Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,539
- 4,854
*SANAA NI NINI ?* Kwa maelfu ya miaka sanaa imekuwa ikiendelea kushika uzito katika jamii nyingi za wanadamu huku ikiwa ni msaada katika jamii tofauti sanaa ilikuwepo toka enzi na enzi kabla na baada ya mitume . Mitume walipokuja walikuta sanaa nyingi zikifanyika duniani, walikuta ushairi, nyimbo,? Chezaji, uchingaji, ufinyanzi na nyingine nyingi zikifanyika na hata baadhi ya sanaa zipo katika vitabu vitakatifu vya dini. Sanaa ni neno liliochukuliwa katika msemo wa kiarabu, unaomaanisha *ufundi wa kuwasilisha mawazo yaliyo katika fikra za mwanadamu* , maana ambayo inatumika pia katika kuelezea za nwana sanaa bora ambae anawekeza katika kuelezea maoni yake katika njia iliyobuniwa zaidi. Wengine hutafsiri neno sanaa kama *umbo lililisanifiwa katika ustadi na kusanifika* , sanaa inaweza kuwa katika umbo moja lakini likawa na maane zaidi ya elfu sanaa na kipawa ambacho kila binadamu amepewa kulingana na mungu alivyoamua kumpa kipawa ambacho kama kikitumik vyema kinakuwa na faida sana na kikitumika vibaya kinakuwa nahasara isiyo na mfano. Sanaa ni kipawa kitokacho katika akili ya ndani ya mwanadamu kipawa hiki kina muda maalumu wa kufunguka, kuna ambao watafungukiwa mapema sana na katika umri mdogo, kuna ambai kitafunguka katika umri wa kati, wengine umri wa ujana, uzee na utu uzima. Siyo kila mmoja inakuwa ni rahisi kwake kugundu kipawa chake, wengi wetu tumechelewa kugundua vipaji vyetu kunakotokana na sababu nyingi ikiwemo mazingirq tunayoishi ama tuliyoishi, mfumi wa jamii zetu watanzania nao huchangia katika kuficha vipawa vya watu.