M23 wamtaja Nyerere kama fahari yao

CHAMVIGA

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
7,687
2,238
Wingu zito.

Mtanzania aliyenaswa na M23
Jumatano, Julai 24, Na Ratifa Baranyikwa

*Waasi hao sasa wadai wako tayari kumwachia huru huku wakimtaja Nyerere kuwa fahari yao. WINGU bado linaendelea kutanda, kuhusu ukweli na uhalisia wa madai ya kundi la waasi la M23 la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, linalodaikumshikilia askari anayedaiwa kuwa na uraia wa Tanzania.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti la MTANZANIA Jumatano kuhusu madai hayo ya M23, unaonyesha kuwapo na ukakasi na utata mkubwa kuhusu taarifa hizo ambazo zilianza kusambazwa katika mitandao ya intaneti kuanzia mwishoni mwa wiki iliyopita.

Hata hivyo, wakati maswali yakiongezeka kuhusu sakata hilo, waasi hao wa M23 ambao wamekuwa wakipambana kumng'oa kutoka madarakani, Rais Joseph Kabila bado wanaendelea kupata kigugumizi kueleza iwapo askari wanayemshikilia alikuwa miongoni mwa wanajeshi wa Tanzania wanaounda kikosi cha kulinda amani nchini Kongo au la.
 
Mfa maji,...

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

M23 na Gen. Kagame naona wanakaribia mwisho. Feedback umeona kwamba propaganda za Gen Kagame zimeanza kupata counter attack? Taarifa ya serikali ya Marekani kutamka waziwazi kuitaka Rwanda iache kuwasaidia M23 ni pigo kubwa la kidiplomasia kwa Gen. Kagame. Baada ya kauli ya Marekani sasa ndio mtaona Gen. Kagame anavyoweweseka.
 
Last edited by a moderator:
M23 na Gen. Kagame naona wanakaribia mwisho. Feedback umeona kwamba propaganda za Gen Kagame zimeanza kupata counter attack? Taarifa ya serikali ya Marekani kutamka waziwazi kuitaka Rwanda iache kuwasaidia M23 ni pigo kubwa la kidiplomasia kwa Gen. Kagame. Baada ya kauli ya Marekani sasa ndio mtaona Gen. Kagame anavyoweweseka.

Nimefurahia kauli ya Marekani kwani naona kama Kagame anataka kurudi msituni. Asipojirekebisha atajikuta kwenye wakati mgumu sana kwani mataifa mengi yamemweka kiporo na siku ikifika watamrudia na sijui atakimbilia wapi
 
Mbaona hilo linajulikana kwa muda mrefu kuwa Nyerere alikuwa mtutsi kulingana na kabila la wazanaki maana ya jina (wazanaki) ni kwamba umekuja na nini walikuwa ni jamii ya wafugaji waliokuwa wakizinguka maeneo mbalimbali kwenye ukanda huu wa maziwa ambao kwa sehemu ndiyo watutsi na ndiyo maana Nyerere alikubali kuhakikisha ule mkataba wa kuigawa Congo DRC kwa masilahi ya wahutu ambayo kabila mkubwa aliyaita makubaliano ya porini ambayo ndiyo yanayompa wazimu Kagame na kutaka kuhakikisha kuwa makubaliano yamechukua nafasi na kuwatengenezea watutsi nchi ya ahadi kwa lazima.



Ni ile hoja kuwa Nyerere ni Mhutu, haitasaidia kwa lolote muda huu, Kila mtu akifuatiliwa miaka 100 kurdi nyuma identity yake itakuwa changed kiaina.
 
M23 ni watu wa ajabu mno. Eti wanamsifia nyerere hivi lengo lao hasa ni nini? Au wanataka kutufarakanisha Watanzania kwamba alichofanya Kikwete kupeleka jeshi kulinda amani amekosea?
 
\
Nimefurahia kauli ya Marekani kwani naona kama Kagame anataka kurudi msituni. Asipojirekebisha atajikuta kwenye wakati mgumu sana kwani mataifa mengi yamemweka kiporo na siku ikifika watamrudia na sijui atakimbilia wapi

Alikuwa rafiki wa Marekani lakini sasa Marekani wamemchoka; Wafaransa nao hawako naye; urafiki wake na Uganda ni wa mashaka huku akimpiga Kabila wa Kongo na kuleta maneno yasiyo na maana kwa Tanzania. Mkuu Gen. Kagame hana msitu wa kukimbilia asipojirekebisha. Ngoja tu watu wafufue mauaji ya Habyarimana na Ntaryamira kama Gen. Kagame hatajikuta kwenye misukosuko na Fatouh Bensouda.
 
Ukabila unajadiliwa karne hii?..hivi nyie mpo wapi?acheni upumbavu mataifa makubwamakubwa yanaungana kuua ukabila leo Watanzania tujadili uhutu na ututsi....------- zaidi!....
 
Ukabila unajadiliwa karne hii?..hivi nyie mpo wapi?acheni upumbavu mataifa makubwamakubwa yanaungana kuua ukabila leo Watanzania tujadili uhutu na ututsi....------- zaidi!....

Bwana Viscom. Tanzania hakuna suala ukabila. Utusi na Uhutu upo Rwanda na Kagame anafufua yaliyosahaulika kuhusu mauaji ya Kimbari. Hapa watu wanajadili uhalisia mambo yalivyo kutokana na madai ya Kagame.
 
Last edited by a moderator:
Namtetea kikwete katika hili lakini pia kuna walakini,tutasemaje kagame akae na waasi waongee wakati huohuo tunapeleka jeshi congo,why can't we walk the talk?!
 
Back
Top Bottom