Yaani inapendeza mpaka raha.Wiki iliyopita mpaka sasa kumetokea mabadiko makubwa ya kisiasa jimboni Kalenga ambayo pamoja na kazi kubwa inayo endelea kufanywa na makanda,sababu kubwa za mabadiliko hayo ni Hotuba ya M/kiti wa ccm taifa dhidi ya rushwa ndani ya ccm,Kukamatwa na kuhusika mwana ofisi ya Mbunge Lukuvi na kashfa ya Kuuza meno ya Tembo ni sababu ambazo zimefanya chadema sasa kung'ara kwa kuwa kimejionesha ukweli,na nzuri zaidi waziri kivuli wa utalii na maliasili yupo hapa Iringa na ameongeza point kwa kauli yake "WAPO VIGOGO WA CCM NA SERIKALI WANAHUSIKA NA BIASHARA YA MENO YA TEMBO".HAYAWI HAYAWI YAMEKUWA,MKIA ULIOBAKI KUMALIZIA NG'OMBE' ccm ni kazi ndogo sana kwetu wanachadema,ila tusibweteke,nayo ni kujenga msingi imara wa nyumba chadema.KAZI HII NDIYO INAYOFANYWA HAPA JIMBO LA KALENGA AMBAPO JUMLA YA VIJANA 180 Kutoka vyuo vikuu mbalimbali wanafanya kazi kwenye vijiji,vitongoji na familia vya jimbo la Kalenga.MWENDO MDUNDO CHADEMA.