Maamuzi ya Spika sio Obstruction of justice?

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
37,547
47,199
Hivi majuzi Mh. Spika alihitimisha mjadala wa muendelezo wa debate sehemu mbali mbali kuhusiana na vitwndo vya Polisi kuwakamata wabunge, kwa kutoa kauli kwamba, of is a yoyote anayemhitaji mbunge lazima amwambie!

Ingawa kwa macho ya wabunge wengi ni kauli sahihi, lakini Spika na wabunge wanasahau kwamba wabunge hawapo katika makundi ya watu wenye immunity ya kushtakiwa kutokana na makosa wanayoyafanya wakiwa wabunge kama kosa hilo halijafanyika ndani ya Bunge, ingawa Kuna utaratibu wa kumwajibisha mbunge kwa kosa atalolifanya akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge!

Kwakua basi wabunge wanastatus sawa kabisa na raia wengine wanapokua nje ya ukumbi wa Bunge sio vyema kuanza kutengeneza matabaka ya watu katika nchi hii tunayoishi wote.

Haiingii akilini kwanini mtu afanye kosa halafu itoke ruhusa ya Kumkamata au kutomkamata! Huko ni kupotoka na kuelewa madaraka tu tuliyowapa sisi kwa kura zetu wenyewe.

Katiba ya nchi haimuweki Mbunge juu ya sheria za nchi, wala haimpi mamlaka Spika ya kuzuia vyombo vya dola kufanya kazi yake pale inapotakiwa kufanya hivyo!

Ningependa kujua, agizo hilo la spika limetokana na sheria ipi na litakua na vigezo gani kwa spika kutoa ruhusa ya Mbunge kukamatwa!

Je, spika haoni kwamba ruhusa yake itakua imeprejudice court process!

Mfano akaletewa hati ya kukamatwa kwa mbunge! Akasema hapana asikamatwe! Haoni kwamba atakua amechukua jukumu la polisi na mahakama at the same time? Na je kwa katazo hilo haoni kwamba atakua amezuia haki ya upande mwingine kupatikana?

Sidhani kama wabunge wamechukulia kwa uzito kauli zao na kuzipima na namna katiba inavyotaka au namna jamii inavyolichukulia swala zima la usawa mbele ya sheria?

Kwa uchache ni kuwa Bunge limeonesha ubinafsi wa hali ya juu, na kuzidi kutengeneza matabaka baada ya kuendelea kuwa kada inayopokea masarufu mengi na mazuri kuliko wengine.
 
Obstruction of justice kivipi?

Kafafanua vizuri. Anaweza kuwa amepanga kamati flani ikae kesho yake na ili hilo lifanyike, lazima quorum itimie. Ghafla bin vuu wanakutana na kushtuka mmoja hayupo. Kisa? Jana usiku Makonda au Sirro au any Dick aliagiza junior officers wamvizie Mbunge nje ya gate na kumkamata. Huhitaji degree kujua hili si sawa.

Yeye hazuii kukamatwa whether kwa tuhuma za jinai au madai. Anademand apewe info mapema. Ule ni Muhimili ati.
 
Hivi majuzi Mh. Spika alihitimisha mjadala wa muendelezo wa debate sehemu mbali mbali kuhusiana na vitwndo vya Polisi kuwakamata wabunge, kwa kutoa kauli kwamba, of is a yoyote anayemhitaji mbunge lazima amwambie!

Ingawa kwa macho ya wabunge wengi ni kauli sahihi, lakini Spika na wabunge wanasahau kwamba wabunge hawapo katika makundi ya watu wenye immunity ya kushtakiwa kutokana na makosa wanayoyafanya wakiwa wabunge kama kosa hilo halijafanyika ndani ya Bunge, ingawa Kuna utaratibu wa kumwajibisha mbunge kwa kosa atalolifanya akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge!

Kwakua basi wabunge wanastatus sawa kabisa na raia wengine wanapokua nje ya ukumbi wa Bunge sio vyema kuanza kutengeneza matabaka ya watu katika nchi hii tunayoishi wote.

Haiingii akilini kwanini mtu afanye kosa halafu itoke ruhusa ya Kumkamata au kutomkamata! Huko ni kupotoka na kuelewa madaraka tu tuliyowapa sisi kwa kura zetu wenyewe.

Katiba ya nchi haimuweki Mbunge juu ya sheria za nchi, wala haimpi mamlaka Spika ya kuzuia vyombo vya dola kufanya kazi yake pale inapotakiwa kufanya hivyo!

Ningependa kujua, agizo hilo la spika limetokana na sheria ipi na litakua na vigezo gani kwa spika kutoa ruhusa ya Mbunge kukamatwa!

Je, spika haoni kwamba ruhusa yake itakua imeprejudice court process!

Mfano akaletewa hati ya kukamatwa kwa mbunge! Akasema hapana asikamatwe! Haoni kwamba atakua amechukua jukumu la polisi na mahakama at the same time? Na je kwa katazo hilo haoni kwamba atakua amezuia haki ya upande mwingine kupatikana?

Sidhani kama wabunge wamechukulia kwa uzito kauli zao na kuzipima na namna katiba inavyotaka au namna jamii inavyolichukulia swala zima la usawa mbele ya sheria?

Kwa uchache ni kuwa Bunge limeonesha ubinafsi wa hali ya juu, na kuzidi kutengeneza matabaka baada ya kuendelea kuwa kada inayopokea masarufu mengi na mazuri kuliko wengine.
Kwahiyo wewe unaona ni sahihi Jengo la Bunge kufanywa kichochoro cha Polisi na bunduki zao kuwavizia wabunge??

Kama Polisi hawauogopi muhimili muhimu wa bunge ni vipi wanaweza kuheshimu haki ya raia wa kawaida huko Tandahimba??

Hebu jaribu kukivua cheo ulichojaliwa na uuvae uhusika wa mtuhumiwa wa makosa ambayo hayathibitishwa!!

Acha hizo
 
Loyers are layers swala la sheria hukinzana kwwnye tafsiri tu ndugai yuko sahihi sama vizuri kanuni za kudumu za bunge na sheria za mabunge ya jumuia za madola utamuelewa ndugai acha chuki soma vizuri sheria.
 
Wewe nawe umekurupuka.....Spika hajakataa wabunge wasikamatwe endapo wamefanya kosa....Spika yeye kasema kabla mbunge wake hajakamatwa ni lazima apewe taarifa....usikurupuke kama Yule KONDAKTA.
 
Kwahiyo wewe unaona ni sahihi Jengo la Bunge kufanywa kichochoro cha Polisi na bunduki zao kuwavizia wabunge??

Kama Polisi hawauogopi muhimili muhimu wa bunge ni vipi wanaweza kuheshimu haki ya raia wa kawaida huko Tandahimba??

Hebu jaribu kukivua cheo ulichojaliwa na uuvae uhusika wa mtuhumiwa wa makosa ambayo hayathibitishwa!!

Acha hizo
...Swali lingine je ikiwa polisi wanamuhitaji mtu ambaye kwa kipindi hicho yuko Ikulu kwenye kikao au for any other reasons, je polisi pia wanaweza kumvizia na bunduki zao pale geti la magogoni?
 
ni sawa na kumpa mtu mshamba aongoze kampuni yako. ametoka zake kuchunga ng'ombe huko, mshamba, unampa kampuni aongoze. kila kitu kimeharibika. hata hivyo, tunampongeza rais kwa hatua anazochukua.
 
watu walifanya makosa makubwa sana 2015, imetugarimu sana. watz huwa hatujifunzi kutokana na makosa. tatizo la makondakta akili yake na ya baba yake ni sawa, wote akili zao ziko vilevile hata wangekuwa wasomi namna gani. wanafaa kuwa wachunga ng'ombe. ndo maana hawajui kimombo.
 
Kwahiyo wewe unaona ni sahihi Jengo la Bunge kufanywa kichochoro cha Polisi na bunduki zao kuwavizia wabunge??

Kama Polisi hawauogopi muhimili muhimu wa bunge ni vipi wanaweza kuheshimu haki ya raia wa kawaida huko Tandahimba??

Hebu jaribu kukivua cheo ulichojaliwa na uuvae uhusika wa mtuhumiwa wa makosa ambayo hayathibitishwa!!

Acha hizo
Kwahiyo wafanye makosa tu kadri wanavyoweza kwakua Spika yupo atawakingia kifua?

Mkuu inamaana huoni namna tunavyotengeneza matabaka hapa? Kwamba wengi e wanakamatwa tu na wengine mpaka ruhusa itoke kwa mtu flani?

What happened to Article 13 ya CURT of 1977?
 
apewe taarifa . ..hajakataza kukamatwa
Mkuu naomba ufafanuzi! Taarifa ili afanyaje baada ya hiyo Taarifa? Kama ni swala la taarifa! Anaweza akapewa hata baada ya mtuhumiwa kukamatwa!

Yeye anataka taarifa kabla, huoni hili linatengeneza mlolongo wa upatikanaji wa haki na utekelezaji wa amri halali kisheria?
 
Wa tz wengi elimu ndogo sana! Jamaa kaandika mistari mingi bila utafiti wowote yani hovyo kabisa
 
Mkuu naomba ufafanuzi! Taarifa ili afanyaje baada ya hiyo Taarifa? Kama ni swala la taarifa! Anaweza akapewa hata baada ya mtuhumiwa kukamatwa!

Yeye anataka taarifa kabla, huoni hili linatengeneza mlolongo wa upatikanaji wa haki na utekelezaji wa amri halali kisheria?
hapana....kuna ugumu gani kutoa taarifa ofisi ya spika iko wazi...hakuna mlolongo...watoe tu taarifa ajue anapanga vipi kazi zake...
 
Back
Top Bottom