koyola
JF-Expert Member
- May 20, 2015
- 2,644
- 1,748
Kukiwa bado kuna sintofahamu juu ya uchaguzi uliofutwa Zanzibar, Mgombea wa urais kupitia CUF Maalim Seif Hamad, amesema amekua akiandaa baraza la mawaziri ili mara tu akiapishwa aanze kuwatumikia wanzazibari.
Seif amesema hayo jana katika ofisi za CUF alipokua anaongea na wanachama wa chama hicho. Seif amesema katika baraza lake la mawaziri atawajumuisha na wana CCM kama ilivyoainishwa katika marekebisho ya katiba ya Zanzibar juu ya uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa.
Amesema yy ndio mshindi halali na anachosubiri kuapishwa tu, Seif pia amewataka wanachama wake kupuuzia propaganda za wana CCM za marudio ya uchaguzi huo.
Source: The Citizen
Haya maalim kila la heri