Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Leo mchana niliingia kwenye restaurant moja hapa Moshi mjini inayotazamana na Shree Hindu Temple. Nikaagiza chakula wakaleta baada ya muda mrefu na kuwapigia kelele kwa sababu wahudumu walikuwa wanaangdalia video ya harusi sijui ya nani. Anyway, hiyo si muhimu. Baada ya kula nikashangaa wahudumu wananipita tu, nikashtukia dk 15 zimepita tangu nimalize kula. Nikamwita mhudumu kwa sauti ya ukali
MIMI : we mhudumu weeee
MHUDUMU: sema...
MIMI: Huoni kuwa nimemaliza kula?
MHUDUMU: kwahiyo...
MIMI: Nataka kulipa
MHUDUMU: lipa sasa
MIMI: shi'ng ngapi?
MHUDUMU: elfu tatu mia sita
MIMI: mbona unafanya kazi kama umelazimishwa?
MHUDUMU: hapa hatufukuzi wateja mzee...
MIMI : we mhudumu weeee
MHUDUMU: sema...
MIMI: Huoni kuwa nimemaliza kula?
MHUDUMU: kwahiyo...
MIMI: Nataka kulipa
MHUDUMU: lipa sasa
MIMI: shi'ng ngapi?
MHUDUMU: elfu tatu mia sita
MIMI: mbona unafanya kazi kama umelazimishwa?
MHUDUMU: hapa hatufukuzi wateja mzee...