Maana ya kuhonga katika ulimwengu wa kifikra

Victor Mlaki

JF-Expert Member
May 1, 2016
3,542
3,451
Leo kuna Dada zetu na Kaka zetu wengi wamenaswa kwenye mtego uliotokana na kuhongwa wakiamoni wanafaidika kumbe ni mtego.

Hongo ni mtego unaofanya kazi kwenye ulimwengu wa kifikra kuliko ulimwengu wa vitu vinavyoonekana na kubainika kupitia milango mitano ya fahamu.

Ili kubaini mitego hiyo sharti mlango wako wa sita wa fahamu uwe wazi na usiingiliwe na vichocheo vya nje.

Unapopokea hongo inakulazimisha kurahisisha uumbaji wa tukio analotazamia aliyekuhonga na hili linafanyika kwa hatari yako au kwa lazima,ni kama inakufanya upekee mitetemo ya nguvu za kiumbaji za aliyekuhonga na kumsaidia kutekeleza kusudi lake.

Kuna watu wameoa,wameolewa au wameoana kutokana na nguvu iliyopo nyuma ya hongo na siyo hongo yenyewe.

Wapo Dada zetu walioolewa kwa hongo za viazi mbatata na kachumbari na wengine kwa soda baridi.Halikadhalika wapo akina Kaka ambao nao leo wamejikuta kwenye ndoa kutokana na hongo.

Hongo ni sawa na sadaka inayotolewa kuwajulisha hitaji la mtu.Kuwa makini sana usipende sana ofa ofa au burebure.Ni James la hatari sana kupokea chochote kwa mtu yoyote bila kutafakari kwa kina na kuruhusu "akili ya akili yako kufanya kazi".

Kuna watu leo ni wamekuwa mateka wa watu wengine kutokana na kushindwa kuelewa nguvu inayoambatana na kile unachopewa na mtu mwingine ni nguvu gani.

Binadamu yeyote anapotoa sadaka makanisani,kwa waganga kusaidia masikini n.k huwa kuna kitu anaambatanisha nyuma ya kile anachotoa"kunuwia"na tunachokiambatanisha kina nguvu na ndicho kinachotakiwa.

Hakuna msaada wa bure"kipo kinachosemwa nyuma ya huo msaada"..hatupaswi kufurahia tunasaidiwa au tunahongwa sana ila tujiulize ni nini kinachoambatana na hongo hizo.

Kuna akina Dada na akina Kaka leo wanatamanj kuolewa na kuoa wanashindwa kwa sababu walishafungwa na nguvu iliyombatana na hongo za watu wengine walizowahi kupokea.Suala hili halihitaji kwenda kwa Mchungaji kuombewa ila kujitathmini kwanza kabla ya kukurupuka.

Hayupo anayotoa kitu chochote bure awe ni matajiri au masikini "kipo anachohitaji"na ndicho anachokiambatanisha na kile anachokupatia.

Unaweza ukaona unapewa gari pesa,ofisi nzuri n.k lakini jiulize ni kipi cha maana kufurahia "Je ni kile kidogo unachoona au kikubwa usichokiona nyuma ya kitu?).
 
.......................................................................
Hakuna msaada wa bure"kipo kinachosemwa nyuma ya huo msaada"..hatupaswi kufurahia tunasaidiwa au tunahongwa sana ila tujiulize ni nini kinachoambatana na hongo hizo.

....................................................................

Hayupo anayotoa kitu chochote bure awe ni matajiri au masikini "kipo anachohitaji"na ndicho anachokiambatanisha na kile anachokupatia.

.......................................................................
Mleta mada hapa napingana na wewe kwa nguvu zote. Sababu ni kuwa sio kweli kwamba kila msaada mtu anaotoa huwa anataka kitu in return. Mimi nina mifano yangu binafsi. Nimesaidia watu wengi japo hata kidogo bila kutegemea kupata chochote na mara nyingine bila hata kuwafahamu hata kwa jina moja tu.

Hivi mfano ukakutana na omba omba town akakuomba hela ya kula ukampa hapo unategemea akulipe nini? Labda akuombee kwa Mungu ulipopunguza paongezeke.

Kuna watu wanajitoa bila kutarajia kupokea mkuu. Mioyo ya watu iko tofauti.

Kiujumla tu naweza kukubaliana na wewe kama ungesema 'wengi wetu hutoa tukijarajia kulipwa kwa aina fulani'.
 
Kiujumla tu naweza kukubaliana na wewe kama ungesema 'wengi wetu hutoa tukijarajia kulipwa kwa aina fulani'.


Na ndivyo ilivyo 100% tunatoa ili tuje kulipwa, ama sivyo kutoa kunakuwa hakuna maana, ni kwamba ama uliyemsaidia akulipe au Mungu akulipe.
 
Anaye hongwa huwa siku zote ni mtumwa asiye jitambuwa na kujielewa wa yule mtoaji.

Kupokea kilicho stahili na kilicho cha haki huleta raha ya kweli ya ubinadamu kamili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta mada hapa napingana na wewe kwa nguvu zote. Sababu ni kuwa sio kweli kwamba kila msaada mtu anaotoa huwa anataka kitu in return. Mimi nina mifano yangu binafsi. Nimesaidia watu wengi japo hata kidogo bila kutegemea kupata chochote na mara nyingine bila hata kuwafahamu hata kwa jina moja tu.

Hivi mfano ukakutana na omba omba town akakuomba hela ya kula ukampa hapo unategemea akulipe nini? Labda akuombee kwa Mungu ulipopunguza paongezeke.

Kuna watu wanajitoa bila kutarajia kupokea mkuu iko tofauti.

Kiujumla tu naweza kukubaliana na wewe 'wengi



wetu hutoa tukijarajia kulipwa kwa aina fulani'.

Asante Mkuu ila inaonekana hujanielewa nimemaanisha nini hasa.Ipo hivi sijamaanisha ukimpa masikini unategemea huyo masikini akupe....la hasha !..
Unapaswa kuelewa kuwa chochote akipatacho mtu ni zao la nguvu uliyotumia kukivuta kwake.Ukimkuta mtu ambaye ni tajiri fahamu kuwa utajiri huo ni zao la mkusanyiko wa nguvu zilizotumika (nguvu za kimiwili,kiakili,kihisia na kani za uhai).
Nyuma ya kila kitu cha kila mtu kuna nguvu zilizotumika kukivuta kitu hicho na nguvu zilizosukuma hitaji la mtu huyo.Hayupo binadamu asiyehitaji chochote awe na ukwasi kiasi gani au fukara kiasi gani bado mahitaji yapo palepale.
Mtu akikupa kitu hata kama akisema ni kwa nia njema kama unavyosema bado kuna nguvu zilizotumika na zinabeba hitaji lake.
Mkuu hata ulipomsaidia huyo masikini nina uhakika uliamini hiyi ni sadaka umetoa kwa Mungu ili Mungu azidi akubariki na kukusaidia katika mahitaji yako uwe unajua au haujui.
 
Back
Top Bottom