M4C-OPD Ifakara; live coverage

M4C-OPD Ifakara; live coverage

"Siwezi kuachia Uongozi katikati ya Mapambano"

"Nina kesi 13,nimekoswa kuuawa mara 2 leo anatokea mtu anahongwa hela na Magamba anataka uenyekiti"

Asante Kamanda Mkuu Mbowe.

Watanzania tunakuunga mkono.
 
Hongereni wananchi wa Ifakara. Poleni kwa kazi kubwa makamanda Mbowe na wenzio. Tuko nanyi.

Hao wanaodai watu wako kazini saa hizi kwani wanadhani kinachofanyika hapo mkutanoni ni kitu gani? Ni kazi nzito ya kumtokomeza yule mwovu!
 
Mtu ambaye hajafunguliwa hata kesi moja anautaka uenyekiti kupitia Facebook...huku kakunja nne LOL!!!

sina sikia na yeye anataka kupima upepo kwa kuzunguka nchi nzima sasa sijui kwa chama gani,labda cha mizigo.
 
Kamanda Mboe alishaapa kuiangusha ccm na ndicho kinachoendelea sasa.

R.I.P CCM
 
tunakushukuru kwa wema wako wa kutushirikisha kwenye ukombozi .
 
Kamanda mkuu, Mh. Mbowe akiambatana na Mh. Halima Mdee na makamanda wengine wameshatua na kufika kiwanja cha Kiungani, Polisi mjini Ifakara.
Ufunguzi tayari kwa dua umeshafanyika na Makamanda mbalimbali wanazungumza...

CHAMA cha SIASA NI MABARABARANI NA MAJUKWAANI - JK NYERERE .
 
Mtu ambaye hajafunguliwa hata kesi moja anautaka uenyekiti kupitia Facebook...huku kakunja nne LOL!!!

hahaaa mbowe ana madongo sana ...hahaaaa Zitto na uenyekiti kutitia twitter na facebook....kazi ipo ...
 
Hakika, CHADEMA ni mpango wa Mungu!
Kamanda wa anga Mh.Mtu huru, Mbowe! akiwa Ifakara-Kilombero leo Asubuhi ametanabaisha kuwa!


1. Polisi walio husika kwenye Mlipuko wa arusha, katika mkutano wa CHADEMA viwanja vya soweto, walitoka Morogoro na wanajulikana. hivyo anasubiri tume huru ya kimahakama iundwe ili apelekeushahidi wake

2. Amelazimika kuhamishia watoto wake nje ya nchi baadaya kuwa wanawindwa kila sIku na watekaji wa CCM hapa tz, hivyo kubaki yeye tz iliikibidi hata kufa afe yeye ,kwakupigania watz.

3.Yeye kama amiri jeshi mkuu kwenye mapambano, asingependa kuona Chadema inabadilisha amiri jeshi mkuu kwa sasa kwani wako katikati ya mapabano!

4.Anakesi zaidi ya 13 ambazo anahudhuri mahakamani kutokana na harakati za Ukomboz kupitia CHADEMA, amekoswa koswa kuuawa mara nyingi halafu watokee watu wajinga wajinga ambao kwenye maadamano(ambapo amesema kuwa maandamano ni moja ya kazi yao kama chama cha Upinzani) hawashiriki, hawana kesi mahakamani, wanakula na kunywa na maCCM, eti wanataka uongozi CHADEMA, kwa kazi gani? hayuko tayari kutoka madarakani mpaka kieleweke!

5.Kwasasa hakuna kazi iliyo nyepesi na rahisi kama kupambana na CCM, Kwani Mungu amewapiga upofu watawala hawaoni shida za wananchi

6. M4C-PMOJA DAIMA ni kwaajili ya kuwaunganisha wananchi wote bila kujali itikadi yao, kidini, kisiasa n.k

7.Kuunganisha viongozi wa vyama vya vyaupizani haiwezekani, kwani wengi ni Mawakala wa CCM, hivyo CHADEMA kupitia OPD imeaumua kuunganisha wananchi na siyo viongozi wa upinzani.
8. 2015 CHADEMA inaingia Ikulu kwa kishindo.

9.CCM wamebakiza nguvu mbili 2 za kuwalinda, dola na sheria Kandamizi

10.Kwa sasa CCM ni ya watu wachache tu, ndiyo wenye chama! wengine wote ni dampo tu.

Hakika kwa umati wa maerufu ya watu waliojitokeza leo Ifakara, CCM mtaisoma namba! CHADEMA ndiyo habari ya Mjini leo ifakara! Mungu ibariki CHADEMA, Mungu ibariki Tanzania Amina:
 
Back
Top Bottom