Mbunge wa Mtera kwa tiketi ya CCM,Livingstone Lusinde aka Kibajaji ameivua nguo Serikali ya CCM. Akihutubia mbele ya Katibu Mkuu Kinana jimboni kwake Mtera,Lusinde amesema wananchi wamechoka kudanganywa. Amesema Serikali imezoea kuwadanganya wananchi juu ya mambo ya maendeleo huku Rais akiagiza michango ya lazima ya maabara.
Lusinde alitangaza na kuwataka wananchi wa Mtera kugomea agizo la Rais Kikwete juu ya michango ya maabara. "Ametamba alivyotaka mbele ya Kinana na Kinana hakumjibu wala kuweka mambo sawa. Amesema kuwa Serikali inadanganya watu. Hakika ameonesha jinsi CCM ilivyoshindwa kutekeleza Ilani yake" alisema shuhuda toka Mtera.
Katibu mkuu Kinana umebariki haya ya Lusinde?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam