Maajabu: Rais Juzi - Mimi sipangiwi cha kufanya. Leo - Nyie kwanini mnamwandika yule mnaniacha mimi?

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Hivi jaman huyu ni rais kweli au Mungu katupa adhabu kama wana wa Israel kuteseka jangwani.

Hivi si huyu alisema hapangiwi cha kufanya kwanini awapangie wahariri wa vyombo vya habari waandike nini?
Nachojua kuna magazeti, tv na redio za chama na serikali ndo vinawajibika kweke.

Inakuwaje awapangie na wa vyombo binafsi wakati hata matangazo siku hizi hawapi? Kwanini anapenda kula kuliwa hataki?

Kashasema biashara zote zifanywe na vyombo vya serikali sasa mbona vinamuuma sana?

Hivi huyu ni msukuma au naye sio mwanakwetu.

Kama kila mtu anamamlaka yake wahariri wanaandika kile soko linataka sio serikali inataka na hakuna sheria waliovunja kuandika yale.

Na kukwambia Mwakyembe yasijirudie tena nini maana yake? Kuwa kabla ya kuchapisha au kurushwa inabidi waziri ahakiki habari au???

Na ITV kuonyesha migogoro ya wakulima na wafugaji inakukera we vipi???? Kama umeshindwa kutatua tuachie nchi yetu, inakukera kwa sababu umeshindwa. Na hii kufungwa kwa waandishi na kupigwa naona inatokea kwako amri sio bure.



Ukweli ndo huu


CCM na Serikali ya JPM wamebaki kama Yatima! Soma hizi Leading Story za magazeti ya leo...

GROUP A
1. DAILY NEWS: Sand container retained at Dar port (Kontena la mchanga lazuia bandari ya Dar)

2. UHURU: Udanganyifu (Bandarini.. na picha ya makontena yamefunguliwa)

3. HABARI LEO: JPM atinga tena bandarini Dar

GROUP B
1. NIPASHE: Mwendo wa [HASHTAG]#Bastola[/HASHTAG] Tu! Nape atishiwa kupigwa risasi ili asizungumze na waandishi.

2. MTANZANIA: Hata Nape!! Mkutano wake wavunjwa na Polisi, atishiwa na Bastola. Awataka Vijana wasiwe na woga, wapiganie wanachokiamini. Akumbusha alishawahi kufukuzwa CCM.

3. MWANANCHI: Kishindo cha Nape! Taarifa ya kukutana na waandishi saa chache baada ya kuondolewa uwaziri ziliwachanganya Polisi; lakini jitihada zao za kumzuia asiseme zilikwama. (Picha tatu: hii ndiyo bastola aliyolalamika kutishiwa)

4. MAJIRA: Nape Atikisa! Uteuzi wake watenguliwa, azuiwa kuzungumza na waandishi hotelini; atolewa [HASHTAG]#Bastola[/HASHTAG], atema cheche.
Michezoni- [HASHTAG]#Bastola[/HASHTAG] yankimbiza Harmorapa sakata la Nape.

5. JAMBO LEO: Nape anyooshewa [HASHTAG]#Bastola[/HASHTAG] hadharani, saa chache baada ya kuvuliwa uwaziri; atema Cheche.

6. THE CITIZEN: Nape's parting shot

7. THE GUARDIAN: Nape - A seed must die to live (Nape : Mbegu lazima ife ili iote)
______

Group B angalau wameripoti ziara ya Bandarini kwa maandishi madogo sana pembeni, sio stori inayouza. Group A hawajagusia kabisa vurumai ya kumzuia Nape kusema. Hawawezi jihukumu!

Nadhani kwa tulipofika, utengano utaendelea kuwa dhahiri zaidi..
 
Kama vyombo vya habari vimesajiliwa kisheria na vinalipa kodi visipangiwe vitu vya kuandika,pesa zao ,wafanyakazi wao na mitambo yao hawakusindikizwa kununua wala kusajili waachwe waandike wanachoona kinauza ili mradi hawavunji sheria za nchi
 
Shule nisome mwenyewe.
Ada nilipe mwenyewe.
Kazi nitafute mwenyewe.
Leo unipangie cha kuandika?
3c31d4fc2eae96e72fea34fb9f7c33e6.jpg
 
Back
Top Bottom