Maalim Seif vs CCM sita

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,306
25,929
Wakati jitihada za kutafuta suluhisho la mgogoro wa kisiasa Zanzibar zikiendelea,vikao vinavyoendelea baina ya CCM na CUF havina uwiano wa uwakilishi;makada sita wa CCM dhidi ya Maalim Seif Sharrif Hamad wa CUF. Pande hizo zimeunda Kamati Maalum inayoongozwa na Rais wa Zanzibar, Dr. Ali Mohamed Shein lakini inakosa uwiano wa uwakilishi.

Mbali na Dr. Shein, wengine walio kwenye kamati hiyo ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, Rais wa Awamu ya Pili ya Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Serikali ya awamu ya nne, Jakaya Kikwete na Marais wastaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume na Dr. Salmin Amour. CUF inawakilishwa na Katibu Mkuu wake Maalim Seif ambaye ndiye aliyegombea Urais wa Zanzibar.


Kamati husika imeshaanza vikao vyake.

Chanzo: Mwananchi la 29/12/2015, uk. 4
 
siku kama hizi , itafikia kipindi tuzikumbuke, hasa kwa wale wenzangu na mie wakazi wa kilimani, kiwengwa, bububu , mwanakwelekwe, daraja bovu, kisonge kwa kina cholo, bila kusahau darajani na malindi.
 
Nawashangaa sana hawa ccm wakishidwa kwako ni kosa turudi mfumo dume chama kimoja
Yaani hakika hawa CCM kwenye chama chao hakuna msamiati unaoitwa kushindwa kwenye uchaguzi.
Msamiati pekee wanaoujua wao ni kushinda kwenye chaguzi zote hata kama ikibidi walazimishe goli la mkono, kama ambavyo hao CCM wa Zanzibar wanavyotaka kufanya kwenye marudio ya uchaguzi.
Yote hayo wanayalazimisha kwa sababu tu kuwa kwenye uchaguzi uliofanyika tarehe 25/10/2015 Maalim Seif alimbwaga Dr Shein kwenye kinyang'anyiro cha Urais!
 
Wanajua wakiruhusu kuwepo kwa uwiano sawa katika idadi ya wajumbe, basi ni dhahiri ya kwamba, Ismail Jussa atakuwa miongoni mwao na hivyo malengo ya CCM kutotimia.
 
Tatizo la CCM wanaogopa yale waliyowatendea upinzani na wao watatendewa.
 
Kwanini huyu MW. Seif anapenda kuingia kwenye hii mikutano pekee, kwani CUF haina watu? Au naye pia ana njama zake?
 
Maalim seif ameambatana na Mungu , hayupo peke yake , nakuomba maalim usithubutu kulipa kisasi baada ya kuapishwa .
 
Back
Top Bottom