Lusinde aivua nguo Serikali mbele ya Kinana

Lusinde aivua nguo Serikali mbele ya Kinana

Wekeni picha ya lusinde. Wengine hatumfaham
attachment.php

 

Attachments

  • 4.LivingstoneLusindeakisisitizajambo.jpg
    4.LivingstoneLusindeakisisitizajambo.jpg
    46.9 KB · Views: 623
Last edited by a moderator:
Tatizo la Lusinde bangi.... hapo alijisahau akahisi bado yuko CHADEMA ... Mtakumbuka JK alimponda sana kwa jinsi ambavyo wabunge wa CCM walivyokuwa wanawafagilia watuhumiwa wa ESCROW ...
Mbunge wa Mtera kwa tiketi ya CCM,Livingstone Lusinde aka Kibajaji ameivua nguo Serikali ya CCM. Akihutubia mbele ya Katibu Mkuu Kinana jimboni kwake Mtera,Lusinde amesema wananchi wamechoka kudanganywa. Amesema Serikali imezoea kuwadanganya wananchi juu ya mambo ya maendeleo huku Rais akiagiza michango ya lazima ya maabara.

Lusinde alitangaza na kuwataka wananchi wa Mtera kugomea agizo la Rais Kikwete juu ya michango ya maabara. "Ametamba alivyotaka mbele ya Kinana na Kinana hakumjibu wala kuweka mambo sawa. Amesema kuwa Serikali inadanganya watu. Hakika ameonesha jinsi CCM ilivyoshindwa kutekeleza Ilani yake" alisema shuhuda toka Mtera.

Katibu mkuu Kinana umebariki haya ya Lusinde?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Ata saa mbovu atleast kwa dakika moja kwa siku husema ukweli.
 
Hebu tusaidiane kidogo, hivi mbunge analeta maendeleo ama ni muwakilishi wa wananchi wa enoe husika bungeni? Nivuavyo mimi mbunge kazi yake ni kuisimamia na kuishauri serekali. Huwa ninapata shida unaposikia eti mbunge hajaleta maendeleo yoyote. Kazi ya kuleta maendeleo inaletwa na serekali kupitia kodi zet na mbunge kazi yake ni kuhamasisha tu au kuwakikilisha wananchi wake bungeni hasa kusemea matatizo yao.

Kazi ya Mbunge ni kuwahamasisha wananchi wa jimbo lake ili wajitambue na wajiletee maendeleo; mbunge wao anatakiwa kuwa ndio kiongozi wa kuongoza na kuonesha njia ambayo wananchi wa jimbo lake watapita ili wapate maendeleo na sio kwenda bungeni na kutukana matusi!! Serikali ni catalyst tu! Mfano wa mbunge anaewajibika kwa wananchi wa jimbo lake kwa kuwahamasisha ni Deo Filikunjombe ambae anajumuika na wananchi kujenga zahanati,vyumba vya madarasa, visima vya maji na kuwaunganisha kuanzisha SACCOS!!.
 
Hajui siasa na anajiona mbabe kumbe na jamaa wa chini ya reli.Anajaribu kumuigizia Kinana bila ya kujua yule anafanya siasa ya kuangalia wapi kuna makosa ili wajipange vizuri wakati wa kampeni.Ndiyo faida ya kuwa na wasomi....lakini Lusinde shule hakuna basi MATATIZO NA MATUSI
 
Ndio tupo ! mfano mimi huwa namsikiliza kidogo ,kwa kuwa ni jembe la CCM ,Mfano alipopewa dk 30 kuutete uozo wa ESCROW ! Ni muhimu kumsilikliza ili kuwa na uhakika kuwa kuwa kweli CCM CHAMA KILICHOKUWA CHA UKOMBOZI NA MAPINDUZI ,KILICHOASISIWA NA JULIUS NYERERE imekufa ! Wakati mwingine ni kitaka kucheka na kupumzisha akili huwa naingia kwa YOUTUBE NABOFYA ...HOTUBA YA LUSINDE KAMPENI ZA ARUMERU!
Hivi kuna watu huwa wanamsikiliza Lusinde?
 
Mbunge wa Mtera kwa tiketi ya CCM,Livingstone Lusinde aka Kibajaji ameivua nguo Serikali ya CCM. Akihutubia mbele ya Katibu Mkuu Kinana jimboni kwake Mtera,Lusinde amesema wananchi wamechoka kudanganywa. Amesema Serikali imezoea kuwadanganya wananchi juu ya mambo ya maendeleo huku Rais akiagiza michango ya lazima ya maabara.

Lusinde alitangaza na kuwataka wananchi wa Mtera kugomea agizo la Rais Kikwete juu ya michango ya maabara. "Ametamba alivyotaka mbele ya Kinana na Kinana hakumjibu wala kuweka mambo sawa. Amesema kuwa Serikali inadanganya watu. Hakika ameonesha jinsi CCM ilivyoshindwa kutekeleza Ilani yake" alisema shuhuda toka Mtera.

Katibu mkuu Kinana umebariki haya ya Lusinde?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

mkuu vp mafisi nayo yalikuwepo?
 


hii video sikuwahi kupata muda wa kuiangalia hata siku moja.

leo nimeangalia nusu tu....aisee! huyu kijana kweli ni nutcase. kajisemea yeye mwenyewe humo ndani ya video eti yeye ni "kichaa wa kuzaliwa" and I full agree with him...ni kichaa wa kuzaliwa kweli kweli!!

CCM sijui huwa inawaokota wapi watu dizaini hii...
 
Last edited by a moderator:
Watajifanya hawajasikia, si unajua mpaka leo Nape hajapata matokeo ya Songea?
 
Back
Top Bottom