Maalim Seif: Mimi ndio Rais wenu

Maalim Seif: Mimi ndio Rais wenu

Kukiwa bado kuna sintofahamu juu ya uchaguzi uliofutwa Zanzibar, Mgombea wa urais kupitia CUF Maalim Seif Hamad, amesema amekua akiandaa baraza la mawaziri ili mara tu akiapishwa aanze kuwatumikia wanzazibari.

Seif amesema hayo jana katika ofisi za CUF alipokua anaongea na wanachama wa chama hicho. Seif amesema katika baraza lake la mawaziri atawajumuisha na wana CCM kama ilivyoainishwa katika marekebisho ya katiba ya Zanzibar juu ya uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa.

Amesema yy ndio mshindi halali na anachosubiri kuapishwa tu, Seif pia amewataka wanachama wake kupuuzia propaganda za wana CCM za marudio ya uchaguzi huo.

Source: The Citizen

Haya maalim kila la heri
 
Asubiri kupanda mahakamani tu na washenga wake wa ZEC wenziwe wapo kimya wanakusanya ushahidi yeye anachachawa tu..kweli za mwizi arobaini mwaka huu wamemkamata pabaya
 
Maalim Seif alijiandaa vizuri si kama UKAWA wameshindwa hata kulipa mawakala posho,wanadai wameshinda ukiwaambia walete matokeo waliyokusanya wanakimbia kimbia kama ndama hawakujipanga kuanzia mgombea uRais,wagombea ubunge na madiwani.

Utashangaa chama kinachopata ruzuku kubwa kimeshindwa kwa miaka mitano kutenge fungu la kuwalipa mawakala posho na chakula,wameshndwa kuandaa bajeti ya kundesha kampeni za uchaguzi hadi wategemee mgombea wa kukodi kutoka CCM awaletee fedha.

He is far better than UKAWA bara.
 
Kaa chini na ujiulize kwa nini uchaguzi urudiwe...?

Toa sababu za kisheria tafadhali...

Maalim kwa nn aogope kurudia Uchaguzi wakati wapiga kura ni wale wale kama walimpigia kura si watampigia tena? Maalim ni mvunja Muungano kwa Maslahi mapana ya Taifa letu tushirikieni kuilinda Znz kuangukia kwny Mikono ya Adui
 
Kaa chini na ujiulize kwa nini uchaguzi urudiwe...?

Toa sababu za kisheria tafadhali...

Kabla ya kutoa Amri ya kumkalisha mtu chini jiulize kasimama au kalala huyo mtu? Otherwise utaonekana hamnazo? Kisheria Mwnykt wa ZEC anapaswa kutangaza matokeo ya uchaguzi yaliyo ya haki na huru? Kama uchaguzi umejiridhisha kwa viashiria vyote umejaa kila aina ya dhulma, wizi, uvunjifu wa Taratibu utaacha kuufuta kwa sababu tu hakuna sheria inayoruhusu kuufuta? Ungekuwa wewe ndi Jecha ungemtangaza mshindi hata kama kuna viashiria vya hujuma kwa kuwa tu hakuna kifungu hicho? Mzee Karume kama angesubiri kifungu cha katiba 1964 mpaka keo hii znz ingekuwa wapi?
 
Kama ingekuwa ni mtihani basi umefeli...

Katika nukuu yako sijaona jibu lolote la kisheria...

Kabla ya kutoa Amri ya kumkalisha mtu chini jiulize kasimama au kalala huyo mtu? Otherwise utaonekana hamnazo? Kisheria Mwnykt wa ZEC anapaswa kutangaza matokeo ya uchaguzi yaliyo ya haki na huru? Kama uchaguzi umejiridhisha kwa viashiria vyote umejaa kila aina ya dhulma, wizi, uvunjifu wa Taratibu utaacha kuufuta kwa sababu tu hakuna sheria inayoruhusu kuufuta? Ungekuwa wewe ndi Jecha ungemtangaza mshindi hata kama kuna viashiria vya hujuma kwa kuwa tu hakuna kifungu hicho? Mzee Karume kama angesubiri kifungu cha katiba 1964 mpaka keo hii znz ingekuwa wapi?
 
Kama ingekuwa ni mtihani basi umefeli...

Katika nukuu yako sijaona jibu lolote la kisheria...

Wanasema sheria ipo kimya juu ya suala hili.....hakuna kifungu kinachomzuia ama kuruhusu yale ambayo Jecha ameyafanya.......
 
Maalim kwa nn aogope kurudia Uchaguzi wakati wapiga kura ni wale wale kama walimpigia kura si watampigia tena? Maalim ni mvunja Muungano kwa Maslahi mapana ya Taifa letu tushirikieni kuilinda Znz kuangukia kwny Mikono ya Adui

adui gani mkuu?????
 
Wanasema sheria ipo kimya juu ya suala hili.....hakuna kifungu kinachomzuia ama kuruhusu yale ambayo Jecha ameyafanya.......

Afadhali mkuu umejibu sawa sawia...
 
Kama ingekuwa ni mtihani basi umefeli...

Katika nukuu yako sijaona jibu lolote la kisheria...

Kufeli au kufaulu kunategemea Marking scheme sio ukweli wa Jambo hilo. Kama Marching scheme imetengenezwa na Mpumbavu unategemea Mwerevu atafaulu? Galileo alinyongwa kwa kusisitiza Dunia ni Duara wakati "Marking scheme" zilionesha ni pembe nne, akina Faradays na Isack Newton walipimwa kwa Mitihani feki. Nikuulize swali kati ya Katiba na Public Interest vinapokinzana kipi kina paswa ku prevail? Nilikutolea mfano wa Maamuzi ya wa Znz Jan 12 1964 walitumia katiba au maslah ya wa znZ lakin hujaelewa?
 
Mkuu maneno mengi ya nini?

Nimekuuliza na nimekuomba jibu lako lizingatie sheria na ungetumia katiba kama 'marking scheme' lakini umeshindwa kufanya hivyo...

Ungenukuu sheria inataja ni sababu zipi zenye kufanya uchaguzi mzima uwe batili, nani ana mamlaka ya kufuta uchaguzi n.k

Sasa kama kwako katiba na sheria ya uchaguzi ni 'marking scheme' iliyotungwa na wapumbavu basi sawa...

Lakini swali dogo unaanza kulipigia stori...

Adios

Kufeli au kufaulu kunategemea Marking scheme sio ukweli wa Jambo hilo. Kama Marching scheme imetengenezwa na Mpumbavu unategemea Mwerevu atafaulu? Galileo alinyongwa kwa kusisitiza Dunia ni Duara wakati "Marking scheme" zilionesha ni pembe nne, akina Faradays na Isack Newton walipimwa kwa Mitihani feki. Nikuulize swali kati ya Katiba na Public Interest vinapokinzana kipi kina paswa ku prevail? Nilikutolea mfano wa Maamuzi ya wa Znz Jan 12 1964 walitumia katiba au maslah ya wa znZ lakin hujaelewa?
 
Maalim kwa nn aogope kurudia Uchaguzi wakati wapiga kura ni wale wale kama walimpigia kura si watampigia tena? Maalim ni mvunja Muungano kwa Maslahi mapana ya Taifa letu tushirikieni kuilinda Znz kuangukia kwny Mikono ya Adui

Kwa nini arudie wakati kashinda? kumbe unataka apokwe ushindi kwa hofu kuwa atavunja muungano?

Kumbe demokrasi zanziber ni kiini macho tu. Ni bora mfumo wa vyama vingi ufutwe tubaki na chama kimoja tu.
 
Maalim kwa nn aogope kurudia Uchaguzi wakati wapiga kura ni wale wale kama walimpigia kura si watampigia tena? Maalim ni mvunja Muungano kwa Maslahi mapana ya Taifa letu tushirikieni kuilinda Znz kuangukia kwny Mikono ya Adui

Kila mpinzani ni adui...kwi kwi kwi.asokubali kushindwa.......Hivi rais wetu kachaguliwa na bara au visiwani???Muungano tena????
 
Japo wengine walitaka kuliahirisha hili tatizo ili lionekane ni la awamu ya tano lakini historia itasoma wazi palipokuwa na udhaifu!

Dr. Shein ni Rais wa awamu ya 7, awamu ya Tano ilikuwa ya Dr.Salmeen. Kura kuibiana wameibiana wazanzibari wenyewe, kupigana wamepigana wenyewe, kufuta wamefuta wenyewe msihamishie matatizo yenu huku!! Mkisaidiwa kutawaliwa hamtaki, mkiachwa kujitawala mnapigana, mnafuta matokeo, mnajitangazia ushindi n.k!!! Jk aliwasaidia kuwapatanisha mpaka mkaunda serikal ya mseto mluvyopatana mkajifanya eti mmesuluhishana wenyewe kupitia Nassoro Moyo, Karume na Seif sasa hili linawashinda kitu gani? Zanzibar igeuzwe Halmashauri tu iongozwe na DED iwe chini ya Tamisemi tumalize huu uroho wa Madaraka
 
Kwa nini arudie wakati kashinda? kumbe unataka apokwe ushindi kwa hofu kuwa atavunja muungano?

Kumbe demokrasi zanziber ni kiini macho tu. Ni bora mfumo wa vyama vingi ufutwe tubaki na chama kimoja tu.

Afadhali umejibu ukweli kwa sababu mtu unaenda kwenye uchaguzi na watu waliokwisha panga matokeo useless kabisa.
 
Tume ikibadilika badilika itazidi kuonyesha uchaguzi hauna uhalali
 
Dr. Shein ni Rais wa awamu ya 7, awamu ya Tano ilikuwa ya Dr.Salmeen. Kura kuibiana wameibiana wazanzibari wenyewe, kupigana wamepigana wenyewe, kufuta wamefuta wenyewe msihamishie matatizo yenu huku!! Mkisaidiwa kutawaliwa hamtaki, mkiachwa kujitawala mnapigana, mnafuta matokeo, mnajitangazia ushindi n.k!!! Jk aliwasaidia kuwapatanisha mpaka mkaunda serikal ya mseto mluvyopatana mkajifanya eti mmesuluhishana wenyewe kupitia Nassoro Moyo, Karume na Seif sasa hili linawashinda kitu gani? Zanzibar igeuzwe Halmashauri tu iongozwe na DED iwe chini ya Tamisemi tumalize huu uroho wa Madaraka


Uroho wa Madaraka ni wa wanaCCM na ndiyo umetufikisha hapa .............. Kama wataendelea na hii tabia basi tuna hari mbaya sana huko mbeleni!!
 
Uroho wa Madaraka ni wa wanaCCM na ndiyo umetufikisha hapa .............. Kama wataendelea na hii tabia basi tuna hari mbaya sana huko mbeleni!!

"Asiejipenda afanye fujo, Mie ndie Amiri jeshi Mkuu hakuna Mnywa kiroba wala mfadhili wa kiroba atakaemtisha wala kumbughudhi Mpiga kura yoyote nakuhakikishieni Uchaguzi utakuwa wa Salama salmeen"-Mzee Jakaya tarehe 23-24 October, 2015 Dsm na Mwanza.
 
kilichofanyika zanzibar kimetuonyesha kwamba hstukuwa tayar kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi....
 
Back
Top Bottom