wananchi kujitokeza katika maandamano yatakayoanzia viwanja vya Mnazi mmoja hadi ubalozi wa Uingereza kuwasilisha azimio la kuitaka serikali ya Uingereza kutoa tamko hadharani la kutohusika na maovu yanayofanywa na baadhi ya raia wa nchi hiyo dhidi ya taifa la Tanzania ikiwemo kashfa na udhalilishaji kwa viongozi wa Ngazi za juu wa serikali.

Wito watolewa kuandamana kupinga kashfa kwa viongozi...


source: ITV TANZANIA youtube


N.B
Naona taasisi hii ya HUSETA imekosa kazi za muhimu kutetea mambo muhimu yanayowakera wananchi kama kama kukosa hati miliki za makazi yao, viwanja vyao n.k ili kama kutatokea neema madini, gesi kugunduliwa ktk maeneo wananchi wanayoyamiliki kwa hati waweze kupata kifuta jasho kinachostahili na siyo kufukuzwa toka maeneo yao kwa kisingizio ardhi ni mali ya serikali.


KWANI HII KATUNI NI YA UONGO? Si ndiyo halihalisi ya Tanzania?

government fed by the people_thumb[2].jpg
 
Last edited by a moderator:
Published on 3 Mar 2013Taasisi ya Human settlement of Tanzania-HUSETA- imewataka wananchi kujitokeza katika maandamano yatakayoanzia viwanja vya Mnazi mmoja hadi ubalozi wa Uingereza kuwasilisha azimio la kuitaka serikali ya Uingereza kutoa tamko hadharani la kutohusika na maovu yanayofanywa na baadhi ya raia wa nchi hiyo dhidi ya taifa la Tanzania ikiwemo kashfa na udhalilishaji kwa viongozi wa Ngazi za juu wa serikali.

Wito watolewa kuandamana kupinga kashfa kwa viongozi...


source: ITV TANZANIA youtube


N.B
Naona taasisi hii ya HUSETA imekosa kazi za muhimu kutetea mambo muhimu yanayowakera wananchi kama kama kukosa hati miliki za makazi yao, viwanja vyao n.k ili kama kutatokea neema madini, gesi kugunduliwa ktk maeneo wananchi wanayoyamiliki kwa hati waweze kupata kifuta jasho kinachostahili na siyo kufukuzwa toka maeneo yao kwa kisingizio ardhi ni mali ya serikali.


watu wazima njaa inawasumbua...wanatumiwa na Mengi...kujaribu kujisafisha kesi yake na huyoo mzungu..kosa lile lile alofanya akaonekana ana makosa kule uingereza ndo analirejea...
sasa aibu gani ati mnaandamana kwa matamshi ya muingereza mmoja asiye kuwa kiongozi...
wacheni njaa
 
Last edited by a moderator:
Hakika hata Mimi naona anajipendekeza kwa mafisadi ili apate japo ka cheo Huko CCM, Kwa sababu ni suala la kushukuru kwa kumpata wa kutusemea Matatizo yetu wanyonge, Kwani Rushwa na Udhaifu wa Kiongozi wa Nchi Kila Mtu anaona, Madudu ya CCm yako Peupeeee,
Huyo Dagan Kimbwereza atakuwa kibaraka wa magogoni au ana unanasaba na kiongozi dhaifu.
 
Back
Top Bottom