Maandamano CHADEMA na Escape from Sobibor

Maandamano CHADEMA na Escape from Sobibor

Mjomba wa taifa

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2012
Posts
231
Reaction score
161
Naangalia picha ya zamani iitwayo Escape From Sobibor, naona mtu asie askari kasimama juu anapuliza kipenga ishara ya kuwaita mateka wote katika ngome ya kufanyishwa kazi chini ya utawala wa kijerumani. Vuguvugu limepamba moto, mateka wanatoroka kwa kukata Senyenge zenye miba mikali. Risasi zinalia kuzuia vuguvugu.

Jambo la kushangaza naona kuna baadhi ya mateka wamesimama tu hawajishughulishi kutoroka Sobibor. Ninapata dhana kuwa either hawana mbio kushindana na askari ama wamependezwa na maisha ya pale kwa kuwa wanyapara.

Ghafla nashtuka kumbe nilikuwa ndotoni, nafunua pazia nje naona bendera za M4C na maandamano makubwa ya watanzania wakiimba "tumechoka kudhulumiwa haki zetu leo ndio mwisho wa dhuluma." Wengine wanaimba "Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gesi, Mbuga za Wanyama, Bahari, Maziwa, Mito, Ardhi yenye rutuba, milima lakini bado watoto wetu wanakufa kwa malaria, kipindupindu hakuna pesa za kuwatibu, wanafunzi wanasoma darasani hakuna madawati, madaftari yamweunganishwa kwa nyuzi za viatu"

Kundi la tatu linapita likipaza sauti zaidi ya makundi yaliyopita, "watoto wa viongozi ajira zao BOT, NSSF, PSPF, Bandari, TRA, Ikulu, Bungeni, Ofisi za Kibalozi, Hazina, baba kigogo wa nchi, mtoto mwakilishi fisadi, mama mjumbe fisadi, shemeji mnene RIJESI RA PORISI, uncle Waziri wa madarasa, Dada Katibu Mkuu, maswahiba wamekamata tender zote, utawala kurithishana hali ya kuwa watoto wa masikini waende VETA kujifunza kushika misumeno, kuchimba mitaro, umachinga, ukarani"

Nasikia sauti kwa mbali inakuja inaimba kwa nguvu "rushwa barabarani, hospitalini, tender serikalini .. vijana wote tokeni nje tupiganie nchi yetu"

Duh! Maneno makali yamenigusa uzalendo umenishinda nakimbia nje nikiwa na kaptura yangu kifua wazi. Mara nasikia kichwani sauti ya marehemu babu yangu inasema "mjukuu wangu beba galoni ya maji, vaa suruari na shati la mikono mirefu, huko uendako kuna mabomu na maji ya kuwasha".

Napita kumwamsha rafiki yangu KINENE katika chumba chake alichopanga ambaye tulimaliza nae chuo kikuu Mlimani miaka 4 iliyopita ambaye anafanya kibarua kama Volunteer kugawa vipeperushi vya kampuni moja mpya ya Simu. Namwambia Twende kwenye maandamano ya kujikomboa, ananyanyuka toka kwenye jamvi alilolalia, anafunua pazia la Khanga iliyoshonwashonwa kwa kuchakaa ananijibu "wewe huogopi mabomu mimi siendi huko naenda kugawa vipeperushi"

Shiiiiit, Graduate anagawa vipeperushi barabarani??? 4 years mtaani!!!!!!???

Nakumbuka tena picha niliyoiona ndotoni ya Escape from Sobibor, bado kulikuwa na mateka waliogoma kutoroka, duh!
 
Naangalia picha ya zamani iitwayo Escape From Sobibor, naona mtu asie askari kasimama juu anapuliza kipenga ishara ya kuwaita mateka wote katika ngome ya kufanyishwa kazi chini ya utawala wa kijerumani. Vuguvugu limepamba moto, mateka wanatoroka kwa kukata Senyenge zenye miba mikali. Risasi zinalia kuzuia vuguvugu.

Jambo la kushangaza naona kuna baadhi ya mateka wamesimama tu hawajishughulishi kutoroka Sobibor. Ninapata dhana kuwa either hawana mbio kushindana na askari ama wamependezwa na maisha ya pale kwa kuwa wanyapara.

Ghafla nashtuka kumbe nilikuwa ndotoni, nafunua pazia nje naona bendera za M4C na maandamano makubwa ya watanzania wakiimba "tumechoka kudhulumiwa haki zetu leo ndio mwisho wa dhuluma." Wengine wanaimba "Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gesi, Mbuga za Wanyama, Bahari, Maziwa, Mito, Ardhi yenye rutuba, milima lakini bado watoto wetu wanakufa kwa malaria, kipindupindu hakuna pesa za kuwatibu, wanafunzi wanasoma darasani hakuna madawati, madaftari yamweunganishwa kwa nyuzi za viatu"

Kundi la tatu linapita likipaza sauti zaidi ya makundi yaliyopita, "watoto wa viongozi ajira zao BOT, NSSF, PSPF, Bandari, TRA, Ikulu, Bungeni, Ofisi za Kibalozi, Hazina, baba kigogo wa nchi, mtoto mwakilishi fisadi, mama mjumbe fisadi, shemeji mnene RIJESI RA PORISI, uncle Waziri wa madarasa, Dada Katibu Mkuu, maswahiba wamekamata tender zote, utawala kurithishana hali ya kuwa watoto wa masikini waende VETA kujifunza kushika misumeno, kuchimba mitaro, umachinga, ukarani"

Nasikia sauti kwa mbali inakuja inaimba kwa nguvu "rushwa barabarani, hospitalini, tender serikalini .. vijana wote tokeni nje tupiganie nchi yetu"

Duh! Maneno makali yamenigusa uzalendo umenishinda nakimbia nje nikiwa na kaptura yangu kifua wazi. Mara nasikia kichwani sauti ya marehemu babu yangu inasema "mjukuu wangu beba galoni ya maji, vaa suruari na shati la mikono mirefu, huko uendako kuna mabomu na maji ya kuwasha".

Napita kumwamsha rafiki yangu KINENE katika chumba chake alichopanga ambaye tulimaliza nae chuo kikuu Mlimani miaka 4 iliyopita ambaye anafanya kibarua kama Volunteer kugawa vipeperushi vya kampuni moja mpya ya Simu. Namwambia Twende kwenye maandamano ya kujikomboa, ananyanyuka toka kwenye jamvi alilolalia, anafunua pazia la Khanga iliyoshonwashonwa kwa kuchakaa ananijibu "wewe huogopi mabomu mimi siendi huko naenda kugawa vipeperushi"

Shiiiiit, Graduate anagawa vipeperushi barabarani??? 4 years mtaani!!!!!!???

Nakumbuka tena picha niliyoiona ndotoni ya Escape from Sobibor, bado kulikuwa na mateka waliogoma kutoroka, duh!

Hii habari yako inanikumbusha yaliyotokea KENYA, watu waliandamana kudai haki ya matokeo ya uchaguzi mkuu baada ya kibaki kujitangaza kuwa raisi, watu wengi sana walikufa , majerui walikuwa wengi na wengine nyumba zao zilichomwa hadi leo wako kwenye maema hawakujengewa nyumba. Wale waliokuwa wanahamasisha maandamano walikaa chini na kugawana madaraka na kuwasahau wale waandamanaji. DUNIANI hamna haki, haki mbinguni, hutakuja kufa au kuumia alafu wenzako wakapatana baadae wakagawana vyeo. Akiri kumkichwa.
 
Naangalia picha ya zamani iitwayo Escape From Sobibor, naona mtu asie askari kasimama juu anapuliza kipenga ishara ya kuwaita mateka wote katika ngome ya kufanyishwa kazi chini ya utawala wa kijerumani. Vuguvugu limepamba moto, mateka wanatoroka kwa kukata Senyenge zenye miba mikali. Risasi zinalia kuzuia vuguvugu.

Jambo la kushangaza naona kuna baadhi ya mateka wamesimama tu hawajishughulishi kutoroka Sobibor. Ninapata dhana kuwa either hawana mbio kushindana na askari ama wamependezwa na maisha ya pale kwa kuwa wanyapara.

Ghafla nashtuka kumbe nilikuwa ndotoni, nafunua pazia nje naona bendera za M4C na maandamano makubwa ya watanzania wakiimba "tumechoka kudhulumiwa haki zetu leo ndio mwisho wa dhuluma." Wengine wanaimba "Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gesi, Mbuga za Wanyama, Bahari, Maziwa, Mito, Ardhi yenye rutuba, milima lakini bado watoto wetu wanakufa kwa malaria, kipindupindu hakuna pesa za kuwatibu, wanafunzi wanasoma darasani hakuna madawati, madaftari yamweunganishwa kwa nyuzi za viatu"

Kundi la tatu linapita likipaza sauti zaidi ya makundi yaliyopita, "watoto wa viongozi ajira zao BOT, NSSF, PSPF, Bandari, TRA, Ikulu, Bungeni, Ofisi za Kibalozi, Hazina, baba kigogo wa nchi, mtoto mwakilishi fisadi, mama mjumbe fisadi, shemeji mnene RIJESI RA PORISI, uncle Waziri wa madarasa, Dada Katibu Mkuu, maswahiba wamekamata tender zote, utawala kurithishana hali ya kuwa watoto wa masikini waende VETA kujifunza kushika misumeno, kuchimba mitaro, umachinga, ukarani"

Nasikia sauti kwa mbali inakuja inaimba kwa nguvu "rushwa barabarani, hospitalini, tender serikalini .. vijana wote tokeni nje tupiganie nchi yetu"

Duh! Maneno makali yamenigusa uzalendo umenishinda nakimbia nje nikiwa na kaptura yangu kifua wazi. Mara nasikia kichwani sauti ya marehemu babu yangu inasema "mjukuu wangu beba galoni ya maji, vaa suruari na shati la mikono mirefu, huko uendako kuna mabomu na maji ya kuwasha".

Napita kumwamsha rafiki yangu KINENE katika chumba chake alichopanga ambaye tulimaliza nae chuo kikuu Mlimani miaka 4 iliyopita ambaye anafanya kibarua kama Volunteer kugawa vipeperushi vya kampuni moja mpya ya Simu. Namwambia Twende kwenye maandamano ya kujikomboa, ananyanyuka toka kwenye jamvi alilolalia, anafunua pazia la Khanga iliyoshonwashonwa kwa kuchakaa ananijibu "wewe huogopi mabomu mimi siendi huko naenda kugawa vipeperushi"

Shiiiiit, Graduate anagawa vipeperushi barabarani??? 4 years mtaani!!!!!!???

Nakumbuka tena picha niliyoiona ndotoni ya Escape from Sobibor, bado kulikuwa na mateka waliogoma kutoroka, duh!
Ukosefu wa elimu kwa Watanzania ndio mtaji wa CCM
 
That's Bg Up , We Love To Fight We Can Fight Fighting 4right. I Will Die Im Trying 2fight 4right ,jahbless This Situation.
 
Naangalia picha ya zamani iitwayo Escape From Sobibor, naona mtu asie askari kasimama juu anapuliza kipenga ishara ya kuwaita mateka wote katika ngome ya kufanyishwa kazi chini ya utawala wa kijerumani. Vuguvugu limepamba moto, mateka wanatoroka kwa kukata Senyenge zenye miba mikali. Risasi zinalia kuzuia vuguvugu.

Jambo la kushangaza naona kuna baadhi ya mateka wamesimama tu hawajishughulishi kutoroka Sobibor. Ninapata dhana kuwa either hawana mbio kushindana na askari ama wamependezwa na maisha ya pale kwa kuwa wanyapara.

Ghafla nashtuka kumbe nilikuwa ndotoni, nafunua pazia nje naona bendera za M4C na maandamano makubwa ya watanzania wakiimba "tumechoka kudhulumiwa haki zetu leo ndio mwisho wa dhuluma." Wengine wanaimba "Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gesi, Mbuga za Wanyama, Bahari, Maziwa, Mito, Ardhi yenye rutuba, milima lakini bado watoto wetu wanakufa kwa malaria, kipindupindu hakuna pesa za kuwatibu, wanafunzi wanasoma darasani hakuna madawati, madaftari yamweunganishwa kwa nyuzi za viatu"

Kundi la tatu linapita likipaza sauti zaidi ya makundi yaliyopita, "watoto wa viongozi ajira zao BOT, NSSF, PSPF, Bandari, TRA, Ikulu, Bungeni, Ofisi za Kibalozi, Hazina, baba kigogo wa nchi, mtoto mwakilishi fisadi, mama mjumbe fisadi, shemeji mnene RIJESI RA PORISI, uncle Waziri wa madarasa, Dada Katibu Mkuu, maswahiba wamekamata tender zote, utawala kurithishana hali ya kuwa watoto wa masikini waende VETA kujifunza kushika misumeno, kuchimba mitaro, umachinga, ukarani"

Nasikia sauti kwa mbali inakuja inaimba kwa nguvu "rushwa barabarani, hospitalini, tender serikalini .. vijana wote tokeni nje tupiganie nchi yetu"

Duh! Maneno makali yamenigusa uzalendo umenishinda nakimbia nje nikiwa na kaptura yangu kifua wazi. Mara nasikia kichwani sauti ya marehemu babu yangu inasema "mjukuu wangu beba galoni ya maji, vaa suruari na shati la mikono mirefu, huko uendako kuna mabomu na maji ya kuwasha".

Napita kumwamsha rafiki yangu KINENE katika chumba chake alichopanga ambaye tulimaliza nae chuo kikuu Mlimani miaka 4 iliyopita ambaye anafanya kibarua kama Volunteer kugawa vipeperushi vya kampuni moja mpya ya Simu. Namwambia Twende kwenye maandamano ya kujikomboa, ananyanyuka toka kwenye jamvi alilolalia, anafunua pazia la Khanga iliyoshonwashonwa kwa kuchakaa ananijibu "wewe huogopi mabomu mimi siendi huko naenda kugawa vipeperushi"

Shiiiiit, Graduate anagawa vipeperushi barabarani??? 4 years mtaani!!!!!!???

Nakumbuka tena picha niliyoiona ndotoni ya Escape from Sobibor, bado kulikuwa na mateka waliogoma kutoroka, duh!

du.......imenigusa sana kama ihi kitu ni alisia. hapo ulipo mkuu. nchi yetu inasikitisha sana watawala ni kama wapo usingizini tena usingizi wapono. macho yao yamejaa magamba hawaoni na masikio wametia gunzi la chuma. hawajui wala hawataki kujua wapo kwa maslai yao na familia zao. na kumbuka usemi wa ben mkapa mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe. tangupale wenye akili zetu tuligundua kwamba serikali imeanza kuwatelekeza wananchi. kwa kukwepa wajibu wake kikatiba. kama serikali ingetimiza wajibu wake.kusingekuwa na kundi la kuandamana watu hawana ajira ajira ni zakiundugu serikalini. wasomi wanaishia kuwa wachuuzi na umachinga barabarani kila kukicha wanakimbizwa na migambo wa jiji. wezi wameongezeka matumaini kwa serikali yamepotea. mafisadi yanalindwa kwa nguvu kubwa. je hapo watu wataacha kuandamana? hali wanaona watu wanagawana laki 3 kila siku aliwao hawajui hata uhakika wa mlo wa mchana? mungu atuepushie mbali maana kiona mbali kinatoa ishara mbaya sana kwa taifa letu tanzania. watawala amkeni usingizini hali ni mbaya sana. kabla mambo hayaja aribika.
 
Naangalia picha ya zamani iitwayo Escape From Sobibor, naona mtu asie askari kasimama juu anapuliza kipenga ishara ya kuwaita mateka wote katika ngome ya kufanyishwa kazi chini ya utawala wa kijerumani. Vuguvugu limepamba moto, mateka wanatoroka kwa kukata Senyenge zenye miba mikali. Risasi zinalia kuzuia vuguvugu.

Jambo la kushangaza naona kuna baadhi ya mateka wamesimama tu hawajishughulishi kutoroka Sobibor. Ninapata dhana kuwa either hawana mbio kushindana na askari ama wamependezwa na maisha ya pale kwa kuwa wanyapara.

Ghafla nashtuka kumbe nilikuwa ndotoni, nafunua pazia nje naona bendera za M4C na maandamano makubwa ya watanzania wakiimba "tumechoka kudhulumiwa haki zetu leo ndio mwisho wa dhuluma." Wengine wanaimba "Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gesi, Mbuga za Wanyama, Bahari, Maziwa, Mito, Ardhi yenye rutuba, milima lakini bado watoto wetu wanakufa kwa malaria, kipindupindu hakuna pesa za kuwatibu, wanafunzi wanasoma darasani hakuna madawati, madaftari yamweunganishwa kwa nyuzi za viatu"

Kundi la tatu linapita likipaza sauti zaidi ya makundi yaliyopita, "watoto wa viongozi ajira zao BOT, NSSF, PSPF, Bandari, TRA, Ikulu, Bungeni, Ofisi za Kibalozi, Hazina, baba kigogo wa nchi, mtoto mwakilishi fisadi, mama mjumbe fisadi, shemeji mnene RIJESI RA PORISI, uncle Waziri wa madarasa, Dada Katibu Mkuu, maswahiba wamekamata tender zote, utawala kurithishana hali ya kuwa watoto wa masikini waende VETA kujifunza kushika misumeno, kuchimba mitaro, umachinga, ukarani"

Nasikia sauti kwa mbali inakuja inaimba kwa nguvu "rushwa barabarani, hospitalini, tender serikalini .. vijana wote tokeni nje tupiganie nchi yetu"

Duh! Maneno makali yamenigusa uzalendo umenishinda nakimbia nje nikiwa na kaptura yangu kifua wazi. Mara nasikia kichwani sauti ya marehemu babu yangu inasema "mjukuu wangu beba galoni ya maji, vaa suruari na shati la mikono mirefu, huko uendako kuna mabomu na maji ya kuwasha".

Napita kumwamsha rafiki yangu KINENE katika chumba chake alichopanga ambaye tulimaliza nae chuo kikuu Mlimani miaka 4 iliyopita ambaye anafanya kibarua kama Volunteer kugawa vipeperushi vya kampuni moja mpya ya Simu. Namwambia Twende kwenye maandamano ya kujikomboa, ananyanyuka toka kwenye jamvi alilolalia, anafunua pazia la Khanga iliyoshonwashonwa kwa kuchakaa ananijibu "wewe huogopi mabomu mimi siendi huko naenda kugawa vipeperushi"

Shiiiiit, Graduate anagawa vipeperushi barabarani??? 4 years mtaani!!!!!!???

Nakumbuka tena picha niliyoiona ndotoni ya Escape from Sobibor, bado kulikuwa na mateka waliogoma kutoroka, duh!

Hii habari yako inanikumbusha yaliyotokea KENYA, watu waliandamana kudai haki ya matokeo ya uchaguzi mkuu baada ya kibaki kujitangaza kuwa raisi, watu wengi sana walikufa , majerui walikuwa wengi na wengine nyumba zao zilichomwa hadi leo wako kwenye maema hawakujengewa nyumba. Wale waliokuwa wanahamasisha maandamano walikaa chini na kugawana madaraka na kuwasahau wale waandamanaji. DUNIANI hamna haki, haki mbinguni, hutakuja kufa au kuumia alafu wenzako wakapatana baadae wakagawana vyeo. Akiri kumkichwa.
 
A VISIONARY WRITER!!. Siku si nyingi ndiko tunakoelekea ambapo kila mtu atakuwa anafunguka kutoa yaliyoko moyoni. Utakuwa mwendo wa "ENOUGH IS ENOUGH na LIWALO NA LIWE"
 
Nimeguswa sana na hii simulizi and it is relevant to our situation today.

Huko ndiko hasa tunakokutaka na tayari tumeshafika!!..

Personally niko tayari kuitikia kipenga cha kutoka katika utumwa wa kufanyishwa kazi za kifungwa na hapa sitabaki kuzubaa zubaa kama wale watumwa wenzetu maCCM (daraja la tatu) na katika story hii tuyafananishe na manyampara na ambayo yapo yanashangaa shangaa tu kwa sababu ya kutokuelewa nini kinaendelea!!

Inaumiza sana kwa situation ambayo nchi yetu imefikia kwa sasa. Yaani watu wanjitengenezea mazingira ya kisheria, sheria za kidhuluma kwa ajili ya kujipatia rasrimali za nchi wao tu huku wakiwaacha wananchi maskini wasio na uwezo wakitaaabika katika mtungi wa huduma dhoofu na duni kabisa za kijamii. Mfano mzuri na wa jana tu yule kijana mwanafunzi wa Ihungo Secondary School aliyeaamua kujiua kwa sababu ya kukaa siku tatu hospitalini (hosptali ya mkoa!) pasipo kupata matibabu. Na ni wazi si kwa sbb ziwazo zozote bali ni aidha hakuna dawa au hakuna mfumo dhabiti wa kuhudumia wagonjwa, mfumo wa kifisadi!!..

Mfano mwingine wa wazi kabisa kuonesha kuwa kuna watu katika nchi hiihii wakiamua leo au kesho wajilipe mabilioni ya fedha pasipo hata kufanya kazi na kuwaacha watu ambao wanafanya kazi kweli kweli hadi tone lao la mwisho la damu pasipo kuambulia hata ingalau ule ujira wao halali na wa haki na kwa wakati wanajilipa tu bila ya matatizo ya kujiuliza fedha watoe wapi au ziko wapi, unawahusu walimu kama mia mbili na hamsini hivi (250) wa wilaya ya Nzega (kwa Hamisi Kigwangallah) mkoani Tabora kama ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari na mimi mwenyewe kuwashuhudia kwani ilikuwa kidogo wawatwange mangumi viongozi wao wa CWT (Chama Cha Walimu Tanzania wa wilaya) pamoja na wale wa Halmashauri (serikali) ya wilaya yao kwa maana ya DED na HRO kwa kudhani kuwa hawashughulikii ipasavyo kero yao hii!!.

Basically,haingii akili kwa namna yoyote kuwa kuna watu wanachota takribani Tshs. 450,000/= kwa siku moja sawa na Tshs takribani 13,500,000/= kwa mwezi bila kukatiwa kodi ya Pay As You Earn (PAYE)!!....Huku wakiwa wamekaa kwenye viyoyozi tu wakati kuna watumishi wa umma (kama hawa walimu) wanao toil kweli kweli kutoa haduma kwa wananchi na katika mazingira magumu na yenye kutia kinyaa wanaambulia kiasi chini ya ya hicho kwa mwezi mzima na huku wakikatwa kodi kubwa katika ujira wao huo bila huruma wala longolongo kuliko maelezo!!.

Kinachoumiza unaweza kukuta kwa mfano hawa walimu 250 wa Nzega (na wengine popote pale walipo ktk Tanzania hii), likely wengine wanadai kiasi kidogo sana cha pesa masikini wa Mungu, labda laki mbili (200,000/=), au milioni moja (1,000,000/=) au hata Tshs, 50,000/- tu lakini inakuwa taabu kwelikweli kulipwa (mpaka wengine wanakufa na kuacha haki zao hizi kidogo) kwa sababu tu ya ubinafsi wa viongozi wetu hawa mahayawani wakisaidiwa mfumo mbovu, kandamizaji wa utawala unaowapendelea wao na watoto wao na wenye kuwatisha hawa wanyonge kudai haki zao ambao hawa watawala wameujenga kwa miaka mingi na wanatumia kila njia kuulinda na kuuimarisha ambacho ndicho kinachotokea huko Dodoma leo kwa kigezo eti wanaandika Katiba ya wananchi na kwamba eti BMK liko kisheria na hakuna mwenye uwezo wa kuliahirisha na hata kulifutilia mbali!!

Nikirudi kwa hawa walimu wa Nzega ni kwamba wanaidai serikali hiihii ya CCM inayofanya vituko hivi jumla ya takribani shilingi milioni mia saba na hamsini (750,000,000/=) kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji (W) na CWT Nzega ikiwa ni madai yao halali kabisa ya fedha za malimbikizo ya mishahara,matibabu,uhamisho,likizo nk,nk kwa miaka na miaka. Nimeongea nao wengine wanasema madai yao yapo tangu mwaka 2008 pasipo hata na dalili yoyote ya kulipwa kwa kisingizio cha eti serikali hii chini ya Chama Cha Mapinduzi a.k.a CCM haina fedha au kisingizio kingine ambacho ni very funny ni kuwa eti serikali inaendelea kufanya uhakiki wa madeni hayo!!

Najiuliza kwa walimu hawa wa Nzega tu,kwamba, laiti kama nchi hii ingekuwa na kiongozi sahihi na mwenye maamuzi yenye tija na asiyepepesa macho na anayeweza kutambua vipaumbele vya taifa hili vya muda mfupi na muda mrefu, pesa ya siku tano tu wanayolipwa hawa jamaa wa waliopo Dodoma wakiendelea na BMK ingetosha kuwalipa walimu hawa wa Nzega na wakaendelea kufanya kazi ya maana inayoonekana na yenye tija kuliko hawa hayawani walioko Dodoma ambao Work done yao watakayotoka nayo huko ni zero na huku wakiwa wametekeketeza mabilioni ya fedha amabazo rightfully persons wangelipwa. Wananchi wanapoanza kuilalamikia kazi wanayofanya ya uandishi wa Katiba hiyo, ujue mara moja kuwa hiyo kazi wanayofanya hapa Dodoma haina uhalali!!

Hawa ni walimu na watumishi wa umma wa wilaya moja, idara moja tu!!....Naamini na wilaya zingine,mikoa mingine wana madai kama hayahaya na majibu ya serikali ni hayahaya wakati wao wanapiga pesa kutoka katika hazina ilelile ambayo wanasema haina pesa na tayari Bwana mkubwa sana mtoto wa kitaa Jakaya Mrisho Kikwete yuko nje ya nchi yake isiyokuwa na pesa,yuko U.S.A anatanua tu,hajali na hana time na tension inayoendelea ku build katika nchi yake anayodai anaiongoza!!..

I think ENOUGH IS ENOUGH actions must be taken now na wenye nchi yao!!
 
Get out of your pathetic KEYBOARD and come out to streets for the riots. We are eagerly waiting for your dear spinal cord to break it......
Watz wamewashtukia, hamtaungwa mkono na yeyote zaidi ya wale wenye hulka za kubweka.. nadhani unawajua maana mnafanana
 
Umenikumbusha hii muvi,ilinisikitisha sana!Huu ni ushahidi kwingine kuwa dhuluma haitashindana na haki daima.
 
Mkuu umenitia ujasiri wa ajabu sana ! Japo nina jeraha mkono wa kulia lakini sijali sana , asante .
 
Get out of your pathetic KEYBOARD and come out to streets for the riots. We are eagerly waiting for your dear spinal cord to break it......
Watz wamewashtukia, hamtaungwa mkono na yeyote zaidi ya wale wenye hulka za kubweka.. nadhani unawajua maana mnafanana
Maandamano yamefanyika na yataendelea kufanyika bila kikomo , UOGA NDIYO DHAMBI MBAYA NA KUBWA KULIKO ZOTE , hao unaowategemea ni wepesi kuliko pamba ! Na ndio maana wanahangaika na meza ya mazungumzo , usithubutu kucheza na nguvu ya umma .
 
Babu na baba yangu walipigania uhuru wa taifa hili wala hatujafaidi chochote zaidi ya nyinyi kufaidika. labda piganeni na nyinyi tuone kama na sisi tutafaidika.

Naangalia picha ya zamani iitwayo Escape From Sobibor, naona mtu asie askari kasimama juu anapuliza kipenga ishara ya kuwaita mateka wote katika ngome ya kufanyishwa kazi chini ya utawala wa kijerumani. Vuguvugu limepamba moto, mateka wanatoroka kwa kukata Senyenge zenye miba mikali. Risasi zinalia kuzuia vuguvugu.

Jambo la kushangaza naona kuna baadhi ya mateka wamesimama tu hawajishughulishi kutoroka Sobibor. Ninapata dhana kuwa either hawana mbio kushindana na askari ama wamependezwa na maisha ya pale kwa kuwa wanyapara.

Ghafla nashtuka kumbe nilikuwa ndotoni, nafunua pazia nje naona bendera za M4C na maandamano makubwa ya watanzania wakiimba "tumechoka kudhulumiwa haki zetu leo ndio mwisho wa dhuluma." Wengine wanaimba "Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gesi, Mbuga za Wanyama, Bahari, Maziwa, Mito, Ardhi yenye rutuba, milima lakini bado watoto wetu wanakufa kwa malaria, kipindupindu hakuna pesa za kuwatibu, wanafunzi wanasoma darasani hakuna madawati, madaftari yamweunganishwa kwa nyuzi za viatu"

Kundi la tatu linapita likipaza sauti zaidi ya makundi yaliyopita, "watoto wa viongozi ajira zao BOT, NSSF, PSPF, Bandari, TRA, Ikulu, Bungeni, Ofisi za Kibalozi, Hazina, baba kigogo wa nchi, mtoto mwakilishi fisadi, mama mjumbe fisadi, shemeji mnene RIJESI RA PORISI, uncle Waziri wa madarasa, Dada Katibu Mkuu, maswahiba wamekamata tender zote, utawala kurithishana hali ya kuwa watoto wa masikini waende VETA kujifunza kushika misumeno, kuchimba mitaro, umachinga, ukarani"

Nasikia sauti kwa mbali inakuja inaimba kwa nguvu "rushwa barabarani, hospitalini, tender serikalini .. vijana wote tokeni nje tupiganie nchi yetu"

Duh! Maneno makali yamenigusa uzalendo umenishinda nakimbia nje nikiwa na kaptura yangu kifua wazi. Mara nasikia kichwani sauti ya marehemu babu yangu inasema "mjukuu wangu beba galoni ya maji, vaa suruari na shati la mikono mirefu, huko uendako kuna mabomu na maji ya kuwasha".

Napita kumwamsha rafiki yangu KINENE katika chumba chake alichopanga ambaye tulimaliza nae chuo kikuu Mlimani miaka 4 iliyopita ambaye anafanya kibarua kama Volunteer kugawa vipeperushi vya kampuni moja mpya ya Simu. Namwambia Twende kwenye maandamano ya kujikomboa, ananyanyuka toka kwenye jamvi alilolalia, anafunua pazia la Khanga iliyoshonwashonwa kwa kuchakaa ananijibu "wewe huogopi mabomu mimi siendi huko naenda kugawa vipeperushi"

Shiiiiit, Graduate anagawa vipeperushi barabarani??? 4 years mtaani!!!!!!???

Nakumbuka tena picha niliyoiona ndotoni ya Escape from Sobibor, bado kulikuwa na mateka waliogoma kutoroka, duh!
 
Hii habari yako inanikumbusha yaliyotokea KENYA, watu waliandamana kudai haki ya matokeo ya uchaguzi mkuu baada ya kibaki kujitangaza kuwa raisi, watu wengi sana walikufa , majerui walikuwa wengi na wengine nyumba zao zilichomwa hadi leo wako kwenye maema hawakujengewa nyumba. Wale waliokuwa wanahamasisha maandamano walikaa chini na kugawana madaraka na kuwasahau wale waandamanaji. DUNIANI hamna haki, haki mbinguni, hutakuja kufa au kuumia alafu wenzako wakapatana baadae wakagawana vyeo. Akiri kumkichwa.

Mzee Uchwara hapa hakuna cha maana sanana inafutwa tu kiki ya kisiasa ukizingatia 2015 sio mbali watu wapigwe waumiee baadae wakuu watoe matamko na baada ya wiki utawasikia wako ikulu wakitafuta maridhiano na Mr President halafu wahanga wa maandano wanaendelea kuteseka hospital bila hata msaada wa chama mbya zaidi hutasikia Mtoto au ndugu wa Mbowe au Slaa kaumizwa kwenye maandamano.

Hii pia umenikumbusha kwenye ile kesi ya Lema Arusha Lema kakataa kuwekewa dhamana eti anataka awaonyeshe watawala kwamba haogopi jela!! hazijapita hata siku mbili eti watu wanaambiwa waandamane kushinikiza Lema apewe dhamana kha!!! yaani mtu kaenda kwa hiari yake halafu aanze kusumbua watu kuandamana kisa kachoka kukaa Lupango halafu watu wanakubali kuandamana?? kweli waji..nga hawataisha dunia hii
 
Back
Top Bottom