Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,607
- 46,245
Kwa maoni ya mtandaoni na mtaani wana CHQDEMA karibia wote wameridhia na kufurahishwa kufukuzwa uanachama kwa wabunge wake wanawake 19.
Kwa upande wa CCM asilia mtandaoni, ile iliyoshikilia usukani serikalini na kwenye chama kwa sasa iko nyutro na kimya. Haionekani kujishughulisha, kutatizwa au kuhangaishwa na CDM kuwafukuza kwenye chama chao waliokuwa wanachama wake.
Wanaolalamika, waliochukizwa na kukasirishwa na uamuzi huo ni MATAGA!. Wameandika nyuzi za kila aina kuwananga CDM na hususani Mbowe kwa maamuzi hayo. Wamewashauri wabunge hao kwenda mahakamani, wanawatetea hawajatendewa haki na mwishowe wanafurahi wabunge hao kuendelea kuingia bungeni na wanatamba kwa nyuzi kwamba hakuna kitu kitabadilika, wabunge hao wataendelea kuingia bungeni CDM ipende au isipinde.
Wengine wamefikia mbali zaidi kusema CDM imefanya uamuzi wa kipumbavu na itayumba au itajifia kwa kuwafukuza wanawake hao!
Kwa nini wanaonekana kuchukizwa zaidi na kufukuzwa kwa wanachama 19 wa CDM ni kundi la watu walio katika chama kingine na sio baadhi ya wana CDM ambao labda ingekuwa ni wafuasi wao? Wana maslahi gani nao?
Kwa upande wa CCM asilia mtandaoni, ile iliyoshikilia usukani serikalini na kwenye chama kwa sasa iko nyutro na kimya. Haionekani kujishughulisha, kutatizwa au kuhangaishwa na CDM kuwafukuza kwenye chama chao waliokuwa wanachama wake.
Wanaolalamika, waliochukizwa na kukasirishwa na uamuzi huo ni MATAGA!. Wameandika nyuzi za kila aina kuwananga CDM na hususani Mbowe kwa maamuzi hayo. Wamewashauri wabunge hao kwenda mahakamani, wanawatetea hawajatendewa haki na mwishowe wanafurahi wabunge hao kuendelea kuingia bungeni na wanatamba kwa nyuzi kwamba hakuna kitu kitabadilika, wabunge hao wataendelea kuingia bungeni CDM ipende au isipinde.
Wengine wamefikia mbali zaidi kusema CDM imefanya uamuzi wa kipumbavu na itayumba au itajifia kwa kuwafukuza wanawake hao!
Kwa nini wanaonekana kuchukizwa zaidi na kufukuzwa kwa wanachama 19 wa CDM ni kundi la watu walio katika chama kingine na sio baadhi ya wana CDM ambao labda ingekuwa ni wafuasi wao? Wana maslahi gani nao?