Maadui wa Watanzania: Aongezeka mmoja

Maadui wa Watanzania: Aongezeka mmoja

Yaani adui CCM ni chimbuko au mama wa maudui wengine!ukiua kizalia,itakuwa rahisi kumaliza maadui watoto waliosalia!CCM ni janga kubwa sana kwa taifa la tanzania!
 
Yaani CCM ni adui mbaya kabisa kwani ndiye anayeleta ujinga, maradhi na hali ngumu ya maisha.
Inatudanganya kama watoto. Watu wanaumwa, badala ya kuwapa dawa imewaletea babu wa loliondo na shehe yahaya
 
Adui aliyeongezeka ni RUSHWA. Lakini mimi siamini kama UJINGA bado ni adui kwa jamii ya Watanzania wa leo; kuna watoto wadogo hivi leo kukwea pipa mpaka China na elimu yao ya Std VII ni kawaida bado utawaita hao ni wajinga?

Kwa maoni yangu maadui waliobaki ni
1) RUSHWA
2) UMASKINI (unaosababishwa na namba moja)
3) MARADHI (yanayosababishwa na namba 2)

Tukiangamiza RUSHWA tutakuwa na rasilimali za kutosha kukabili UMASKINI wa Watanzania na hivyo kuwajengea uwezo wa kuangamiza MARADHI

Maadui wote wameweka mizizi yao kwenye ujinga.
RUSHWA inadaiwa na kutolewa kwa sababu ya kutojua haki na stahili za raia wanaohitaji huduma.
UMASKINI unatokana na kutegemea viongozi wasiojua wanalolifanya, uwezo wao wa kufikiri ni kama chifu mangungo pamoja na kwamba tunawaita wasomi.
MARADHI yanasababishwa na mipango mibovu, maamuzi mabovu kama kuomba misaada ya chandarua badala ya kuangamiza msalia ya mbu n.k
Maliasili na rasilimali zetu zinaporwa na wageni huku viongozi na vyombo vya usalama vikiwalinda na kufanikisha uporaji kwa sababu ya ujinga tu wakisingizia uwekezaji.
Wananchi wanakula mapanki huku minofu ikipelekwa ulaya, kwa sababu ya ujinga wanaandamana kuilinda hali hiyo!

Hata hivyo, usijaribu kulinganisha kupanda ndege kwenda China na kufuta ujinga kwani wajinga wengi wanapanda ndege kwenda kusaini mikataba ya kijinga, kufanya ukahaba, kununua madawa ya kulevya, kusafirisha watu kwa ajili ya kutumikishwa n.k.
 
Tumekua na raisi mwenye vision mmoja tu hapa bongo, Mwl Nyerere. Wengine hawa huwezi jua hata vision yao ya Tz iweje iko vipi. Hata maandishi ya kuelezea visions hizo hawana. Kwa mtizamo huo bado tunachukulia vision ya Mwl Nyerere na matatizo aliyoyaainisha ambayo kwa kipindi hicho ndio yaliunda timu ya maadui wa taifa. Lakini toka awamu ya pili iingie matatizo ama maadui wa taifa wameibuka wengi sana wengine wakiwa ni zao la mifumo ya uongozi uliofuata.
 
BILA ccm KUFA hatuwezi kushinda vita dhidi ya hawa maadui hata siku moja!
 
Wana JF

Kwa muda mrefu tumekuwa na maadui watatu yaani Ujinga, maradhi na umasikini na tumekuwa tukipambanao mimi kwa mtazamo wangu ni kuwa ameongezeka adui mwingine ambaye CCM nasema hivyo kwa sababu CCM haijui kwanini Tanzania ni masikini na kama hujui tatizo hilo la umaskini si rahisi kuwa na strategy ya kulitatua.

Na adui aliyeongezeka miezi ya karibuni ni ulalamishi wa Chadema.
 
Huyo adui namba 6, kaasisiwa na Baba Liz! Poor him!
 
kama tupo watu makini tanzania tutaiwajibisha ccm mwaka huu.zipo sababu nyingi za kufanya hivyo na kwa kutaja chache tu niseme tatizo la umeme tanzania ingeweza ikawa sababu ya kutosha kuwaambia ccm wapumzike kwa amani.haiwezekani nnchi ikawa na viwanda na ajira kama hakuna umeme wa uhakika na wa kutosha,kwa zaidi ya miaka 30 serikali ya ccm imeshindwa kabisa kumaliza tatizo la umeme.inashangaza kama kwa mfano kiwanda cha sukari moshi kinaweza kujizalishia umeme wake halafu serikali ikashindwa.aibu.tujiulize kama tukiwapa wapinzania dola ni mambo gani mabaya zaidi ya yale yaliyofanywa na ccm watayafanya?tuwapime wapinzani kwa miaka mitano siyo dhambi.
 
Unachekesha kweli kweli wewe, nikuulize magufuli anamiliki ilani? Utanijibu lkn nikwambie hivi kwa mujibu wa katiba ya nchi serikali inayoundwa ni ya chama dola. hatuchagui mtu tunachagua chama na hii ni baada ya chama kutuelezea sera zake ndipo tunachagua. sasa kila chama kina mifumo yake, misingi yake,kina tabia yake,kina utaratibu wake,kina mazoea yake,kina misimamo yake Hivyo kwa tabia za ccm hatukitaki tena kimezalisha maadui wengine watatu zaidi Rushwa,Ufisadi na mizaha. kwa hiyo sasa tuna maadui 6
1Ujinga
2Umaskini
3Maradhi
4Rushwa
5Ufisadi
6Mizaha

Ili taifa lisonge mbele,liondoke hapa lilipo kwama ni lazima ccm kife kiingie makumbusho kama KANU, leo kenya na rwanda zipo dunia ya 2 sisi bado tupo dunia ya 3 ujinga kabisa!

Ni kweli kabisa kwamba ni mizaha ya hali ya juu kwa watanzani. Mtu mwenye maradhi na homa ya kiharusi kugombea uraisi. Hiyo ni mizaha iliyopitilioza
 
Ni kweli kabisa kwamba ni mizaha ya hali ya juu kwa watanzani. Mtu mwenye maradhi na homa ya kiharusi kugombea uraisi. Hiyo ni mizaha iliyopitilioza

Kwa hali ilivyo nchini/kwa hapa tulipokwama kwa sababu ya ccm kwa dhati kabisa hatuihitaji tena ccm hata kama akija mzungu mwenye uwezo kwa kuondoa ccm kama lowasa sie tunampa kura

......Sijui kwanini hamuelewi tunasema hivi tumechoka kuendelea kuwa mateka wa ccm ..ccm kife kwanza mengine badae....hatuwezi kupiga fiesta tu kila wakati wa kampeni na kuzalisha rushwa na ufisadi tu kila siku..\


Ni lowasa tu kila kona ya nchi
 
Back
Top Bottom