Mabibi na mabwana si busara sana kuukimbia ukweli. Ukweli ni mchungu na msema kweli ni mpenzi wa Mungu.
Au nasema uongo ndugu zangu?
Kumekuwa na mengi kuhusu ACT na Maalim Seif hasa baada ya kujiunga SUK.
Ufuatao ndiyo ulio ukweli kuhusiana na jembe hili la Zanzibar.
Maalim Seif kaipigania Zanzibar maisha yake yote. Angali anapigana na ataendelea inshallah (mola apishilie mbali) hadi kifo kitakapo mtenga.
Kuipigania kwake Zanzibar ndipo kunakompa hii credibility au kupendwa aliko nako. Ni umaarufu huo ambao pia ndiyo iliyo sababu kuu ya yeye kuibiwa kura na mahasimu wake kila uchao.
Alipo Seif wapo!
Alikuwa CUF yuko ACT hata akienda TADEA au wapi watakuwa naye huko.
Zanzibar ni kipaumbele chake. Si Bara. "Mtu kwao" na "mcheza kwao hutunzwa."
Akiitisha Seif hata leo kule Zanzibar kitanuka. Tofauti kubwa sana ya kule na Bara. Huyu gwiji ana msingi uliojichimbia barabara chini ya ardhi.
Pana tofauti kubwa ya Maalim Seif kama binadamu na ACT kama chama. Huu nao ni ukweli mchungu. ACT ni chama imara ushukuriwe uwepo wa Maalim. ACT ni butu kama CUF bila Maalim. Profesa anaweza kuuthibitisha ukweli huu.
Maalim ni mpambanaji mzoefu. Huyu ana mbinu na uwezo wa mapambano kuliko majenerali wengi. Kumbeza Maalim ni kukosa kumtambua vyema wala kutambua agenda yake iliyokuu.
Kumhusisha Maalim na ukosefu wa haki kule Kagera au Rukwa ni kutojitendea haki sisi wenyewe.
Mambo ya Ngoswe huachiwa Ngoswe mwenyewe!
Kila mtu na apambane na hali yake. Maalim anapambania Zanzibar na anaowapigania wamempa ridhaa hiyo.
Kwenye hili si CCM wala awaye yote Bara anaweza kujidhania kashinda au kashindwa au hata kasalitiwa. Busara ni kukubali kutokubaliana.
Udumu Maalim Seif jembe la ukweli la Wazanzibari!
Au nasema uongo ndugu zangu?
Kumekuwa na mengi kuhusu ACT na Maalim Seif hasa baada ya kujiunga SUK.
Ufuatao ndiyo ulio ukweli kuhusiana na jembe hili la Zanzibar.
Maalim Seif kaipigania Zanzibar maisha yake yote. Angali anapigana na ataendelea inshallah (mola apishilie mbali) hadi kifo kitakapo mtenga.
Kuipigania kwake Zanzibar ndipo kunakompa hii credibility au kupendwa aliko nako. Ni umaarufu huo ambao pia ndiyo iliyo sababu kuu ya yeye kuibiwa kura na mahasimu wake kila uchao.
Alipo Seif wapo!
Alikuwa CUF yuko ACT hata akienda TADEA au wapi watakuwa naye huko.
Zanzibar ni kipaumbele chake. Si Bara. "Mtu kwao" na "mcheza kwao hutunzwa."
Akiitisha Seif hata leo kule Zanzibar kitanuka. Tofauti kubwa sana ya kule na Bara. Huyu gwiji ana msingi uliojichimbia barabara chini ya ardhi.
Pana tofauti kubwa ya Maalim Seif kama binadamu na ACT kama chama. Huu nao ni ukweli mchungu. ACT ni chama imara ushukuriwe uwepo wa Maalim. ACT ni butu kama CUF bila Maalim. Profesa anaweza kuuthibitisha ukweli huu.
Maalim ni mpambanaji mzoefu. Huyu ana mbinu na uwezo wa mapambano kuliko majenerali wengi. Kumbeza Maalim ni kukosa kumtambua vyema wala kutambua agenda yake iliyokuu.
Kumhusisha Maalim na ukosefu wa haki kule Kagera au Rukwa ni kutojitendea haki sisi wenyewe.
Mambo ya Ngoswe huachiwa Ngoswe mwenyewe!
Kila mtu na apambane na hali yake. Maalim anapambania Zanzibar na anaowapigania wamempa ridhaa hiyo.
Kwenye hili si CCM wala awaye yote Bara anaweza kujidhania kashinda au kashindwa au hata kasalitiwa. Busara ni kukubali kutokubaliana.
Udumu Maalim Seif jembe la ukweli la Wazanzibari!