Uhakika ni kuwa CCM na Tume ZEC katika mzunguko huu iliokwisha wameshindwa kufunga goli la mkono (Maradona style) na ndio sababu wanataka uchaguzi urudiwe. Huu uliopo si mgogoro, ni uhuni tu na ung'ang'anizi wa madaraka wa CCM.Jamani tupeane taarifa za uhakika! Ila tuwe na subira juu ya mgogoro huu!
Upo uzi wa dada Faiza nimeona kule kuna mchangiaji ameweka vivuli vya matokeo na zile fomu za matokeo zilizosainiwa na mawakala wa vyama na masimamizi wa kituo .
Wakati CCM bara (NEC) wanasema uchaguzi umekwisha, tusonge mbele. CCM Zanzibar wamekusudia kutumia kila mbinu chafu ili na wao watangazwe "mshindi".