Siku ya Ijumaa waliokuwa wakifuatilia Kikao cha Bunge kinachoendelea Dodoma, Mbunge wa CHADEMA Mh. Msigwa wakati wa kuchangia aliishauri serikali kupunguza matumizi ikiwemo kupunguza misafara ya Waziri isiwe mikubwa sana.Alisema alichokiona ilinga kuwa msafara wa Waziri Mkuu unakuwa na Magari zaidi ya 50, Baada ya kusema hilo alishambuliwa vibaya sana haswa na Wabunge wa CCM, yeye Lukuvi akasema msigwa ni muongo sana huku akikejeli kuwa hafai kuwa mchiungaji, na wengine wakisema waongo hawataingia ufalme wa MunguKejeli na dharau za kila aina zilitolewa siku hizo zikimlenga Mtumishi wa Mungu Mh. Msigwa.Nimeshangaa leo Mbunge wa Nkenge Mh. Assumpter akisema nawashangaa wengine wakilalamika kuwa msafara wa Waziri Mkuu unakuwa mkubwa sana, akasema sisi kwetu alikuja na Magari zaidi ya 50 na siku hiyo ilikuwa ni heshima kubwa sana kwa Waziri wetu mkuu tumpendaye, ni haki yake bwana.Itakuwa ni ungwana kama Mh. Lukuvi atamuomba msamaha Mh. Msigwa kwa maneno mabaya aliyomrushia siku ile ,pia wabunge wengine wamuombe msamaha Mh. Msigwa isije ikageuka wao ndo wasiuone ufalme wa Mungu kwa kumnena vibaya mtumishi wa Mungu, aliyoyasema leo Mbunge wa Nkenge yanadhibitisha kuwa Mh. Msigwa alikuwa sahihi.