Maalim Seif kutumbua nyongo kesho

Maalim Seif kutumbua nyongo kesho

Tamko hilo alipeleke Zanzibar aache ubabaishaji huku bara

Wakuu msichoke , haya mambo ya Zanzibar kiukweli hayajaisha , ndio kwanza yanaanza .

Taarifa mpya zilizonakiliwa kwenye gazeti la Mwananchi zinaeleza kwamba Shujaa Maalim Seif atazungumza na dunia kesho tarehe 10 / 4 ambapo atapata nafasi ya kuweka wazi mustakabali wake kisiasa .

Mwamba huyo wa siasa za nchi hii ambaye sasa dunia nzima inamtambua na kumkubali ataelezea mikakati , mipango na mwelekeo wa chama chake cha CUF katika siasa za Zanzibar .

Kila la heri Maalim Mungu akulinde .

====================

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharrif Hamad kesho ataelezea mwelekeo wake kisiasa, ikiwamo kufafanua kiundani uamuzi wa chama hicho kususia uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, mwaka huu.


Mgombea huyo wa urais Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana ataeleza mambo hayo ikiwa imepita takribani wiki moja tangu Baraza Kuu la chama hicho kutoa msimamo wake wa kutomtambua Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein pamoja na wawakilishi na madiwani.

CUF kilisusia kushiriki uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20 mwaka huu baada ya Oktoba 28 mwaka jana, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya urais, uwakilishi na udiwani, akisema kulikuwapo na ukiukwaji wa sheria na kanuni za uchaguzi.

Habari kutoka ndani ya chama hicho zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa mkutano wa kiongozi huyo utakuwa wa kwanza kwake, tangu kumalizika kwa uchaguzi wa marudio na ataeleza mambo muhimu yatakayotoa picha halisi ya mwelekeo wake na CUF.

“Katika mkutano uliopita tamko lilikuwa la Baraza Kuu ila keshokutwa (kesho) Maalim Seif atazungumza kama Katibu Mkuu na aliyekuwa mgombea urais. Kuna masuala mengi atayaeleza kwa kina, hasa hili la uamuzi wa CUF kususia uchaguzi,” zilieleza taarifa hizo.

“Atazungumzia kwa kina uchaguzi ulivyokuwa na kujibu maswali ya watu wa kada mbalimbali waliokuwa wakihoji nini hatima ya CUF, baada ya kususia uchaguzi na hivyo kupoteza nafasi za uwakilishi.”


Chanzo: Mwananchi.
 
Kama uchaguzi wa Oct 2015 yeye ndo mshindi na ndo uchaguzi halali machoni pa waangalizi wa kimataifa ni vyema atangaze serikali yake kamili then negociation ianzie hapo. Cuf ikikaa kimya imefutwa rasmi na haya majizi ya mchana
 
Ingekuwa enzi za Mzoga Tungekuwa kwny vurugu za Maandamano lakin kwa huyu msukuma ni no
 
Wakuu msichoke , haya mambo ya Zanzibar kiukweli hayajaisha , ndio kwanza yanaanza .

Taarifa mpya zilizonakiliwa kwenye gazeti la Mwananchi zinaeleza kwamba Shujaa Maalim Seif atazungumza na dunia kesho tarehe 10 / 4 ambapo atapata nafasi ya kuweka wazi mustakabali wake kisiasa .

Mwamba huyo wa siasa za nchi hii ambaye sasa dunia nzima inamtambua na kumkubali ataelezea mikakati , mipango na mwelekeo wa chama chake cha CUF katika siasa za Zanzibar .

Kila la heri Maalim Mungu akulinde .

====================

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharrif Hamad kesho ataelezea mwelekeo wake kisiasa, ikiwamo kufafanua kiundani uamuzi wa chama hicho kususia uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, mwaka huu.


Mgombea huyo wa urais Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana ataeleza mambo hayo ikiwa imepita takribani wiki moja tangu Baraza Kuu la chama hicho kutoa msimamo wake wa kutomtambua Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein pamoja na wawakilishi na madiwani.

CUF kilisusia kushiriki uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20 mwaka huu baada ya Oktoba 28 mwaka jana, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya urais, uwakilishi na udiwani, akisema kulikuwapo na ukiukwaji wa sheria na kanuni za uchaguzi.

Habari kutoka ndani ya chama hicho zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa mkutano wa kiongozi huyo utakuwa wa kwanza kwake, tangu kumalizika kwa uchaguzi wa marudio na ataeleza mambo muhimu yatakayotoa picha halisi ya mwelekeo wake na CUF.

“Katika mkutano uliopita tamko lilikuwa la Baraza Kuu ila keshokutwa (kesho) Maalim Seif atazungumza kama Katibu Mkuu na aliyekuwa mgombea urais. Kuna masuala mengi atayaeleza kwa kina, hasa hili la uamuzi wa CUF kususia uchaguzi,” zilieleza taarifa hizo.

“Atazungumzia kwa kina uchaguzi ulivyokuwa na kujibu maswali ya watu wa kada mbalimbali waliokuwa wakihoji nini hatima ya CUF, baada ya kususia uchaguzi na hivyo kupoteza nafasi za uwakilishi.”


Chanzo: Mwananchi.
Seif amewapotosha wafuasi wa cuf kwa mkakati wake dhaifu wa kususia uchaguzi. cuf nje ya baraza la wawakilishi na serikali haina maana. Mkakati wa kutomtambua Shein na serikali yake hakika hauna maana. SMZ inatambuliwa na SMT na hiyo inatosha kabisa kwa SMZ kutekekeza majukumu na wajibu wake kwa wananchi wote wa zanzibar. Kutambuliwa SMT kimataifa inatosha.
 
kipi wanachotaka kukiongea wakati wao walisusa? unapokisusa kitu ina maana huna shida nacho! sasa hii mikutano ya kazi gani? wakae pembeni watuachie MAKAPUKU tuendelee na kutafuta maisha. Cuf ndio inapotea hivyo na kufutika
 
Dalili za mtu kupotea ni kama anavyofanya Maalim Seif.
 
Yaone ma lumumba fc na nyuso zao za ajabu watakavyokuja hapa na utumbo!
Serikali ya Zanzibar ipo Tayari kumyoa manyoya Kuku yoyote atakayeleta choko choko na kuhatarisha hali ya amani. hatuna mashaka na wala wasi wasi na Manyumbu..... Chama kichakavu kinahaha....Maalimu anawaza atawaambia nini Manyumbu aliyoyaongoza kususa na sasa wameanza kupata wakati mgumu kimaisha kwa wale waliopoteza majimbo....fani za kufanya kazi nyingine hawana....familia zao zimeanza kuhaha.... huku yeye Maalim akiendelea kula maisha na posho za uwaziri kiongozi na support ya kimaisha kutoka kwa mpwa wake F karume....... Hongera sana Dr Shein kwa kuwachagua Ali Karume na Hamad Rashid kwenye safu yako ya viongozi hawa ni hazina kubwa ya zanzibar na Tanzania....
 
Serikali ya Zanzibar ipo Tayari kumyoa manyoya Kuku yoyote atakayeleta choko choko na kuhatarisha hali ya amani. hatuna mashaka na wala wasi wasi na Manyumbu..... Chama kichakavu kinahaha....Maalimu anawaza atawaambia nini Manyumbu aliyoyaongoza kususa na sasa wameanza kupata wakati mgumu kimaisha kwa wale waliopoteza majimbo....fani za kufanya kazi nyingine hawana....familia zao zimeanza kuhaha.... huku yeye Maalim akiendelea kula maisha na posho za uwaziri kiongozi na support ya kimaisha kutoka kwa mpwa wake F karume....... Hongera sana Dr Shein kwa kuwachagua Ali Karume na Hamad Rashid kwenye safu yako ya viongozi hawa ni hazina kubwa ya zanzibar na Tanzania....
kumchezea mtu anayeungwa mkono na zaidi ya 95% ya wazanzibar ni kujiletea matatizo tu .
 
kipi wanachotaka kukiongea wakati wao walisusa? unapokisusa kitu ina maana huna shida nacho! sasa hii mikutano ya kazi gani? wakae pembeni watuachie MAKAPUKU tuendelee na kutafuta maisha. Cuf ndio inapotea hivyo na kufutika
anaongea seif lakini mapovu unatoa wewe !
 
Maalim anawadanganya wenzake na huku yeye anaendelea kula mafao.

Kimsingi yeye sasa hivi amegeuka kuwa burudani ya kuwaburudisha wana jf kwa maigizo ya matamko walio wajinga wanaendelea kuburudika.

Namshauri atafute namna nyingine na kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa 2020.

Kwasasa hawezi kuwa na matamko kwa serikali inayomtunza. Kama kweli hamtambui Dr. Shein akatae hata mafao yanayotolewa na serikali inayoingozwa na Shein maana kila anachokula kimetafutwa na serikali ya CCM asiyoitambua.

Chama gani kinachoongozwa bila mwenyekiti? Ndio maana kinapoteza mwelekeo CUF isipobadilika kesho tu itakuwa kama TLP.

HAPA DUNIANI, USIJIDANGANYE UKASEMA "BILA MIMI HAWAWEZI FANYA LOLOTE" UKASAHAU KUWA KUNA MAHALI PENGINE WANAFANYA BILA KUWEPO WEWE.

Pole sana Maalim!!!!!!!
 
kesho sasa anakuja mzee mwenyewe Maalim Seif ambaye utafiti unaonyesha kwamba anakubalika kwa 95% na wazanzibar , usikose tukio hili la kihistoria tangu kuumbwa kwa nchi hii .
Sema asilimia 95 ya wana CUF, sio Wazanzibari, She in mwenyewe amepata 91% ya wana CCM
 
IGP zuia huo mkutano wa Seif au na wewe huwezi kuingilia mambo ya Zenj aitwe Jecha?
 
Asipojitangaza raisi basi tamchukulia fal tena wa kiwango cha huu.
 
Ana hekma sana huyu Mzee. Kwa kweli Maalim amekamilika, busara, maono, subra, msimamo ulio thabiti. Ni mojawapo ya viongozi hadimu sana dhama hizi si Tanzania pekee bali duniani kwa jumla
 
Sema asilimia 95 ya wana CUF, sio Wazanzibari, She in mwenyewe amepata 91% ya wana CCM
taarifa zinaonyesha kwamba wazanzibar ambao ni wana ccm hawazidi 50,000 ndio maana shein alipata kura 48,752 .
 
Back
Top Bottom