Zanzibar 2020 Maalim Seif: Wazee watalipiwa daladala na serikali

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Mgombea urais Zanzibar kupitia ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharrif Hamad amesema katika uongozi wa serikali watajali makundi maalum ambayo ni wanawake, watoto, wazee, walemavu na walioathirika na UKIMWI na dawa za kulevya.

Kwa wanawake amesema watahakikisha wanawake hawabaguliwi kwenye masuala ya kazi, hivyo watahakikisha uwiano makazini na kupinga udhalilishaji wa aina zote. Kwa watoto amesema watahakikisha wanapata lishe.

Pia amesema wazee wana mchango mkubwa katika nchi hiyo. Hivyo atafanya kila mzee anapata Tsh laki moja kwa mwezi na kupewa bima za afya. Pia wazee wenye miaka zaidi ya 65 wazee watalipiwa nauli ya daladala na serikali.

Aidha kwa walemavu amesema kila jengo la Zanzibar litakuwa na mazingira rafiki kwa walemavu kuweza kuitumia. Pia kwenye ajira walemavu hawatabaguliwa. Pia watazuia dawa za kulevya zisiingie Zanzibar ili kuwaepusha vijana na uraibu.
 
Mafuta siyo kusema utaenda na mtungi ama ndoo kisimani huko Mkunazini uchote! Mafuta ni mchakato wa kifedha na kiteknolojia kuyapata, kuyakusanya, kuyatunza na kisha kuyasafirisha tayari kwa mauzo!

Niongeze sauti!?
Alishasema hilo sana,alipokuwa makamu wa rais walishasaini mkataba na shell na uchumbaji unaanza ,amini "sheli" wanahela na vifaa vyakutosha
 
Alishasema hilo sana,alipokuwa makamu wa rais walishasaini mkataba na shell na uchumbaji unaanza ,amini "sheli" wanahela na vifaa vyakutosha
Kwa hiyo "Sheli" ni manamba wa Maalim Seif. Atawatumia anavyotaka kwa kuchota pesa kwenye akaunti za benk za hao Sheli kisha atawagawia Wazee wa kitanzania wanaoishi Zanzibaŕ ! Mkuu, tupe ufafanuzi wakina juu ya hili!
 
Znz kuna dalili za wazi za vurugu mwaka huu

Kitendo cha Seif kusema watu wote wakapige kura tarehe 27 then wapige tena tarehe 28 ni kulazimisha vurugu

Kitendo cha kusema hata wakala mmoja akinyimwa fomu basi kinuke ni ugaidi huu
 
Back
Top Bottom